< Leviticus 15 >
1 Yahweh also said to Moses/me and Aaron,
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
2 “Tell this to the Israelis: When an infected discharge comes out of a man’s sexual organs [EUP], that fluid should not be touched.
“Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.
3 Whether that fluid is blocked or continues to drip, it causes him to be someone who should not be touched.
Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:
4 “And any bed that such a man lies on should not be touched, and anything that he sits on should not be touched.
“‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi.
5 Anyone who touches that person’s bed must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
6 Anyone who sits on something that man has sat on must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
7 “Anyone who touches such a man must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
“‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
8 “If such a man spits on someone else, that person who is spit upon should not be touched. He must wash his clothes, and no one should touch him until that evening.
“‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
9 “Everything that a man who has such a discharge of fluid sits on while he is riding [a horse or a donkey] should not be touched,
“‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi,
10 and anyone who touches the seat or saddle that he was sitting on also should not be touched until that evening. And anyone who picks up the seat or saddle must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
11 Anyone whom the man with such a discharge of fluid from his body touches without first rinsing his hands in water must wash his clothes and bathe, and no one should touch him until that evening.
“‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
12 “If such a man touches a clay pot, that pot must be broken into pieces. Anything made from wood that he touches must be rinsed in water.
“‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.
13 “If such a man is healed from his flow of fluid, he must wait for seven days. Then he must wash his clothes and bathe in water from a spring. Then he will be able to be with others.
“‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika.
14 On the eighth/next day, he must take two doves or two young pigeons and come in front of Yahweh at the entrance of the Sacred Tent, and give them to the priest.
Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani.
15 The priest will sacrifice them. One will be an offering for the man to become acceptable to God, and the other one will be completely burned [on the altar]. As a result of the priest doing that, the man will be forgiven for having sinned.
Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.
16 “Then semen accidentally flows from a man’s sexual organs [EUP], he must bathe his whole body, and no one should touch him until that evening.
“‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
17 Any clothing or leather that has semen on it must be washed, and no one should touch it until that evening.
Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni.
18 When a man has sex with a woman and some semen spills, both of them must bathe, and no one should touch them until that evening.
Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.
19 “Then a woman has her monthly menstrual period, no one should touch her for seven days. If anyone touches her [during that time], no one should touch the person who touched her until that evening.
“‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 No one should touch anything that she lies on or sits on during that time.
“‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi.
21 Anyone who touches her bed must wash his clothes and bathe, and no one should touch that person until that evening.
Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
22 Anyone who touches something that she has been sitting on, a bed or anything else, must wash his clothes, and no one should touch that person until that evening.
Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.
24 “If a man has sex with a woman [during that time] and some of the menstrual blood touches him, no one should touch him for seven days, and no one should touch the bed that he lies on.
“‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.
25 “Then a woman has a vaginal discharge of blood for (many days/a long time), which is not her monthly flow of blood, or if her flow of blood continues after her monthly flow ends, no one should touch her until it stops.
“‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake.
26 And no one should touch the bed that she lies on or anything that she sits on while that flow of blood continues, just like during her monthly menstrual period.
Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi.
27 Anyone who touches those things should not touch anyone else; he must wash his clothes and bathe, and he should not touch anyone else until that evening.
Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
28 “After a woman’s monthly menstrual flow ends, she must wait seven days before she touches anyone.
“‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada.
29 On the eighth/next day, she must take two doves or two pigeons to the priest at the entrance of the Sacred Tent.
Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
30 The priest will sacrifice one of them to be an offering to enable her to become acceptable to Yahweh again, and completely burn the other one [on the altar]. By doing that he will cause me, Yahweh, to forgive her for having sinned [DOU].
Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.
31 “You must warn the Israeli people not to do things that (defile them/cause them to be unacceptable to me). If they become (unacceptable to me/defiled), they will cause my Sacred Tent which is among them to become an unacceptable place to worship me, and as a result they will die.”
“‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu, ambayo yapo katikati yao.’”
32 “Those are the regulations for a man who has a fluid that flows from his sexual organs or who should not be touched because some of his semen spills out while having sex [with a woman],
Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa,
33 and for any woman during her monthly menstrual period, and for any man who has sex with a woman during her menstrual period.”
kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.