< Jeremiah 14 >
1 After there had been no rain [in Judah] for a long time, Yahweh gave me this message:
Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:
2 [The people in] Judah are very distressed; people [are sitting] on the ground and mourning; [in all of] Jerusalem people are crying loudly.
“Yuda anaomboleza, miji yake inayodhoofika; wanaomboleza kwa ajili ya nchi, nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.
3 The rich people send their servants to [wells] to get water, but [all] the wells are dry. The servants return with empty pitchers; they cover their heads [because they are ashamed and humiliated/disappointed and sad].
Wakuu wanawatuma watumishi wao maji; wanakwenda visimani lakini humo hakuna maji. Wanarudi na vyombo bila maji; wakiwa na hofu na kukata tamaa, wanafunika vichwa vyao.
4 The ground is extremely dry and cracked open because there has been no rain. The farmers are very worried, [so] they [also] cover their heads.
Ardhi imepasuka nyufa kwa sababu hakuna mvua katika nchi; wakulima wana hofu na wanafunika vichwa vyao.
5 Even the (does/female deer) abandon their newborn babies/fawns because there is no grass in the fields [for them to eat].
Hata kulungu mashambani anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo kwa sababu hakuna majani.
6 The wild donkeys stand on the barren hills, panting like [SIM] [thirsty] jackals/wolves. They become blind because there is no grass [to eat].
Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame na kutweta kama mbweha; macho yao yanakosa nguvu za kuona kwa ajili ya kukosa malisho.”
7 [The people say], “Yahweh, we have turned away from you and sinned many times, and now we know that we are being punished because of our sins, but please help us in order that everyone can see that you are very great [MTY].
Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu, Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako. Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa, nasi tumetenda dhambi dhidi yako.
8 You are the one whom [we] Israelis confidently expect [to do good things for us] when we have [many] troubles/difficulties. So, why do you [not help us]? You act as though you are a stranger in our land, like you are someone who is staying here for only one night.
Ee Tumaini la Israeli, Mwokozi wake wakati wa taabu, kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi, kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?
9 Are you also surprised [about the terrible things that are happening to us]? Why do you act like you are unable to save anyone, even though you are a strong warrior? Yahweh, you are [here] among us, and [others know that] we are your people, [so] do not abandon us!”
Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa, kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa? Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache!
10 And this is what Yahweh says to those people: “You love to wander away [from me]; you run [MTY] from one [idol] to another. Therefore, now I will no [longer] accept you, and I will punish you for your sins.”
Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa: “Wanapenda sana kutangatanga, hawaizuii miguu yao. Hivyo Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”
11 [Then] Yahweh said to me, “Do not pray for these people [any more].
Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa.
12 When they (fast/abstain from food in order to honor me), I will not pay any attention. When they bring [to me] their offerings [of animals] to be completely burned [on the altar] and their offerings of grain, I will not accept them. Instead, I will get rid of them by wars, by famines, and by diseases.”
Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”
13 Then I replied to him, “Yahweh [my] God, [their] prophets are telling the people that they will not experience wars [MTY] or famines. They are telling the people that you will surely allow us to have peace in our land [for many years].”
Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’”
14 Yahweh replied to me, “Those prophets say that they are speaking what I tell them to say [MTY], but they are telling lies. I did not send them, [so] what they are saying is false. They say that they have received visions from me, and that they are telling things that I have revealed to them, but that is not true. They are saying foolish things that they have only thought of themselves.
Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe.
15 So this is what I say about those prophets who are predicting what will happen, saying that I told them those things: They are saying that we Israelis will not die from wars or famines, but I did not send those prophets. And they themselves will die from wars or from famines.
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa.
16 And the people to whom they are predicting these things, they and their wives and their sons and their daughters, will [also die] from wars or from famines. [Their corpses will] be thrown into the streets of Jerusalem, and there will not be anyone to bury them. I will punish them like they deserve to be punished.
Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.
17 [So, Jeremiah], tell this to them [about yourself]: ‘Day and night my eyes are full of tears. I cannot stop crying. I cry for my people, who are [very precious to me, as if they were] [MET] my daughters. I cry for them because they have been severely wounded; they have been severely crushed [DOU].
“Nena nao neno hili: “‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi usiku na mchana bila kukoma; kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu, amepata jeraha baya, pigo la kuangamiza.
18 If I go out into the fields, I see [corpses of] people who have been slaughtered by our enemies. If I walk along the streets of the city, I see [corpses of people who died] from hunger. The prophets and the priests travel through the land, preaching to people, but they do not know [what they are doing] (OR, [in a land] that they know nothing about).’”
Kama nikienda mashambani, ninaona wale waliouawa kwa upanga; kama nikienda mjini, ninaona maangamizi ya njaa. Nabii na kuhani kwa pamoja wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’”
19 [Then I prayed this]: “[Yahweh], have you completely rejected [the people of] Judah? Do you really despise [the people of] Jerusalem [MTY]? Why have you [RHQ] wounded us very badly, with the result that we will never be healed? We hoped that we would have peace, but there was no peace. We hoped that there would be a time when we would be healed, but all that we received were things that terrified us.
Je, umemkataa Yuda kabisa? Umemchukia Sayuni kabisa? Kwa nini umetuumiza hata hatuwezi kuponyeka? Tulitarajia amani, lakini hakuna jema lililotujia; tulitarajia wakati wa kupona lakini kuna hofu kuu tu.
20 Yahweh, we admit/know that we are wicked people, and that our ancestors [also] did many wicked things. We have [all] sinned against you.
Ee Bwana, tunatambua uovu wetu na kosa la baba zetu; kweli tumetenda dhambi dhidi yako.
21 But [Yahweh], in order that we may honor [MTY] you, do not despise/abandon us. Do not dishonor [the city where] [MTY] your glorious throne is. [Please] do not forget [us], and do not (break your agreement with us/stop doing what you agreed to do for us).
Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa; usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka. Kumbuka agano lako nasi na usilivunje.
22 Those idols that [have been brought from] other nations certainly cannot [RHQ] bring rain [to us], and the sky certainly cannot [RHQ] cause rain to fall. Yahweh our God, you are the only one who can do things like that. So we will confidently expect you [to help us].”
Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa iwezayo kuleta mvua? Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua? La hasha, ni wewe peke yako, Ee Bwana, Mungu wetu. Kwa hiyo tumaini letu liko kwako, kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.