< Isaiah 21 >

1 [I received] this message [from Yahweh about Babylonia], [a land that is] near the [Persian] Gulf [but which will soon be] a desert. [An army] will soon come from the desert to invade that land; it is an army that causes its enemies to be terrified, an army that will come like a whirlwind from the south.
Neno kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
2 Yahweh showed me a terrifying vision. [In the vision I saw an army] that will betray/deceive people and steal their possessions [after they conquer them]. [Yahweh said], “You armies from Elam and Media, surround [Babylon] and prepare to attack it! I will cause the groaning [and suffering] that Babylon caused to cease!”
Nimeonyeshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, izunguke kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
3 Because of that, my body is full of pain; my pain is like the pain that women who are giving birth experience. When I hear about and see [what God is planning to do], I am shocked.
Katika hili mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
4 I cannot think straight/correctly, and I tremble. I was eager for it to be nighttime, but now it is night, and I am horrified.
Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
5 [In the vision I saw that the leaders of Babylonia] were preparing a great feast. They had spread rugs [for people to sit on]; everyone was eating and drinking. [But] they should get up and prepare their shields, [because they are about to be attacked]!
Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
6 Then Yahweh said to me, “Put a watchman [on the wall of Jerusalem], and tell him to shout/proclaim what he sees.
Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
7 Tell him to watch for chariots pulled by pairs of horses, and [men riding] camels and donkeys, [coming from Babylon]. Tell the watchman to watch and listen carefully!”
Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
8 [So I did that], and one day the watchman called out, “Day after day I have stood on this watchtower, and I have continued to watch during the day and during the night.
Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
9 Now, I saw a man riding in a chariot pulled by two horses. [I called out to him], and he answered/shouted, ‘Babylon has been destroyed! All the idols in Babylon lie in pieces on the ground!’”
Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’”
10 My people [in Judah], [the army of Babylon has caused] you to suffer greatly [as though] [MET] you were grain that was threshed and (winnowed/thrown up into the air for the wind to blow away the chaff). [But now] I have told you what the Commander of the armies of angels the God whom we Israelis [worship], told me [about Babylon].
Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
11 [I received] this message [from Yahweh] about Edom: Someone from Edom has been calling/shouting to me saying, “Watchman, how long will it be before the night is ended? [DOU]”
Neno kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
12 [I], the watchman, replied, “It will [soon] be morning, but after that, it will [soon] be night again. If you want to inquire [again about what will happen in our country], come back and inquire again.”
Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Kama ungeliuliza, basi uliza; bado na urudi tena.”
13 [I received] this message about Arabia: Give this message to people traveling in caravans from Dedan [town in northwest Arabia], who camp in the scrub there. Tell them to bring water for those who are thirsty.
Neno kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
14 And you people who live in Tema [city in northwest Arabia], must bring food for the (refugees/people who are fleeing from their enemies).
leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
15 They are fleeing in order not to be killed by [their enemies’] swords and not to be shot in battles by arrows.
Wanaukimbia upanga, kutoka upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwenye joto la vita.
16 Yahweh said to me, “Exactly one year from now, all the greatness of the Kedar [area in Arabia] will end.
Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
17 Only a few of their soldiers who know well how to shoot arrows will remain alive. [That will surely happen] because [I], Yahweh, have said it.”
Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Bwana, Mungu wa Israeli, amesema.

< Isaiah 21 >