< Joel 2 >
1 Blow trumpets on Zion [Hill], God’s sacred hill [in Jerusalem]! Tell the people of Judah that they should tremble, because it will soon be the time for Yahweh [to punish us further].
Piga tarumbeta katika Sayuni, na piga kelele juu ya mlima wangu mtakatifu! Wakazi wote wa nchi watetemeke kwa hofu; maana siku ya Bwana inakuja; Hakika iko karibu.
2 [That will be a very] dark and gloomy day; there will be [black] clouds and it will be very dark. A huge [swarm of locusts] has covered the mountains like [SIM] a black [cloud]. Nothing like this has ever happened before, and nothing like this will ever [happen] again.
Ni siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza nene. Kama asubuhi inayoenea kwenye milima, jeshi kubwa na la nguvu linakaribia. Hakujawahi kuwako jeshi kama hilo, na hakutakuwa tena, hata baada ya vizazi vingi.
3 [It is as though the locusts bring] flames of fire from which no one can escape. In front of them, the land was [beautiful] like [SIM] the garden of Eden, but behind them [the land is like] a desert and nothing survives.
Moto unatumia kila kitu mbele yake, na nyuma yake moto unawaka. Nchi hiyo ni kama bustani ya Edeni mbele yake, lakini nyuma yake kuna jangwa lililoharibika. Hakika hakuna chochote kitakayotoroka.
4 [The locusts] resemble horses, and they run like [SIM] war horses.
Muonekano wa jeshi ni kama farasi, na wanakimbia kama wapanda farasi.
5 Leaping over the mountaintops, they make a noise like rumbling chariots, like [SIM] a mighty army that is preparing for a battle, or like [SIM] the roar of a fire that burns up stubble [in a field].
Wanaruka kwa kelele kama ile ya magari juu ya vilele vya milima, kama kelele za muale wa moto ambao huangamiza majani, kama jeshi la nguvu lililo tayari kwa vita.
6 When people see them coming, they become very pale and frightened.
Mbele yao watu wako katika maumivu na nyuso zao zote zinakuwa za rangi.
7 [The locusts] climb over walls like soldiers do; they march along in columns and never turn aside [from their columns].
Wanakimbia kama wapiganaji wenye nguvu; wanapanda kuta kama askari; wanasonga, kila mmoja kwa hatua, na hawavunji safu zao.
8 They rush straight ahead without pushing each other. [Even though people throw] spears and javelins at them, that will not cause them to stop.
Wala hakuna mmoja anayemsukuma mwingine kando; wanasonga, kila mmoja katika njia yake; wao huvunja kwa njia ya ulinzi na si kuanguka nje ya mstari.
9 They swarm over the city walls and enter our houses; they enter through our windows like [SIM] thieves do.
Wanakimbilia jiji, wanakimbia kwenye ukuta, wanapanda ndani ya nyumba, na hupita kupitia madirisha kama wezi.
10 [It is as though] they cause the earth to shake and the sky to tremble. The sun and the moon become dark and the stars do not shine [because there are so many locusts in the sky].
Nchi hutikisika mbele yao, mbingu hutetemeka, jua na mwezi ni giza, na nyota zinaacha kuangaza.
11 Yahweh leads this army [of countless locusts], and they obey his commands. This time when he is judging and punishing us is very terrible, [with the result that it seems that] no one [RHQ] can survive it.
Bwana huinua sauti yake mbele ya jeshi lake; maana wapiganaji wake ni wengi sana; kwa maana wao ni wenye nguvu, wale wanaofanya amri zake. Kwa maana siku ya Bwana ni kubwa na ya kutisha sana. Nani anayeweza kuishi?
12 But Yahweh says, “In spite of [these disasters that you have experienced], you can return to me with all your inner beings. Weep, and mourn, and (fast/abstain from eating food) [to show that you are sorry for having abandoned me].
“Lakini hata sasa,” asema Bwana, “Nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote. Haraka, lia na omboleza.”
13 Do not tear your clothes [to show that you are sorry]; instead, show [MET] that you are sorry.” Yahweh is merciful and kind; he does not quickly become angry; he faithfully loves [people]. He does not quickly become angry; instead, he greatly and faithfully loves [you], and he does not like to punish you.
Rarueni miyoyo yenu, si mavazi yenu tu, na kurudi kwa Bwana Mungu wenu. Kwa maana ni mwenye neema na mwenye huruma, si mwepesi wa hasira na wingi katika uaminifu wa agano, na angependa kugeuka kutokana na adhabu.
14 No one knows [RHQ] if he will change his mind [about punishing you] and if instead he will act mercifully [toward you]. If he does that, he will bless you [by giving you plenty of grain and wine] in order that you can offer [some of] those things as sacrifices to him.
Nani anajua? Labda angegeuka na kuwa na huruma, na kuacha baraka nyuma yake, sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji kwa Bwana, Mungu wenu?
15 Blow the trumpets on Zion [Hill]! Gather the people together! Show by fasting that you are sorry [for the sins that you have committed].
Piga tarumbeta huko Sayuni, itisha kwa ajili ya funga takatifu, na itisheni kusanyiko takatifu.
16 Perform the rituals to cause yourselves to be acceptable to Yahweh. Gather everyone together— the old people and the children, even the babies, and summon brides and bridegrooms from their rooms.
Kusanyeni watu, wito kwa kusanyiko takatifu. Kusanya wazee, kukusanya watoto na watoto wachanga. Bwana arusi waweze kutoka nje ya vyumba vyao, na bibi arusi kutoka kwenye vyumba vyao.
