< Jeremiah 9 >
1 I wish that my head was [like] [MET] a spring of water, and that my eyes were [like] a fountain of tears. Then I would cry night and day for all of my people who have been killed [by our enemies].
Laiti kichwa changu kingekuwa chemchemi ya maji na macho yangu yangekuwa kisima cha machozi! Ningelia usiku na mchana kwa kuuawa kwa watu wangu.
2 I wish that I could leave my people and forget them, and go and live in a shack/shelter in the desert, because they have not remained faithful [MET] [to Yahweh]; they are a mob of people who deceive others.
Laiti ningekuwa na nyumba ya kukaa wasafiri jangwani, ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa kuwa wote ni wazinzi, kundi la watu wadanganyifu.
3 [Yahweh replied to me], “They use their tongues [to tell] [MET] lies like people shoot [arrows] with bows. It is because they tell lies that they have become more powerful in this land, and they do not know me.
“Huweka tayari ndimi zao kama upinde, ili kurusha uongo; wamekuwa na nguvu katika nchi lakini si katika ukweli. Wanatoka dhambi moja hadi nyingine, hawanitambui mimi,” asema Bwana.
4 Do not trust your neighbors and [even] your brothers! They all are as deceitful [as Jacob was]. They slander [each other] and tell lies [about each other].
“Jihadhari na rafiki zako; usiwaamini ndugu zako. Kwa kuwa kila ndugu ni mdanganyifu, na kila rafiki ni msingiziaji.
5 They deceive their friends and never tell the truth. They lie continually and, because of that, they have become skilled liars; they do one oppressive thing after another, and are unable to stop doing it.
Rafiki humdanganya rafiki, hakuna yeyote asemaye kweli. Wamefundisha ndimi zao kudanganya, wanajichosha wenyewe katika kutenda dhambi.
6 They habitually lie and deceive [each other], and no one will admit/say that I am God.
Unakaa katikati ya udanganyifu; katika udanganyifu wao wanakataa kunitambua mimi,” asema Bwana.
7 Therefore [I], the Commander of the armies of angels, say this: Listen carefully to what I say: I will [cause my people to experience great afflictions, ] [like a metalworker puts metal in a hot fire] [MET] to completely burn out the impure bits. Because of all [the evil things] that my people have done, there is absolutely nothing else [RHQ] that I can do.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Tazama, nitawasafisha na kuwajaribu, kwani ni nini kingine niwezacho kufanya kwa sababu ya dhambi ya watu wangu?
8 What they say [MTY] [injures people like] [MET] poisoned arrows do. They say to their neighbors, ‘I hope things will go well for you,’ while they are planning to kill them.
Ndimi zao ni mshale wenye sumu, hunena kwa udanganyifu. Kwa kinywa chake kila mmoja huzungumza maneno mazuri na jirani yake, lakini moyoni mwake humtegea mtego.
9 Should I not punish them for doing that [RHQ]? Yes, I should certainly (get revenge on/give what they deserve to) [the people of] a nation that does things like that!”
Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya jambo hili?” asema Bwana. “Je, nisijilipizie kisasi kwa taifa kama hili?”
10 So, I will weep and wail for [the people who live in] the mountains and in the (pastures/places where the livestock eat the grass), because those areas will be desolate, and no one will live there. There will be no cattle there to call to each other, and all the birds and wild animals will have fled [to other places].
Nitalia na kuomboleza kwa ajili ya milima na kuomboleza kuhusu malisho ya jangwani. Yamekuwa ukiwa, wala hakuna apitaye humo, milio ya ngʼombe haisikiki. Ndege wa angani wametoroka na wanyama wamekimbia.
11 [Yahweh also says], “I will cause Jerusalem to become a heap of ruins, and [only] jackals/wolves will live there. I will destroy the towns of Judah, with the result that they will be completely deserted; no one will live there.”
“Nitaifanya Yerusalemu lundo la magofu, makao ya mbweha; nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa ili asiwepo atakayeishi humo.”
12 [I said], “Only people who are very wise [RHQ] can understand these things. Only those who have been taught by Yahweh can [RHQ] explain these things to others. The wise people are [RHQ] the only ones who can explain why the land will be completely ruined with the result that everyone [RHQ] will be afraid to travel through it.”
Ni mtu yupi aliye na hekima ya kutosha ayaelewe haya? Ni nani aliyefundishwa na Bwana awezaye kuyaeleza haya? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa ukiwa kama jangwa ambapo hakuna awezaye kupita?
13 Yahweh replied, “[These things will happen] because my people have rejected my laws which I gave to them; they have not obeyed me or my instructions.
