< Judges 16 >

1 One day Samson went to Gaza [city in the Philistia area]. He spent some time with a prostitute.
Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake.
2 People soon found out that Samson was there, so the men of Gaza gathered together at the city gate and waited all night. They said to themselves, “When it dawns tomorrow morning, we will kill him [when he tries to leave the city].”
Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”
3 But Samson did not stay there all night. At midnight, he got up. He went to the city gate, he took hold of its two posts, and he lifted it up out of the ground, with its [connecting cross] bar still attached. He put it on his shoulders and carried it [many miles] uphill to Hebron.
Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
4 Later Samson fell in love with a woman named Delilah, [and started to live with her]. She lived in Sorek Valley [in the Philistia area].
Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila.
5 The Philistine leaders went to her and said, “Find out from Samson what makes him so strong. And find out how we can subdue him and tie him up securely. If you do that, each of us will give you 1,100 pieces of silver.”
Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”
6 So Delilah said to Samson, “Please tell me what makes you so strong, and tell me how someone can subdue you and tie you up.”
Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”
7 Samson said, “If someone ties me with seven new bowstrings, ones that are not dry yet, I will become as weak as other men.”
Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
8 So [after Delilah told that to the Philistine leaders], they brought seven new bowstrings to Delilah.
Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni.
9 Then she hid the men in one of the rooms in her house. Then [while Samson was sleeping], she tied him up with the bowstrings. Then she called out, “Samson! The Philistines have come here to capture you!” But Samson snapped the bowstrings as easily as though they were strings that had been singed in a fire. So the Philistines did not find out what made Samson so strong.
Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.
10 Then Delilah said to Samson, “You have deceived me and lied to me! Now tell me [the truth, ] how someone can tie you up securely.”
Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”
11 Samson replied, “If someone ties me with new ropes, ones that have never been used, I will be as weak as other men.”
Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
12 So again, [she told the Philistine leaders, and] they [came and] hid in the room as they had done before. And again, while Samson was sleeping, she took the new ropes and tied him up with them. Then she called out, “Samson! The Philistines have come to capture you!” But Samson snapped the ropes on his arms as easily as if they were threads.
Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.
13 Then Delilah said, “You have deceived me and lied to me [again]! Please tell me how someone can tie you up securely!” Samson replied, “If you weave the seven braids of my hair into the threads you are weaving on the loom, and then fasten those threads with the pin [that makes the threads tight], then I will be as weak as other men.” So again, while Samson was sleeping on her lap, Delilah held the seven braids of his hair, and wove them into the threads on the loom,
Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo,
14 and she tightened them with the pin. Then she called out, “Samson! The Philistines have come to capture you!” But Samson woke up and pulled out the pin, and pulled his hair from the threads on the loom.
na kuvikaza kwa msumari. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.
15 Then Delilah said to him, “How can you say that you love me when you do not tell me the truth about yourself? You have deceived me three times, and you still have not told me what really makes you so strong!”
Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.”
16 Day after day she nagged him like that. He thought he would die from her nagging [IDM].
Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.
17 Finally Samson told her the truth. He said, “I have been set apart for God since the day I was born. And because of that, my hair has never been cut. If my hair were shaved off, my strength would be gone, and I would be as weak as other men.”
Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”
18 Delilah realized that this time he had told her the truth. So she summoned the Philistine leaders again, saying, “Come back one more time, because Samson has really told me everything [about why he is so strong]”. So the Philistine leaders returned and brought to Delilah the money [that they promised to give her].
Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao.
19 Again she lulled Samson to sleep, with his head in her lap. Then she called one of the Philistine men to come and shave off Samson’s hair. As he did that, Samson began to get weaker. And finally his strength was all gone.
Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.
20 Then [after she tied him up], she called out, “Samson! The Philistines have come to capture you!” He woke up and thought, “I will do as I did before. I will shake [these ropes] off myself and be free!” But he did not realize that Yahweh had left him.
Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!” Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.
21 So the Philistine men seized him and gouged out his eyes. Then they took him to Gaza. There they put him in prison and bound him with bronze chains. They made him [turn a millstone to] grind grain [every day].
Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani.
22 But his hair started to grow again.
Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.
23 [Several months later] the Philistine leaders celebrated a big festival. During the festival they offered sacrifices to their god Dagon. They praised him, saying, “Our god has enabled us to defeat our great enemy Samson!”
Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”
24 And when the other people saw Samson, they also praised their god Dagon, saying, “Samson ruined our crops and killed many of our people, but our god has put our enemy into our hands. Our god helped us to capture the one who has killed so many of us!”
Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema: “Sasa mungu wetu amemtia adui yetu mikononi mwetu, yule aliyeharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”
25 By that time the people were half-drunk. They shouted, “Bring Samson out of the prison! Bring him here so that he can entertain us!” So they brought Samson from the prison and made fun of him. Then they made him stand in the center of the temple. They made him stand between the two pillars that held up the roof.
Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao. Wakamweka kati ya nguzo mbili.
26 Samson said to the servant who was leading him by his hand, “Place my hands against the two pillars. I want to rest against them.”
Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.”
27 At that time the temple was full of men and women. All the Philistine leaders were also there. And there were about 3,000 people on the roof, watching Samson and making fun of him.
Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza.
28 Then Samson prayed, saying, “Yahweh, my Lord, think about me again! Please give me strength one more time, so that I may get revenge on the Philistines for gouging out my eyes!”
Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.”
29 Then Samson put his hands on the two center pillars of the temple. He put his right hand on one pillar and his left hand on the other pillar.
Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto.
30 Then he shouted [to God], “Let me die with the Philistines!”, and he pushed with all his strength. [The pillars collapsed], and the temple crashed down on the Philistine leaders and all the other Philistine people, [and they all died]. So Samson killed more people when he died than he had killed all during his life.
Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.
31 Later his brothers and their relatives went down [from Zorah to Gaza] to get his body. They took it back home and buried it between Zorah and Eshtaol, at the place where Samson’s father Manoah was buried. Samson had been Israel’s leader for 20 years.
Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.

< Judges 16 >