< John 8 >

1 But Jesus went [with us disciples] to Olive [Tree] Hill [and we stayed near there that night].
lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
2 Early the next morning, we returned to the Temple [courtyard]. Many people gathered around Jesus, so he sat down to teach them.
Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
3 Then men who taught the [Jewish] laws and some of [SYN] the Pharisee [religious group] brought a woman to him. She was seized {[They] had [arranged to] seize her} while she was having sex with a man who was not her husband. They made her stand up in front of the group [that was listening to Jesus].
Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
4 Then they said to Jesus, “Teacher, this woman was seized {[we] seized this woman} while she was having sex with a man who is not her husband.
Kisha wakamwuliza Yesu, “Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
5 Moses commanded us in the laws that [he gave us] that we should throw stones at such women [and kill them]. So what do you say [we should do]?”
Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?”
6 They asked this question as a trap so that they could accuse him. [If he said that they should not kill her, they would shame him for disobeying the law of Moses. If he said that they should kill her, they could accuse him to the Roman governor]. But Jesus bent down and wrote something on the ground with his finger.
Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
7 While they continued to question him, he stood up and said to them, “Whichever one of you has never sinned can be the first one to start throwing stones at her.”
Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, “Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.”
8 Then he stooped down and wrote [some more] on the ground.
Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
9 After they heard what he said, those [who were questioning him] went away, one by one, the older ones first [and then the younger ones, knowing they were all sinners]. Finally only Jesus was there, along with the woman.
Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
10 Jesus stood up and asked her, “Woman, where are they? Has no one said you must die for your sin?”
Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, “Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
11 She said, “No, sir, no one.” Then Jesus said, “I do not condemn you either. Go [home] now, and do not continue your sinful [life] any longer!”]
Huyo mwanamke akamjibu, “Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!” Naye Yesu akamwambia, “Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena.”
12 Jesus spoke to the people again. He said, “I am [like] a light [MET] for [all the people in] [MTY] the world. [Just like a light reveals what has been in the darkness] [MET], [I reveal God’s truth to them]. Those who walk in the darkness [are unaware of what is around them]. But those who become my disciples will always be aware [of God’s truth] [MET]. They will have my light [which shows them how to have eternal] life.”
Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima.”
13 So the Pharisees said to him, “You are just telling about yourself! [Since there is no one else to verify these things that you say about yourself], [we] do not [need to accept that] what you say is true.”
Basi, Mafarisayo wakamwambia, “Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali.”
14 Jesus replied, “Even if I were the [only one to] say these things about myself, what I say is true, because I know that I came from [heaven], and I know that I am going [back to heaven]. But you do not know where I came from or where I am going.
Yesu akawajibu, “Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 You judge people according to human standards. [The reason] that I am [here is] not (to condemn people/to say that I will punish people) [for their sins].
Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
16 But if I did judge [people], what I decided would be correct, because I am not the [only] one [who will decide those things]. I and the one who sent me will both decide.
Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
17 It is written {[Moses] wrote} in your law that if [at least] two people testify that [some event has happened], [people should consider] that what they say is true.
Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
18 I am telling you about myself, and the other one who is telling you about me is [my] Father who sent me. [So you should believe that what we declare is true].”
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia.”
19 Then they asked him, “[If you have a] father whom [we can question about you], where is he?” Jesus replied, “You do not know [who] I [really am]. If you knew who I [really am], you would know who my Father is also.”
Hapo wakamwuliza, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu “Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
20 He said these things when he was in the Temple [courtyard], near the place where the people put their offerings. [This was also very close to the place where the Jewish council met]. But no one seized him to arrest him, because it was not yet time [MTY] [for him to suffer and die].
Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
21 Jesus also said to them, “I [will soon be] going away. Then [at the end of your life] you will seek me, but you will die [without God forgiving] your sins. Where I will go, you will not be able to come.”
Yesu akawaambia tena, “Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika.”
22 So the Jewish [leaders] said among themselves, “Is he going to kill himself? Is that the reason that he said, ‘Where I go, you will not be able to come’?”
Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?”
23 But Jesus continued by saying to them, “You were born here in this world, but I came from heaven. You belong to those who are opposed to God [MTY]. I do not belong to them.
Yesu akawaambia, “Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 I told you that you will die [without God forgiving] your sins. If you do not believe that I am [who I say that I am], you will die [without God forgiving] your sins.”
Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu.”
25 So they said to him, “You! Who do you think you are?” Jesus said to them, “Ever since I began [teaching], I have been telling you who I am!
Nao wakamwuliza, “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu, “Nimewaambieni tangu mwanzo!
26 I could judge you and say that [you are guilty of] many things. But instead, [I will say only] what the one who sent me tells me to say. [What he says] is true, and I tell the people in the world [MTY] what I have heard from him.”
Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 They did not understand that he was talking about his Father [in heaven].
Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
28 So Jesus said, “I am the one who came down from heaven, but when you lift me up [on a cross to kill me], you will know who I am. You will also know that I do not do anything with my own [authority]. Instead, I say just what [my] Father has taught me.
Basi, Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
29 He is the one who sent me, and he helps me. Because I always do the things that please him, he has never abandoned me.”
Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”
30 As Jesus was saying these things, many people believed that he [was] ([from God/the Messiah]).
Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
31 Then Jesus said to the Jews who now said they believed in him, “If you continue to [live in accordance with] my message, you will truly be my disciples.
Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32 Then you will know [God’s] truth, and as a result of [your believing his] truth, he [PRS] will free you [from being controlled by the one who has made you his slaves].”
Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
33 They replied to him, “We are descendants of Abraham. We have never been anyone’s slaves. So why do you say [we will] be freed [from being someone’s slaves]?”
Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?”
34 Jesus replied, “Listen carefully to what I am going to tell you. All those who continue to sin are [forced to obey] their sinful desires [MET], [just like] a slave [is forced to obey his master].
Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 A slave is not a permanent member of a family. But a son is a member of a family forever. [Similarly, you say you are members of God’s family because you are descendants of Abraham, but really, because you are like slaves of your sinful desires, you are no longer permanent members of God’s family]. (aiōn g165)
Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu. (aiōn g165)
36 So if you allow me to free you, you will truly be free.
Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
37 I know that you are Abraham’s descendants. But you are trying to kill me because [you are not] allowing [PRS] my message to continue [to change] your inner being.
Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
38 I am telling you what I saw when I was with [my] Father. But you do the things that you have heard from your father.”
Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu.”
39 They replied to him, “Abraham is our ancestor.” Jesus said to them, “If you were Abraham’s descendants, [your character would be like Abraham’s character, and] you would do [good] things like Abraham did.
Wao wakamjibu, “Baba yetu ni Abrahamu!” Yesu akawaambia, “Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
40 I have been telling you the truth that I heard from God, but you are trying to kill me. Abraham did not do things like that.
Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
41 No! You are doing the things that your [real] father does.” They said to him, “[We do not know about you, but] we are not illegitimate children. And [spiritually], we have only one Father. That is God, and you do not know who your father is!”
Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu.” Wao wakamwambia, “Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu.”
42 Jesus said to them, “If God were your father, you would love me, because I came from God, and now I have come here [to this world]. My coming was not (because I [appointed] myself/with my own [authority]). He sent me.
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 (And I will tell you why you do not understand what I say./Do you know why you do not understand what I say?) [RHQ] It is because you do not want to accept my message.
Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
44 You belong to your father, (the devil/Satan), and you desire to do what he wants. He has [caused people to become] murderers from the time when [people] first [sinned]. He has abandoned [God’s] truth because he is a liar by his nature. Whenever he lies, he is speaking according to his [nature], because he is a liar and is the one who originates [MET] all lies.
Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
45 But because I tell you the truth, you do not believe me!
Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
46 [Since I have never sinned], (none of you can show that I have sinned./can anyone among you show that I have sinned?) [RHQ] So, since I tell you the truth, (there is no good reason for your not believing me!/why is it that you do not believe me?) [RHQ]
Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
47 Those who belong to God habitually obey God’s message. You do not belong to God, so you do not obey his message.”
Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu.”
48 The Jewish [leaders] [SYN] replied to him, “(We are certainly right by saying that you [believe what is false as] the Samaritans [do]!/Are we not right by saying that you [believe what is false as] the Samaritans [do]?) [RHQ] And that (a demon/an evil spirit) [controls] you!”
Wayahudi wakamwambia, “Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?”
49 Jesus replied, “A demon does not [control] me! I honor my Father, and you do not honor me!
Yesu akajibu, “Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
50 I am not trying to honor myself. There is someone else who desires [to honor me], and he is the one who will judge [whether it is I who am telling the truth or whether it is you who are telling the truth].
Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
51 But the truth is that anyone who obeys what I say will never die!” (aiōn g165)
Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele.” (aiōn g165)
52 Then the Jewish [leaders] [SYN], [thinking that he was talking about ordinary death and not about spiritual death], said to him, “Now we are sure that a demon [controls] you! Abraham and the prophets died [long ago]! But you say that anyone who obeys what you teach will never die! (aiōn g165)
Basi, Wayahudi wakasema, “Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele! (aiōn g165)
53 (You are certainly not greater than our ancestor Abraham!/Do you think you are greater than our ancestor Abraham?) [RHQ] He died, and all the prophets died, so who do you think you are [by saying something like that]?”
Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Jesus replied, “If I were honoring myself, that would be worthless. My Father is the one who you say is your God. He is the one who honors me.
Yesu akawajibu, “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
55 Although you do not know him, I know him [and have a close relationship with him]. If I said that I did not know him, I would be a liar like you are. But I know him, and I obey what he says.
Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
56 Your ancestor Abraham was happy when he thought about what I would [do during] my life [MTY]. [It was as though] he saw that, and was happy.”
Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi.”
57 Then the Jewish [leaders] [SYN] said to him, “You are not 50 years old yet! So (you certainly did not see him!/how could you have seen him?) [RHQ] [Because he died long ago]!”
Basi, Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?”
58 Jesus said to them, “The truth is that I existed before Abraham was born!”
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko.”
59 So, [because they were very angry about Jesus thus saying that he] ([had eternally existed/was equal with God]), they picked up stones to throw at him [to kill him]. But [Jesus] caused them not to be able to see him, and he left the Temple courtyard.
Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.

< John 8 >