< Leviticus 15 >
1 Yahweh also said to Moses/me and Aaron,
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
2 “Tell this to the Israelis: When an infected discharge comes out of a man’s sexual organs [EUP], that fluid should not be touched.
“Waambie watu wa Israeli, na sema kwao, 'Wakati mtu yeyote kisonono kimemwathiri mwili wake unatoa ugiligili, anakuwa najisi.
3 Whether that fluid is blocked or continues to drip, it causes him to be someone who should not be touched.
Unajisi wake unatokana na athari ya kisonono. Iwe mwili wake unatoa ugiligili au umekoma, huo ni unajisi.”
4 “And any bed that such a man lies on should not be touched, and anything that he sits on should not be touched.
Kitanda chochote anachokilalia kitakuwa najisi, na kila kitu ambacho anakaa juu yake kitakuwa najisi.
5 Anyone who touches that person’s bed must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na awe amenajisika mpaka jioni.
6 Anyone who sits on something that man has sat on must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Yeyote anayekaa katika kitu chochote ambacho mtu ambaye ameathiriwa na kisonono alikaa, mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
7 “Anyone who touches such a man must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Na yeyote anayegusa mwili wa ambaye ameathirika na kisonono lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na awe najisi hadi jioni.
8 “If such a man spits on someone else, that person who is spit upon should not be touched. He must wash his clothes, and no one should touch him until that evening.
Kama mtu ambaye anaona majimaji kama hayo kwa mtu fulani ambaye ametakasika, ndipo mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na atakuwa najisi hata jioni.
9 “Everything that a man who has such a discharge of fluid sits on while he is riding [a horse or a donkey] should not be touched,
Tandiko lolote ambalo ambaye anamajimaji ya kisonono atalikalia litakuwa najisi.
10 and anyone who touches the seat or saddle that he was sitting on also should not be touched until that evening. And anyone who picks up the seat or saddle must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Yeyote anayegusa kitu chochote kilichokuwa chini ya mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji; atanajisika mpaka jioni.
11 Anyone whom the man with such a discharge of fluid from his body touches without first rinsing his hands in water must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Ambaye anamajimaji kama hayo akimgusa kabla kwanza ya kuosha kwa maji safi mikono yake, mtu aliyeguswa lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
12 “If such a man touches a clay pot, that pot must be broken into pieces. Anything made from wood that he touches must be rinsed in water.
Chungu chochote cha udongo ambacho ambaye anamajimaji kama hayo akigusa lazima kivunjwe, na kila chombo cha mti lazima kioshwe na maji safi.
13 “If such a man is healed from his flow of fluid, he must wait for seven days. Then he must wash his clothes and bathe in water from a spring. Then he will be able to be with others.
Wakati mwenye kisonono anapotakaswa katika kisonono chake, ndipo lazima ahesabu kwaajili yake siku saba kwaajili ya kutakasika kwake; ndipo afue nguo na aoshe mwili wake kwenye maji yatiririkayo. Ndipo atakuwa safi.
14 On the eighth/next day, he must take two doves or two young pigeons and come in front of Yahweh at the entrance of the Sacred Tent, and give them to the priest.
Katika siku ya nane lazima achukue njiwa wawili au kinda mbili za njiwa na aje mbele za Yahwe pakuingilia kwenye hema ya mkutano; pale lazima atoe hao ndege kwa kuhani.
15 The priest will sacrifice them. One will be an offering for the man to become acceptable to God, and the other one will be completely burned [on the altar]. As a result of the priest doing that, the man will be forgiven for having sinned.
Lazima kuhani awatoe, moja kama sadaka ya dhambi na nyingine kama ya kuteketezwa, na kuhani lazima afanye upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe kwaajili ya kisonono chake.
16 “Then semen accidentally flows from a man’s sexual organs [EUP], he must bathe his whole body, and no one should touch him until that evening.
Kama mtu yeyote ametokwa na shahawa, ndipo lazima aoge mwili wake wote katika maji; atanajisika mpaka jioni.
17 Any clothing or leather that has semen on it must be washed, and no one should touch it until that evening.
Kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa lazama paoshwe kwa maji; itakuwa najisi mpaka jioni.
18 When a man has sex with a woman and some semen spills, both of them must bathe, and no one should touch them until that evening.
Na kama mwanamke na mwanaume watalala pamoja na kunakutokwa kwa shahawa kwenda kwa mwanamke, lazima wote wawili waoge katika maji; watakuwa najisi mpaka jioni.
