< Lamentations 4 >

1 [Previously our people were like] [MET] pure gold, but now they are worthless. [Like] [MET] the sacred stones in the temple have been scattered, [our young men have been scattered].
Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
2 The young men of Jerusalem were as valuable as [MET] large amounts of gold, but now people consider that they are as worthless as [ordinary] clay pots.
Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
3 Even the [female] jackals/wolves feed their pups, but my people act cruelly [toward their children]; they are like [SIM] ostriches in the desert [that abandon their eggs].
Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
4 [My people’s] infants’ tongues cling to the roofs/tops of their mouths because they are [extremely] thirsty; the children plead for some food, but no one gives them [any].
Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
5 People who [previously] ate fine food are [now] starving in the streets; those who previously lived luxuriously [MTY] [now] paw/dig through rubbish heaps [to find some food].
Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
6 [The people of] Sodom were struck with a disaster very suddenly, and there was no one to rescue them; but my people have been punished more severely than [the people of] Sodom were punished.
Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
7 Our leaders’ [behavior] was [previously] very pure, whiter [and brighter] than snow and milk; their bodies were redder than [red] coral/stones; they were very strong and healthy [MET].
Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
8 But now their faces are blacker than soot, and no one recognizes them in the streets. Their skin has shriveled on their bones, and it has become as dry as [SIM] a wooden [stick].
Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
9 It is better to die in a battle [MTY] than to die of hunger. There was no food to harvest in the fields, so the people slowly starved until they died.
Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
10 Women who [usually/previously] were very kind have [killed and] cooked their own children; they ate them [when there was no other food], when Jerusalem was surrounded [by enemy soldiers].
Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
11 Yahweh has shown that he was extremely angry; [it is as though] he started/ignited a fire in Jerusalem that burned everything to ashes.
Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
12 None of the kings on the earth or anyone else believed that any of our enemies could enter the gates of Jerusalem.
Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
13 [But that is what happened]; it happened because the prophets sinned; and the priests [also] sinned by causing innocent people to be executed [MTY].
Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
14 The prophets and priests wandered through the streets [as though they were] blind. No one would touch them because their clothes were stained with the blood [of people who had been killed].
Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
15 The people [who were alive] shouted, “Stay away [from us] [DOU]! You are defiled/untouchable! Do not touch us!” So the prophets and priests fled [from Israel], and they wandered around from one country to another, because people [in each country] kept saying to them, “You cannot stay here!”
Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
16 It is Yahweh himself who has scattered them; he no longer is concerned about them. People do not respect [our] priests or leaders.
Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
17 We [SYN] continued to look for someone to help [us], but it was useless. We continued to watch to see if one of our allies would save us, but none of the nations that we were waiting for could help [us].
Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
18 [Our] enemies were hunting for us, so we could not [even] walk in our streets [lest they seize us]. We were about to be captured; it was time for us to be killed.
Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
19 Those who pursued us were faster than eagles [flying] in the sky. Even if we fled to the mountains or hid in the desert, they [went there ahead of us and] waited [to attack] us.
Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
20 [Our king, ] whom Yahweh appointed, was the one who enabled us to remain alive [MTY]; he was the one whom we trusted to protect us [IDM] from [the armies of] other nations. But he was [captured] [like animals are] [MET] caught in a pit.
Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
21 You people of [IDM] Edom and Uz, [you may] be happy [about what is happening to us now], but [Yahweh] will be punishing [MTY] you [also]. You will become drunk and will be ashamed [because your enemies] will have stripped off your clothes.
Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
22 You [people of] [APO] Jerusalem, the time of your being punished will end; Yahweh will not allow you to continue to live in (exile/foreign countries). But [you people of] [APO] Edom, Yahweh will punish [you]; he will reveal the wicked things that you have done.
Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.

< Lamentations 4 >