Bwana akasema, “Ni kwa sababu wameiacha sheria yangu, niliyoiweka mbele yao: hawajaniheshimu mimi wala kufuata sheria yangu.
14 Instead, they have stubbornly done the things that they wanted to do. They have worshiped the idols that represent the god Baal, which is what their ancestors did.
Badala yake wamefuata ukaidi wa mioyo yao, wamefuata Mabaali, kama vile baba zao walivyowafundisha.”
15 So now listen to what [I], the Commander of the armies of angels, the God of the Israelis, say: [What I will do will be like] [MET] giving these people bitter things to eat and poison to drink:
Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: “Tazama, nitawafanya watu hawa wale chakula kichungu na kunywa maji yenye sumu.
16 I will scatter them to many nations which neither they nor their ancestors have known [anything about]; I will [enable their enemies to] strike them with swords until I have destroyed them.”
Nitawatawanya katika mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuwajua, nikiwafuata kwa upanga mpaka niwe nimewaangamiza kabisa.”
17 This is also what the Commander of the armies of angels says: “Think [about what is happening], [then] summon those women who mourn [when someone has died].
Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Fikiri sasa! Waite wanawake waombolezao waje, waite wale walio na ustadi kuliko wote.
18 Tell them to come quickly and start to wail, with the result that tears will stream down from your(pl) eyes.
Nao waje upesi na kutuombolezea, mpaka macho yetu yafurike machozi na vijito vya maji vitoke kwenye kope zetu.
19 Listen to [the people of] Jerusalem crying/lamenting, saying, ‘We have been ruined/destroyed! We have experienced a terrible disaster! Now we are very ashamed, because our houses have been destroyed [by our enemies], and we [are being forced to] leave our land.’”
Sauti ya kuomboleza imesikika kutoka Sayuni: ‘Tazama jinsi tulivyoangamizwa! Tazama jinsi aibu yetu ilivyo kubwa! Ni lazima tuihame nchi yetu kwa sababu nyumba zetu zimekuwa magofu.’”
20 You women, listen to what Yahweh says [MTY]. Pay attention to his words [DOU]. Teach your daughters to wail. Teach each other how to sing funeral songs,
Basi, enyi wanawake, sikieni neno la Bwana; fungueni masikio yenu msikie maneno ya kinywa chake. Wafundisheni binti zenu kuomboleza; fundishaneni kila mmoja na mwenzake maombolezo.
21 because people will be dying [PRS] in your houses and in palaces. There will be no more children playing in the streets, there will be no more young men [gathering] in the city squares/marketplaces.
Mauti imeingia ndani kupitia madirishani, imeingia kwenye majumba yetu ya fahari; imewakatilia mbali watoto katika barabara na vijana waume kutoka viwanja vya miji.
22 There will be corpses scattered across the fields like dung; their dead bodies will lie there like [SIM] grain that has been cut by reapers/farmers, and there will be no one [still alive] to bury them.
Sema, “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Maiti za wanaume zitalala kama mavi katika mashamba, kama malundo ya nafaka nyuma ya mvunaji, wala hakuna anayekusanya.’”
23 Yahweh says this: “Wise men should not boast about their being wise, strong men should not boast about their being strong; and rich people should not boast about their being rich.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Mwenye hekima asijisifu katika hekima yake, au mwenye nguvu ajisifu katika nguvu zake, wala tajiri ajisifu katika utajiri wake,
24 Instead, those who want to boast should boast about their knowing me and about understanding that I am Yahweh, that I am kind and just and righteous, that I faithfully love [people], and that I am delighted with [people who act] that way.
lakini yeye ajisifuye, na ajisifu kwa sababu hili: kwamba ananifahamu na kunijua mimi, kwamba mimi ndimi Bwana, nitendaye wema, hukumu na haki duniani, kwa kuwa napendezwa na haya,” asema Bwana.
25 There will be a time when I will punish all those people of Egypt and of the Moab people-group and of the Edom [people-group] and of the Ammon [people-group], all those people who live close to desert areas (OR, who cut their hair short [to please their gods]) far from Judah, all those people who have [changed their bodies by] circumcising them [MET] but who have not [changed] their inner beings. I will punish the people of Judah also, because they have not changed their inner beings, [either].”
“Siku zinakuja, nitakapowaadhibu wale wote ambao wametahiriwa kimwili tu, asema Bwana,
yaani Misri, Yuda, Edomu, Amoni, Moabu na wote wanaoishi jangwani sehemu za mbali. Kwa maana mataifa haya yote hayakutahiriwa mioyo yao, nayo nyumba yote ya Israeli haikutahiriwa.”