< Isaiah 2 >

1 This is the message that [Yahweh showed me in a vision], concerning Jerusalem and [the rest of] Judea:
Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:
2 [I saw that] in the future, the hill on which Yahweh’s temple is built will be the most important place on the earth; it will be [as though it is] the highest mountain, [as though] it has been raised up above all other hills; and people from all over the world will come there.
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote, utainuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatamiminika huko.
3 People from many people-groups will say [to each other], “Come, let’s go up to the hill, to the temple of Yahweh, to worship the God whom Jacob [worshiped]. [There] Yahweh will teach us what he [desires us to know], in order that our behavior will [please] him. His teaching will be given [to us] in Jerusalem, and [we will take] his message from Jerusalem [to other places/nations].
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
4 Yahweh will listen to the disputes between nations and he will settle their arguments. [Then, instead of fighting against each other], they will hammer their swords into plow blades, and they will hammer their spears into pruning knives. [The armies of] nations will no longer fight against each other, and they will not [even] train men to fight in battles/wars.”
Atahukumu kati ya mataifa na ataamua migogoro ya mataifa mengi. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
5 You Israeli people, let’s walk in the light [MET] that comes from Yahweh!
Njooni, enyi nyumba ya Yakobo, tutembeeni katika nuru ya Bwana.
6 [Yahweh, ] you have abandoned [us] your people who are descendants of Jacob, because everywhere your people practice the customs of people who live east [of Israel]. Your people also perform rituals to find out what will happen in the future, like the people in Philistia do. They make agreements/treaties with (pagans/people who do not know you).
Umewatelekeza watu wako, nyumba ya Yakobo. Wamejaa ushirikina utokao Mashariki, wanapiga ramli kama Wafilisti na wanashikana mikono na wapagani.
7 Israel is full of silver and gold; there are very many (treasures/valuable things) here. The land is full of war horses and war chariots.
Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.
8 [But] the land is [also] full of idols; the people worship things that they have made with their own hands.
Nchi yao imejaa sanamu, wanasujudia kazi za mikono yao, vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.
9 So now they will be humbled and they will be caused to become disgraced— Yahweh, do not forgive them!
Kwa hiyo mwanadamu atashushwa na binadamu atanyenyekezwa: usiwasamehe.
10 All you people should crawl into [the caves in] the rock cliffs! You should hide [in pits/holes] in the ground because of being afraid of Yahweh and of his glorious and awesome power.
Ingieni kwenye miamba, jificheni ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake!
11 Yahweh will cause you people to no longer be arrogant, and he will stop you from being proud. Only Yahweh will be praised/honored on that day.
Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa na kiburi cha wanadamu kitashushwa, Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.
12 The Commander of the armies of angels has chosen a day when [he will judge] those who are proud, every one of them [DOU], and he will humble them.
Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa),
13 [He will get rid of all those who think they should be admired like] [MET] the tall cedar trees in Lebanon, and [like] all the great oak trees in the Bashan [region].
kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani,
14 He will [get rid of all those who think they are as great as] [MET] all the high hills and even the high mountains.
kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka,
15 He will [get rid of all those who think that they are] high towers and high strong walls [inside of or behind which they will be safe].
kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome,
16 He will destroy all [those who are rich because they own] big ships that carry goods [to other countries] and [they own other] beautiful ships.
kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari.
17 He will cause people to no longer be arrogant and he will cause them to stop being proud. Only Yahweh will be praised/honored on that day.
Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,
18 All idols will (disappear/be destroyed).
nazo sanamu zitatoweka kabisa.
19 When Yahweh comes to shake/terrify the people on the earth, they will run to hide in caves in rock cliffs and in holes/pits in the ground, because of being afraid of Yahweh and of his glorious and awesome power.
Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
20 On that day, people will get rid of all their gold and silver idols that they made to worship, and they will throw them to the bats and rats.
Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu.
21 Then they will crawl into caves and hide in the crags in the cliffs. [They will do that to escape from] the dreadful [punishments] that Yahweh will cause them to endure, from [what he will do because] he is glorious and awesome, when he comes to shake/terrify the people on the earth.
Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
22 [So, ] do not trust that people [will save you], because people are [as powerless as] [MET] their own breath. People certainly cannot help you [RHQ]!
Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?

< Isaiah 2 >