17 Tell the priests who serve Yahweh to cry between the altar and the entrance to the temple and to pray [this]: “Yahweh, rescue/save [us] your people; do not allow people from other nations to despise us; do not allow them to ridicule us and say, ‘Why has [RHQ] their God [abandoned them]?’”
Basi makuhani, watumishi wa Bwana, waliao kati ya patakatifu na madhabahu. Wawaambie, Waitie watu wako, Ee Bwana, wala usitoe urithi wako kwa aibu, ili mataifa watawawale juu yao. Kwa nini wanapaswa kusema kati ya mataifa, “Yuko wapi Mungu wao?”
18 But Yahweh [showed that he] was concerned about his people and that he would act mercifully toward them.
Ndipo Bwana alikuwa mwenye bidii kwa nchi yake na kuwahurumia watu wake.
19 When the people prayed, Yahweh answered and said, “I will give you [plenty of] grain and wine and [olive] oil, and you will be satisfied. And I will no longer allow other nations to insult you.
Bwana akawajibu watu wake, Tazama, nitawaletea nafaka, divai mpya, na mafuta. Utaridhishwa nao, wala sitawafanya kuwa aibu kati ya mataifa.
20 Another army [of locusts will come] from the north [to attack you], but I will force them to continue [past Jerusalem] into the desert. Some will go into the Dead Sea in the east and some will go into the [Mediterranean] Sea in the west. [There] they will [all die, and their bodies] will stink.” Yahweh does great things!
Nitawaondoa washambuliaji wa kaskazini mbali nanyi, na nitawapitisha katika nchi kavu na iliyoachwa. Sehemu ya mbele ya jeshi lao itaingia bahari ya mashariki, na sehemuya nyuma itaingia bahari ya magharibi. Uvundo wake utainuka juu, na harufu yake mbaya itainuka juu. Hakika, amefanya mambo makuu.
21 He does wonderful things! So even the ground should rejoice!
Msiogope, nchi, shangilieni na kufurahi, kwa kuwa Bwana atafanya mambo makuu.
22 And the wild animals should not be afraid, because the meadows will soon become green again; the fig trees and [other] trees will be full of fruit, and the grapevines will be covered with grapes.
Usiogope, wanyama wa kondeni, kwa kuwa malisho ya jangwa yatakua, miti itazaa matunda yake, na miti ya mizabibu na mizabibu itazaa mavuno yao yote.
23 You people of Jerusalem, rejoice about what Yahweh, your God, [will be doing for you]. He will send abundant rain at the (right time/time when it is needed)— (in the spring/early in the year) and (in the autumn/late in the year) like he did previously.
Furahini, enyi watu wa Sayuni, na kufurahi katika Bwana, Mungu wenu. Kwa maana atakupa mvua ya vuli kwa kiasi na kuleta mvua kwa ajili yenu, mvua ya vuli na mvua ya masika kama hapo awali.
24 The ground where you thresh the grain will be covered with grain, and your vats where you store grape juice and [olive] oil will be full.
Sakafu ya kupepetea zitajaa ngano, na vyombo vitafurika kwa divai mpya na mafuta.
25 [Yahweh said, ] “I will repay you for everything that was destroyed by those great swarms of locusts that I sent to attack you.
“Nitawawezesha miaka ya mazao ambayo nzige walikula, Palale, nzige, na nzige wakuteketeza - jeshi langu lenye nguvu ambalo nimelituma kati yenu.
26 You, my people, will eat until your stomachs are full. Then you will praise me [MTY], Yahweh, your God, for the wonderful things that I have done for you. And never again will you be disgraced.
Mutakula chakula tele na kushiba, na kulitukuza jina la Bwana, Mungu wenu, aliyefanya miujiza kati yenu, wala sitawaletea tena watu wangu.
27 When that happens, you will know that I am [always] among you, and that I am Yahweh, your God, and that there is no other [God]. Never again will you be disgraced.”
Utajua ya kwamba mimi niko kati ya Israeli, na kwamba mimi ni Bwana, Mungu wako, wala hakuna mwingine, wala sitawaletea aibu watu wangu.
28 “Some time later, I will give my Spirit to many [HYP] people. Your sons and daughters will proclaim messages that come directly from me. Your old men will have dreams [that come from me], and your young men will have visions [that come from me].
Itakuwa baada ya hayo nitamimina Roho yangu juu ya wenye mwili yote, na wana wenu na binti zenu watatabiri. Wazee wenu wataota ndoto, vijana wenu wataona maono.
29 At that time, I will give my Spirit even to servants, both men and women.
Pia juu ya watumishi na watumishi wa kike, siku hizo nitaimimina Roho wangu.
30 I will do unusual/amazing things on the earth and in the sky. [On the earth] [CHI], there will be much blood [shed] and [there will be very large] fires and smoke that resembles huge clouds.
Nitaonyesha maajabu mbinguni na duniani, damu, moto na nguzo za moshi.
31 [In the sky, ] the sun will become dark and the moon will become [as red as] [MET] blood. [Those things will happen] before that great and terrible day when [I], Yahweh, appear.
Jua litakuwa giza na mwezi kuwa damu, kabla ya siku kuu na ya kutisha ya Bwana itakapokuja.
32 But at that time [I] will save everyone who worships me. I promise that some people in Jerusalem [DOU] will escape [those disasters]; those whom I have chosen will survive.”
Itakuwa kwamba kila mtu anayeita jina la Yahweh ataokolewa. Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na Yerusalemu watakuwa na wale waliokoka, kama Bwana alivyosema, na kati ya wale walisalia, wale ambao Bwana anawaita.