< Jeremiah 49 >
1 [This message is] about the Ammon people-group. This is what Yahweh says: “There are [RHQ] plenty of Israeli people left to occupy [the land of the tribe of] Gad. So, why are [RHQ] [the people who worship the god] Molech living in those towns?
Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo Bwana: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?
2 There will be a time when I will sound the battle-cry [for their enemies] to attack [their capital city], Rabbah. [Then] it will become a heap of ruins, and [all] the nearby towns will be burned. Then [the people of] Israel will again possess the land that the Ammon people-group took away from them.
Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapopiga kelele ya vita dhidi ya Raba mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema Bwana.
3 You people of Heshbon [city] [MTY], wail, because Ai [town nearby] will be destroyed. You people of Rabbah [city], weep; put on (rough clothing/sackcloth) [to show you are mourning]; run back and forth [in confusion] inside the city walls, because [your god] Milcom, along with its priests and officials, will be taken away (in exile/to other countries).
“Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni nguo za gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.
4 You are [RHQ] very proud of your very fertile valleys, [but they will soon be ruined]. You rebellious people, you trusted in your wealth, and you said, ‘Certainly no [RHQ] army will be able to attack us!’
Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’
5 But listen to this: 'I, the Commander of the armies of angels, will cause you to become terrified. You will all be forced to flee [to other countries], and no one will be able to bring you together [again].'
Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.
6 But some day I will enable the Ammon people-group to return to their land. [That will surely happen, because I, ] Yahweh, have said it.”
“Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema Bwana.
7 [This message is] about the Edom people-group. This is what the Commander of the armies of angels says: “It seems that [RHQ] there are no wise people in Teman [district in Edom]! There are no people left who can give others [good] advice. The people who were wise [PRS] have disappeared.
Kuhusu Edomu: Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Je, hakuna tena hekima katika Temani? Je, shauri limewapotea wenye busara? Je, hekima yao imechakaa?
8 You people of Dedan [city in the south of Edom], turn and flee and hide in deep [caves], because when I cause the Edom people-group to experience disaster, I will punish you, too.
Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa, wewe uishiye Dedani, kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau wakati nitakapomwadhibu.
9 Those who harvest grapes always [RHQ] leave some on the vines. When thieves come at night, they surely [RHQ] steal only as much as they want.
Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako, wasingebakiza zabibu chache? Kama wezi wangekujia usiku, je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?
10 But I will cause everything in Edom to be destroyed, and there will be nothing left, and there will be no place for people to hide. [Many of] [HYP] the children, their relatives and their neighbors, will die, and Edom will not exist any more.
Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi, nitayafunua maficho yake, ili asiweze kujificha. Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia, naye hatakuwepo tena.
11 But I will protect the orphans, and the widows [also] will [be able to] depend on me [to help them].”
Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao. Wajane wako pia wanaweza kunitumaini mimi.”
12 And this is [also] what Yahweh says: “If those who do not deserve to suffer [MET] must suffer, you people of Edom must [RHQ] suffer much more [DOU]! You will not escape being punished.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe.
13 I, Yahweh, have solemnly promised, using my own name, that [your chief city] Bozrah will become a place that people will be horrified about. It will be a heap of ruins. People will make fun of it and use its name when they curse people. All the nearby towns and villages will be a ruins forever.”
Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”
14 I heard this message from Yahweh: “I have sent an ambassador to [many] nations, [to tell them to] gather together to attack Edom. They must prepare for battle!”
Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Jikusanyeni ili kuushambulia! Inukeni kwa ajili ya vita!”
15 [And Yahweh says to the people of Edom, ] “I will cause your nation to become very unimportant among the [other] nations. They will all despise your country.
“Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa, aliyedharauliwa miongoni mwa watu.
16 You have caused [people of other nations] to be terrified, and you [MTY] have been very proud, but you have deceived yourselves. You live in caves in the rock cliffs; [you think that you are safe there because] you live high up there. But even if you make your homes as high up as the eagles’ nests, I will cause you to come [crashing] down.
Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayedumu katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
17 Edom will become a place about which people are horrified; people who pass by will be horrified and will (gasp/be shocked) when they see the destruction.
“Edomu atakuwa kitu cha kuogofya; wote wapitao karibu watashangaa na kuzomea kwa sababu ya majeraha yake yote.
18 Edom will be destroyed as [completely as] Sodom and Gomorrah and the nearby towns were destroyed [long ago]. [As a result, ] no one will live there [any more] [DOU].
Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa, pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
19 I will come to Edom [suddenly] like [SIM] a lion comes out of the jungle and [leaps on the sheep that are] eating in the good pastureland. I will quickly chase the people of Edom from their land. And [then] I will appoint for them a leader whom I will choose; [I can do that] because there is no one [RHQ] like me who can object to what I do. No ruler can oppose me.
“Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
20 Listen to what I have planned to do to the people of Teman [town] and [the rest of] Edom: Even the little children will be dragged away, and I will completely get rid of the people [MET] who live there.
Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu, kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali; yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
21 When Edom is destroyed, the noise [will be extremely great], with the result that the earth will shake, and the wailing of the people will be heard [as far away as] the Red Sea.
Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka. Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.
22 Look! The enemy troops will swoop/rush down over Bozrah like an eagle spreads its wings when it swoops down [to seize an animal]. On that day, [even the strongest] warriors of Edom will [be afraid] like [SIM] a woman who is about to give birth.”
Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula, akitandaza mabawa yake juu ya Bosra. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
23 [This message is] about Damascus. [This is what Yahweh says]: “[The people in the nearby cities of] Hamath and Arpad are confused, because they have heard bad news [about Damascus]. They are very anxious and restless, like [SIM] a sea in a big storm.
Kuhusu Dameski: “Hamathi na Arpadi imetahayarika, kwa kuwa wamesikia habari mbaya. Wamevunjika moyo na wametaabika kama bahari iliyochafuka.
24 The people of Damascus have become very weak, and [they all] have (panicked/fled [because] they are very afraid). The people are anguished and in pain like [SIM] a woman [experiences] who is about to give birth.
Dameski amedhoofika, amegeuka na kukimbia, hofu ya ghafula imemkamata sana; amepatwa na uchungu na maumivu, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
25 That famous city, that I was [previously] pleased with, will be abandoned.
Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa, mji ambao ninaupenda?
26 Its young men will fall in the streets. Its soldiers will all be killed in one day.
Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
27 And I, the Commander of the armies of angels, will start a fire to burn the walls that surround Damascus, and the palaces of [King] Ben-Hadad will be burned down.”
“Nitatia moto kuta za Dameski; utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”
28 [This is a message] about the Kedar [people-group] and the kingdom of Hazor which [the army of] Nebuchadnezzar King of Babylon attacked. This is what Yahweh says: “[I will cause an army to] advance to attack Kedar and destroy those people who live east [of Judah].
Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia: Hili ndilo asemalo Bwana: “Inuka, ushambulie Kedari na kuwaangamiza watu wa mashariki.
29 Their tents and their flocks [of sheep] will be captured. The curtains [in their tents] and their camels and their other possessions will be taken away. [Everywhere] men will shout, ‘We are terrified [because terrible things are happening] all around us!’
Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa; vibanda vyao vitatwaliwa pamoja na mali zao zote na ngamia zao. Watu watawapigia kelele, ‘Hofu kuu iko kila upande!’
30 So [I, ] Yahweh, say, ‘Run away [quickly]! You people who live in Hazor, go and hide in deep [caves], because King Nebuchadnezzar of Babylon wants to attack you [with his army]; he is planning to destroy you!’
“Kimbieni haraka! Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,” asema Bwana. “Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu; amebuni hila dhidi yenu.
31 But I say [to Nebuchadnezzar], ‘Go up and attack that nation whose people feel secure; they do not have allies [who will help them] and do not have [walls with] gates that have bars in them.
“Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe, linaloishi kwa kujiamini,” asema Bwana, “taifa lisilo na malango wala makomeo; watu wake huishi peke yao.
32 Your troops will seize their camels and [other] livestock. I will scatter in every direction [IDM] those people who live in remote places (OR, who cut their hair short). I will cause them to experience disasters from every direction.
Ngamia wao watakuwa nyara, nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa. Wale walio maeneo ya mbali nitawatawanya pande zote, nami nitaleta maafa juu yao kutoka kila upande,” asema Bwana.
33 Hazor will become a place where jackals/wolves live, and it will be deserted forever. No one will live there again; no one will settle there [DOU].’”
“Hazori itakuwa makao ya mbweha, mahali pa ukiwa milele. Hakuna yeyote atakayeishi humo; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
34 I received this message from Yahweh when King Zedekiah was starting to rule Judah.
Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:
35 This is what the Commander of the armies of angels says: “The men of Elam are famous (archers/men who shoot arrows well); that is how they have made their country very powerful. But I will get rid of them [MET].
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama, nitavunja upinde wa Elamu, ulio tegemeo la nguvu zao.
36 I will bring their enemies from all directions [IDM, DOU], and they will scatter the people of Elam in all directions. The people of Elam will be exiled to every nation on the earth [LIT, HYP].
Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu toka pande nne za mbingu, nitawatawanya katika hizo pande nne, wala hapatakuwa na taifa ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa hawatakwenda.
37 Because I am very angry with the people of Elam, I will enable their enemies to smash Elam; I will cause the people of Elam to experience great disasters. I will enable their enemies, who want to kill them, to pursue them [and kill them] with swords until I completely get rid of all of them.
Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao, mbele yao wale wanaotafuta uhai wao; nitaleta maafa juu yao, naam, hasira yangu kali,” asema Bwana. “Nitawafuatia kwa upanga mpaka nitakapowamaliza.
38 I, Yahweh, will judge them there [MTY], and [then] I will get rid of their king and [his] officials.
Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,” asema Bwana.
39 But some day, I will enable the people of Elam to return to their land. [That will surely happen because I, ] Yahweh, have said it.”
“Lakini nitarudisha mateka wa Elamu katika siku zijazo,” asema Bwana.