< Jeremiah 7 >

1 Yahweh gave me another message. He said to me,
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 “Go to the entrance of my temple, and give this message to the people: You people of Judah who worship here, listen to this message from Yahweh!
“Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
3 The Commander of the armies of angels says to you, ['If you] stop doing evil things and start doing what is right, I will allow you to remain living in your land.'
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
4 [But some people] are repeatedly saying to you, ‘The temple of Yahweh is here, [so we will be safe]; [he will not allow us and the temple to be destroyed].’ But do not pay attention to what they say, because they are deceiving you.
Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
5 [I will act mercifully to you only] if you change your behavior and stop doing evil things, and if you [start to] act fairly/justly toward others,
Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
6 and if you stop oppressing foreigners [who live in your country], and orphans and widows, and if you stop murdering people, and if you stop worshiping (foreign gods/idols). However, if you continue to do those things, you will be destroyed.
kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
7 If you do what I have told you, I will allow you to stay in this land that I promised to your ancestors that it would belong to them [and their descendants] forever.
ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
8 [People are repeatedly] telling you, [‘The temple is here, so we are safe]’, and you are trusting/believing [that what they are saying is true], but it is a lie. [Those people are deceiving you, and what they say is] worthless.
Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
9 You think that [RHQ] you can steal things, murder people, commit adultery, tell lies in court, and worship Baal and all those other gods that you did not know about previously,
“‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
10 and then come here and stand in front of this temple, which is my temple, and say ‘Nothing bad will happen to us!’, while you continue to do all those abominable things.
kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
11 Do you realize that you are causing this temple, which is my temple, to become like [MET] a den where bandits hide [RHQ]? Do you not know that I see [all the evil things that you people do there]?
Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
12 [Long ago] I put my Sacred Tent at Shiloh [city], to be a place where people would worship me [MTY]. Think about how I [destroyed it] because my people, the Israeli people, did [many] wicked things there.
“‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
13 And while you were continually doing those wicked things, I told you about it many times, but you refused to listen. I called out to you, but you refused to answer [me].
Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
14 Therefore, just like I destroyed Shiloh, I will [now] destroy this temple that was built for people to worship me [MTY], this temple that you trust in, that is in this place that I gave to you and your ancestors.
Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
15 And I will expel you from this land and send you [to other countries] far away from me, just like I did to your relatives, the people of Israel.”
Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
16 [Yahweh said to me, “Jeremiah], do not pray for these people [any longer]. Do not cry for them or plead for [me to help] them, because I will not pay any attention to you.
“Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
17 Do you see [the wicked things] that they are doing in the streets of Jerusalem and in the [other] towns in Judah?
Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
18 The children gather firewood and their fathers use it to make fires [on the altars to burn sacrifices]. The women knead/make dough to make cakes to offer to [their goddess Astarte who is called] the Queen of Heaven. And [on their altars] they pour out offerings of wine to [their] other idols. All of those things cause me to become extremely angry!
Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
19 But I am not [RHQ] the one whom they are hurting; they are really [RHQ] hurting themselves [by doing these things for which they should be] very ashamed!”
Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
20 So Yahweh the Lord says this: “Because I am extremely angry with [what happens at] this place, I will punish these people severely [MTY]; my being very angry will be [like] [MET] a fire that will not be extinguished, and I will destroy the people, [their] animals, [their] fruit trees, and [their] crops.”
“‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
21 Therefore, this is what the Commander of the armies of angels says: “Take away [IRO] your offerings that you bring to burn completely on your altars and your [other] sacrifices; [don’t give them to me]; eat them [yourselves]!
“‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
22 When I led your ancestors out of Egypt, it was not offerings to be completely burned on the altar or [other] sacrifices that I wanted from them.
Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
23 What I told them was, ‘Obey me; [if you do that], I will be your God and you will be my people. If you do the things that I want you to do, everything will go well for you.’
lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
24 But your ancestors would not pay any attention [DOU] to me. They continued to do [the evil things] that they wanted to do, everything that in their stubborn inner beings they desired to do. Instead of coming closer to me, they went further away from me.
Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
25 From the day that your ancestors left Egypt until now, I have continued to send my prophets to you.
Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
26 But you, [my people], have not listened to me or paid attention to what I said; you have been stubborn, and you have done more sinful things than your ancestors did.”
Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
27 [Then Yahweh said to me], “When you tell all this to my people, they will not listen to you. When you call to them, they will not answer.
“Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
28 Say to them, ‘You people [of Judah] have not obeyed Yahweh, your God; you have not accepted it when he tried to correct you. No one among you is truthful; you do not say anything that is true; [you speak only lies].’
Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
29 [So, tell them to] cut off their hair [to show that they are mourning]; tell them to go up into the hills and sing a sad funeral song, because I have completely rejected [DOU] this generation [of people] who have made me angry.”
Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
30 Yahweh says this: “The people of Judah have done many things that I say are evil. They have set up their disgusting idols in my temple, causing it to become an unacceptable [place to worship me].
“‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
31 They have built altars at Topheth in Ben-Hinnom Valley [outside Jerusalem], and they sacrifice their sons and daughters on those altars. I never commanded them to do that; I never even thought that anyone would do that.
Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
32 So they should beware! There will be a time when that place will no longer be called Topheth or the Hinnom Valley; instead, it will be called the Valley of Slaughter. There will be a huge number of people who will be buried there, with the result that there will be no space to bury more bodies.
Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
33 The corpses of my people that are [not buried and are] left on the ground will be eaten by vultures and wild animals, and there will be no one to shoo/chase them away.
Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
34 There will be no one singing and laughing any more in the streets of Jerusalem; there will be no more joyful voices of bridegrooms and brides in Judah, because the land will be completely destroyed.”
Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.

< Jeremiah 7 >