< Jeremiah 38 >

1 [Four officials, ] Shephatiah the son of Mattan, Gedaliah the son of Pashhur, Jehucal the son of Shelemiah, and Pashhur the son of Malkijah, heard what I had been telling all the people.
Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema,
2 [I had been telling them] that Yahweh was saying, “Everyone who stays in Jerusalem will die. They will be killed by [their enemies’] swords or from famines or from diseases. But those who surrender to the Babylonian army, they will be spared. They will not be killed.
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’
3 Yahweh also says that the army of the King of Babylon will certainly capture this city [DOU].”
Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’”
4 So those officials [went] to the king and said, “This man [Jeremiah] should be executed! Because of what he is saying, he is discouraging our soldiers who remain in the city. He is also discouraging the people. He is not saying things that will help us; he is saying things that will defeat us.”
Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”
5 King Zedekiah said, “All right, do to him what you want to; I do not have the power to stop you.”
Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”
6 So those officials took me from my cell and lowered me by ropes into a well in the courtyard. The well belonged to Malkijah, who was a son of the king. There was no water in the well, but there was [a lot of] mud, so I sank [down deep] into the mud.
Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.
7 But Ebed-Melech, a palace official from Ethiopia, heard [someone say] that I was in the well. [At that time] the king was deciding/judging people’s cases at the Benjamin Gate.
Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini,
8 Ebed-Melech went out of the palace and said to the king,
Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia,
9 “Your majesty, those men have done a very evil thing. They have put the prophet Jeremiah in a well. [Almost] all the food in the city is gone, [so they will not be able to bring him any food] and as a result he will die from hunger!”
“Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”
10 So the king told Ebed-Melech, “Take thirty of my men/soldiers with you, and pull Jeremiah out of the well, in order that he does not die!”
Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”
11 So Ebed-Melech took thirty men with him and they went into a room in the palace below the room where they stored very valuable things. There they found some old rags and discarded clothing. They took those things and went to the well. They fastened them to a rope and lowered the rope to me.
Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima.
12 Then Ebed-Melech called down to me, “Put these rags underneath your armpits, to protect you from [being injured by] the ropes!” So I did that.
Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo,
13 Then they pulled me out of the well. I [returned] to the courtyard where the palace guards stayed, and I stayed there.
nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.
14 [One day] King Zedekiah summoned me, and I was brought to the king, [who was waiting for me] at the entrance of the temple. He said to me, “I want to ask you something. I want you [to answer me truthfully, and] and to not conceal anything.”
Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”
15 I replied, “If I tell you [the truth], you will [command that I] be executed. And if I give you [good] advice, you will not pay attention to what I say.”
Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”
16 But King Zedekiah secretly promised me, “[Tell me the truth]! And as surely as Yahweh lives, I will not [cause] you to be executed, and I will not hand you over to those who are wanting to kill you.”
Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”
17 [So] then I said to Zedekiah, “This is what the Commander of the armies of angels, the God whom [we] Israelis [worship], says: ‘If you surrender to the officers of the king of Babylon, you and your family will (be spared/not be killed), and this city will not be burned.
Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi.
18 But if you refuse to surrender to them, you will not escape. And the army from Babylonia will capture this city and completely burn it.’”
Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’”
19 The king replied, “But I am afraid [to surrender to the soldiers from Babylon], because their officers may hand me over to the people of Judah who have already joined the soldiers from Babylonia, and those people from Judah will mistreat me.”
Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”
20 I replied, “If you obey Yahweh by doing what I tell you to do, they will not hand you over to our people. Things will go well for you, and you will remain alive.
Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama.
21 But if you refuse to surrender, this is what Yahweh has revealed to me:
Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia:
22 All the women who remain in your palace will be brought out and given to the officers of the king of Babylon. Then those women will say to you: ‘You had friends whom [you thought] you could trust, but they have deceived you and caused you to make a wrong decision. Now [it is as though] you are stuck in mud, and your friends have abandoned you.’
Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia: “‘Walikupotosha na kukushinda, wale rafiki zako uliowaamini. Miguu yako imezama matopeni; rafiki zako wamekuacha.’
23 All of your wives and children [in the city] will be led out to the soldiers from Babylonia, and you also will not escape. [The soldiers of] the King of Babylon will seize you, and they will burn down this city.”
“Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”
24 Then Zedekiah said to me, “Do not tell anyone what you told me; if you tell anyone, my officials may kill you.
Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa.
25 If my officials find out that I talked to you, perhaps they will come to you and say, ‘Tell us what you and the king were talking about. If you do not tell us, we will kill you.’
Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’
26 If that happens, [just] tell them that you pleaded with me not to send you back to the [dungeon/cell in] Jonathan’s house, [because you were afraid that] you would die [if you were put there again].”
basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’”
27 And [that is what happened]. The king’s officials came to me and asked [why the king had summoned me. But] I told them what the king told me to tell them. So they did not ask me any more [questions], because no one had heard what the king and I had said to each other.
Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.
28 So I remained being guarded in the courtyard [of the palace], until the day that [the army of Babylonia] captured Jerusalem.
Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.

< Jeremiah 38 >