< Leviticus 6 >

1 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana akamwambia Mose:
2 “If any one of you you sins against me by deceiving someone—if you refuse to return what someone has lent you, or if you steal something of his, or if you find something and claim that you do not have it,
“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
3 you are guilty. You must return to its owner what you have stolen or what someone has lent you and you have not returned, or what you found that someone else had lost,
au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
4 or whatever you lied about.
wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
5 You must not only return anything like that to its owner, but you must also pay to the owner one-fifth of its value.
au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
6 You must also bring to the Supreme Priest a ram to be an offering to me in order that you will no longer be guilty. The ram that you bring must be one that has no defects, one that has the value that has been officially determined.
Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
7 Then he will offer that ram to be a sacrifice that will cause you to no longer be guilty, and you will be forgiven for the wrong things that you did.”
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
8 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana akamwambia Mose:
9 “Tell this to Aaron and his sons: These are the regulations concerning the offerings that will be completely burned [on the altar]: The offering must remain on the altar all during the night, and the fire on the altar must always be kept burning.
“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
10 [The next morning] the priest must put on his linen under-clothes and linen outer clothes. Then he must remove the ashes of the offering from the fire and put them beside the altar.
Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
11 Then he must take off those clothes and put on other clothes, and take the ashes outside the camp, to a place that is acceptable to me.
Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
12 The fire on the altar must always be kept burning; the priest must not allow it to (go out/quit burning). Each morning the priest must put more firewood on the fire. Then he must arrange more offerings on the fire, and burn on the altar the fat of the offerings to be burned to maintain fellowship [with me].
Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
13 The fire on the altar must be kept burning continually; the priest must not allow it to go out.”
Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
14 “These are the regulations concerning the offerings made from grain: Aaron’s sons must bring them to me in front of the altar.
“‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
15 The priest must take a handful of fine flour mixed with olive oil and incense and burn that on the altar. That handful will signify that the whole offering truly belongs to me. And the aroma while it burns will be pleasing to me.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
16 Aaron and his sons may eat the remaining part of the grain offering. But they must eat it in a holy place, in the courtyard of the Sacred Tent.
Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
17 It must not have yeast mixed with it. Like the offerings for sin and the offerings to cause people to no longer be guilty of sin, that offering is very holy.
Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
18 Any male descendants of Aaron are permitted to eat it, because it is forever their regular share of the offerings given to me and burned in the fire [on the altar]. Anyone else who touches those offerings made from grain will be punished by God.”
Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
19 Yahweh also said to Moses/me,
Tena Bwana akamwambia Mose,
20 “Tell Aaron and his sons that this is the offering that they must bring to Yahweh on the day that any of them (is ordained/becomes a priest): That person must bring two quarts/liters of fine flour as an offering made from grain. He must bring half of it in the morning and half of it in the evening.
“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
21 He must mix it well with olive oil and bake it in a shallow pan. He must then break it into small pieces to be burned [on the altar]. And the aroma while it burns will be pleasing to Yahweh.
Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
22 I have commanded that the descendants of Aaron who are appointed in turn to become the Supreme Priests after Aaron dies are the ones who must prepare those things. These offerings must be completely burned [on the altar] to be sacrifices to me, Yahweh.
Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
23 Every offering that a priest gives that is made from grain must be completely burned; none of it is to be eaten.”
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
24 Yahweh also said to Moses/me,
Bwana akamwambia Mose,
25 “Tell Aaron and his sons: These are the regulations concerning the offerings that people must bring to me so that I will forgive the people for the sins they have committed:
“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
26 The animals must be slaughtered in my presence in the same place that the animals that are to be completely burned [on the altar] are slaughtered, in the courtyard in front of the Sacred Tent.
Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
27 Any other person who touches any of its meat will be punished by God. And if its blood is splattered on your clothes, you must wash the clothes in a holy place.
Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
28 If the meat is cooked in a clay pot, the pot must be broken [afterwards]. But if it is cooked in a bronze pot, the pot must be scoured [afterwards] and rinsed with water.
Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
29 Any male in a priest’s family may eat some of the cooked meat; that meat is very holy.
Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
30 But if the blood of those sin offerings is brought into the Sacred Tent to enable the people to be forgiven for having sinned, the meat of those animals must not be eaten. The meat must be completely burned.”
Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.

< Leviticus 6 >