< Jeremiah 12 >

1 Yahweh, whenever I tell you that I am unhappy [about what is happening to me], you [always] act justly/fairly. So now allow me to ask about one more thing [that I do not understand]: Why are wicked people [often] very prosperous? Why do things go very well for dishonest/wicked people?
Wewe daima u mwenye haki, Ee Bwana, niletapo mashtaka mbele yako. Hata hivyo nitazungumza nawe kuhusu hukumu yako: Kwa nini njia ya waovu inafanikiwa? Kwa nini wasio waaminifu wote wanaishi kwa raha?
2 You allow them to prosper like [MET] trees that grow tall and bear [a lot of] fruit. They [always] say [MTY] good things about you, but their hearts are [really] far from you.
Umewapanda, nao wameota, wanakua na kuzaa matunda. Daima u midomoni mwao, lakini mbali na mioyo yao.
3 But Yahweh, as for me, you know what is in my inner being. You see what I [do] and you are able to know what I am thinking. So drag away those [wicked] people, like [people drag away] sheep that they are going to butcher. Set them aside like sheep that are about to be slaughtered!
Hata hivyo unanijua mimi, Ee Bwana; unaniona na kuyachunguza mawazo yangu kukuhusu wewe. Wakokote kama kondoo wanaokwenda kuchinjwa! Watenge kwa ajili ya siku ya kuchinjwa!
4 This land is [RHQ] becoming very dry and even the grass is withering. The wild animals and the birds have [all] died because the people are [very] wicked. [All that has happened] because the people have said, “Yahweh does not know what we are doing (OR, what will happen to us)!”
Je, nchi itakaa katika hali ya kuomboleza mpaka lini, na majani katika kila shamba kunyauka? Kwa sababu wale waishio ndani yake ni waovu, wanyama na ndege wameangamia. Zaidi ya hayo, watu wanasema, “Bwana hataona yatakayotupata sisi.”
5 [Then to show me that I needed to be prepared to endure even greater difficulties, Yahweh said to me], [“It is as though] you have become exhausted from racing against men; so how will you be able to race against horses? If you [stumble and] fall when you are running on open/bare/smooth ground, what will happen to you when you are running through the thornbushes near the Jordan [River]?
“Ikiwa umeshindana mbio na watu kwa mguu na wakakushinda, unawezaje kushindana na farasi? Ikiwa unajikwaa kwenye nchi ambayo ni salama, utawezaje kwenye vichaka kando ya Yordani?
6 [Already] your brothers and [other members of] your own family oppose you. They (plot against/plan to do evil things to) you and they say bad things about you. So even if they say nice things about you, do not trust them!
Ndugu zako, watu wa jamaa yako mwenyewe: hata wao wamekusaliti; wameinua kilio kikubwa dhidi yako. Usiwaamini, ingawa wanazungumza mema juu yako.
7 I have abandoned my [Israeli] people, the people whom I chose to belong to me. I have allowed their enemies to conquer the Israeli people, whom I love.
“Nitaiacha nyumba yangu, nitupe urithi wangu; nitamtia yeye nimpendaye mikononi mwa adui zake.
8 My people have become to me like [SIM] a lion in the forest. [It is as though] they roar at me like a lion, so now I hate them.
Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba wa msituni. Huningurumia mimi, kwa hiyo ninamchukia.
9 My chosen people have [RHQ] become like speckled hawks that are surrounded by vultures [waiting to eat their flesh after they are dead]. Tell all the wild animals to come and eat [the flesh of their corpses].
Je, urithi wangu haukuwa kama ndege wa mawindo wa madoadoa ambaye ndege wengine wawindao humzunguka na kumshambulia? Nenda ukawakusanye pamoja wanyama wote wa mwituni; walete ili wale.
10 Many rulers [from other countries have come with their armies and] devastated/destroyed my people [whom I care for like a farmer takes care of his] vineyard. They have caused my beautiful land to become a barren desert where no one lives.
Wachungaji wengi wataliharibu shamba langu la mizabibu na kulikanyaga shamba langu; watalifanya shamba langu zuri kuwa jangwa la ukiwa.
11 They have caused it to become completely empty; [it is as though] I hear the land crying sadly/mournfully. The whole land is desolate, and no one (worries about/pays any attention to) it.
Litafanywa kuwa jangwa, lililokauka na kuachwa ukiwa mbele zangu; nchi yote itafanywa jangwa kwa sababu hakuna hata mmoja anayejali.
12 The soldiers [of our enemies] have marched across all the barren hilltops. But [I], Yahweh, am using those armies [MTY] to punish your land from one end to the other, and no one will escape.
Juu ya miinuko yote ilivyo kama jangwani mharabu atajaa, kwa maana upanga wa Bwana utawala, kuanzia ncha moja ya nchi hadi nyingine; hakuna hata mmoja atakayekuwa salama.
13 [It is as though] my people planted wheat, but now they are harvesting thorns. They have become very tired [because of much hard work], but they have gained nothing [from all that work]. They will be very disappointed because their harvests [will be very small], [and that will happen] because [I], Yahweh, am extremely angry [with them].”
Watapanda ngano lakini watavuna miiba; watajitaabisha lakini hawatafaidi chochote. Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.”
14 This is [also] what Yahweh said to me: “[I will punish] the evil nearby nations that have been trying to take away the land that I gave to my Israeli people, and I will force them to leave their own land. But I will throw the people of Judah out of their land, also.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa habari ya majirani zangu wote wabaya wanaonyangʼanya urithi ambao ninawapa watu wangu Israeli, nitawangʼoa kutoka nchi zao, nami nitaingʼoa nyumba ya Yuda kutoka katikati yao.
15 But later I will act mercifully toward those nations again, and I will bring them back to their own lands again. Each [clan] will come back to its own land.
Lakini baada ya kuwangʼoa, nitawahurumia tena na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake mwenyewe na kwenye nchi yake mwenyewe.
16 And if the people [of the other nations whose armies have invaded Israel] learn the [religious] customs of my people, and if they learn that I [am listening] when they solemnly promise that they will do something good, like they taught my people to believe that [their god] Baal [was listening] when they made solemn promises, I will cause them to become prosperous, and they also will be my people.
Ikiwa watajifunza vyema njia za watu wangu na kuapa kwa Jina langu, wakisema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo,’ hata kama wakati fulani walifundisha watu wangu kuapa kwa Baali, ndipo watakapofanywa imara katikati ya watu wangu.
17 But I will expel any nation whose people refuse to obey me, and I will destroy that nation and its people. [That will surely happen because I], Yahweh, have said it.”
Lakini kama taifa lolote halitasikiliza na kutii, nitalingʼoa kabisa na kuliangamiza,” asema Bwana.

< Jeremiah 12 >