19 “Then a woman has her monthly menstrual period, no one should touch her for seven days. If anyone touches her [during that time], no one should touch the person who touched her until that evening.
Mwanamke anapokuwa kwenye hedhi, ataendelea kunajisika kwa siku saba, na yeyote anayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 No one should touch anything that she lies on or sits on during that time.
Chochote anacholala juu yake wakati wa hedhi kitakuwa najisi; kila kitu ambacho anakalia kitakuwa pia najisi.
21 Anyone who touches her bed must wash his clothes and bathe, and no one should touch that person until that evening.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
22 Anyone who touches something that she has been sitting on, a bed or anything else, must wash his clothes, and no one should touch that person until that evening.
Yeyote anayegusa chochote ambacho amekikalia lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo anakuwa najisi mpaka jioni.
Iwe juu ya kitanda au kitu chochote juu ya popote atakapokaa, kama akikigusa, mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
24 “If a man has sex with a woman [during that time] and some of the menstrual blood touches him, no one should touch him for seven days, and no one should touch the bed that he lies on.
Kama mwanaume yeyote akilala naye, na unajisi wa mwanamke ukamgusa, atakuwa amenajisika siku saba. Kila kitanda ambacho anakilalia mwanaume huyo kitanajisika.
25 “Then a woman has a vaginal discharge of blood for (many days/a long time), which is not her monthly flow of blood, or if her flow of blood continues after her monthly flow ends, no one should touch her until it stops.
Kama mwanamke ametokwa damu kwa siku nyingi ambayo siyo kipindi cha hedhi yake, au ikitoka zaidi ya kipindi chake cha hedhi, wakati wote wa siku za kunajisika, atakuwa kama alikuwa kwenye siku zake za hedhi. Yeye ni najisi.
26 And no one should touch the bed that she lies on or anything that she sits on while that flow of blood continues, just like during her monthly menstrual period.
Kila kitanda anachokilalia wakati wote wa kutokwa damu itakuwa kwake sawa tu kama kitanda anacholalia wakati wa hedhi, na kila kitu ambacho anakalia kitakuwa najisi, kama tu unajisi wa hedhi yake.
27 Anyone who touches those things should not touch anyone else; he must wash his clothes and bathe, and he should not touch anyone else until that evening.
Na yeyote anayegusa kitu kati ya vitu hivyo atakuwa najisi; lazima yeye afue nguo zake na aoge mwenyewe kwenye maji, na atakuwa amenajisika mpaka jioni.
28 “After a woman’s monthly menstrual flow ends, she must wait seven days before she touches anyone.
Lakini kama mwanamke ametakasika katika kutokwa na damu, ndipo atahesabu kwaajili yake siku saba, baada ya hizo atakuwa safi.
29 On the eighth/next day, she must take two doves or two pigeons to the priest at the entrance of the Sacred Tent.
Katika siku ya nane atachukua kwake njiwa wawili au kinda wawili wa njiwa na atawaleta kwa kuhani pakuingilia hema ya mkutano.
30 The priest will sacrifice one of them to be an offering to enable her to become acceptable to Yahweh again, and completely burn the other one [on the altar]. By doing that he will cause me, Yahweh, to forgive her for having sinned [DOU].
Huyo kuhani atatoa ndege mmoja kama sadaka ya dhambi na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa, na atafanya upatanisho kwaajili ya huyo mbele ya Yahwe kwaajili unajisi wa mwanamke atokwaye damu.
31 “You must warn the Israeli people not to do things that (defile them/cause them to be unacceptable to me). If they become (unacceptable to me/defiled), they will cause my Sacred Tent which is among them to become an unacceptable place to worship me, and as a result they will die.”
Hivi ndivyo lazima uwatenge watu wa Israeli katika unajisi wao, hivyo hawatakufa tokana na unajisi wao, kwa kuchafua hema langu, ambapo naishi kati yao.
32 “Those are the regulations for a man who has a fluid that flows from his sexual organs or who should not be touched because some of his semen spills out while having sex [with a woman],
Huu ndio utaratibu kwa kila ambaye anakisonono, kwaajili kila mwanaume ambaye shahawa yake inatoka na inamfanya kuwa najisi,
33 and for any woman during her monthly menstrual period, and for any man who has sex with a woman during her menstrual period.”
kwaajili ya mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha hedhi, kwaajili ya yeyote aliye na kisonono, awe mwanaume au mwanamke, na kwaajili ya yeyote anayelala na mwanamke najisi.