< Isaiah 17 >

1 [I received] this message [from Yahweh] about Damascus [the capital of Syria]: “Listen carefully! Damascus will no longer be a city; it will be [only] a heap of ruins!
Neno kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
2 The towns near Aroer [city] will be abandoned. Flocks [of sheep] will [eat grass in the streets and] lie down there, and there will be no one to chase them away.
Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
3 The cities in Israel will not have walls around them [to protect them]. The power of the kingdom of Damascus will be ended, and the few people who will remain in Damascus will be disgraced like the people in Israel were disgraced.” [That is what] the Commander of the armies of angels says.
Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 “At that time, Israel will become insignificant. It will be [like] [MET] a fat person who has become very thin.
“Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
5 The entire land will be like [SIM] a field where the harvesters have cut all the grain; there will be nothing left, like [SIM] the fields in the Rephaim Valley after all the crops have been harvested.
Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
6 Only a few of the Israeli people will remain [MET], like [SIM] the few olives that remain on the top of a tree after the workers have caused all the other olives to fall [to the ground]. [There will be only] two or three olives in the top branches, [or] four or five olives on the other branches.” [That is what] the Commander of the armies of angels says.
Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yazaayo sana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli.
7 [Then], at that time, [you] people [of Israel] will (turn for help to/look up to) God, your creator, the Holy One of Israel.
Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 You will no [longer] seek to get help from your idols or worship the idols that you have made with your own hands [DOU]. You will never again bow down in front of the poles [where you worship the goddess] Asherah. You will never again worship at the shrines [that you have built for burning incense].
Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
9 The largest cities in Israel will be abandoned, like the land that the Hiv and Amor people-groups abandoned (OR, like the forests that the [Canaan people-group] abandoned) when the Israelis [attacked them long ago]. No one will live there.
Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
10 [That will happen] because you have stopped worshiping God who is [like] [MET] a huge rock under which you can be safe. You have forgotten that he is the one who can hide/protect you. So, [now] you plant very nice grapevines and [even] plant very expensive ones that come from other countries.
Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
11 [But] even if they sprout leaves on the day that you plant them, and even if they produce blossoms on that same morning, at harvest time, there will not be any grapes for you to pick. All that you will get is a lot of agony/misery.
hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
12 Listen! [The armies of] many nations will roar like the sea roars. It will sound like the noise of crashing waves.
Lo! Ghadhabu ya mataifa mengi, wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Lo! Makelele ya mataifa wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
13 But even though their loud roaring will be like the sound of crashing waves, when Yahweh rebukes them, they will run far away. They will flee like [SIM] chaff on the hills scatters when the wind [blows], like tumbleweeds scatter when a windstorm blows.
Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anapoyakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani livingirishwapo na dhoruba.
14 And, even though you people of Israel will be terrified, in the morning [your enemies] will all be gone/dead. That is what will happen to those who invade our land and [then] steal our possessions.
Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyangʼanya mali zetu.

< Isaiah 17 >