< Isaiah 10 >

1 Terrible things will happen to you judges who are unjust and who make unfair laws.
Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
2 You refuse to help poor people, and you do not allow them to get the things that they should get. You [allow people to] steal things from widows and do unfair things to orphans.
kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
3 When I punish you by sending people from distant lands to cause you to experience disasters, (to whom will you run to get help?/there will be no one who can help you.) [RHQ] Your valuable possessions will certainly [not be safe] [RHQ] anywhere.
Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
4 You will be able only to stumble along as you are taken away with other prisoners, or [else] your corpses will lie on the ground with others who have been killed. But even after that happens, Yahweh will still be very angry with you. He will still be ready to strike you again with his fist.
Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
5 [Yahweh says], “Terrible things will happen to Assyria. [It is true that their army] is like a rod/club [DOU] with which I [punish other nations] because I am very angry with those nations [DOU].
“Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
6 [Sometimes] I send the armies of Assyria to attack a godless nation, to fight against [other] people who have caused me to be angry. I send them to capture people and to seize and take away their possessions, and to trample them like [SIM] people walk on mud in the streets.
Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
7 But the [king of Assyria] does not understand, he does not realize [that he is only like a weapon in my hand]. He wants [only] to destroy people, to get rid of many nations.
Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
8 He says, ‘All of my army commanders will soon be kings [of these nations that I conquer]!
Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
9 We destroyed Calno [city] like we destroyed Carchemish [city], We destroyed Hamath [city] like we destroyed Arpad [city]; we destroyed Samaria just like we destroyed Damascus.
Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
10 We were able to destroy [all] those kingdoms [that were full] of idols, kingdoms whose idols were greater than the idols in Jerusalem and Samaria.
Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
11 So we will defeat Jerusalem and destroy the idols that are there, just like we destroyed Samaria and the idols that were there!’
je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
12 [But, I, Yahweh, say that] after I [have used Assyria to] finish what I want to do to punish the people in Jerusalem [DOU], I will punish the king of Assyria because he has been very proud and arrogant/boastful [DOU].
Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
13 He says, ‘By my own great power [MTY] I have done these things. I have been able to do them because I am very wise and very intelligent. My army removed the barriers [at the borders] of nations and carried away all their valuable things. My army has knocked down their kings like [SIM] a ferocious bull would.
Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
14 Like [MET] a farmer reaches into a bird’s nest [to take away the eggs], we have taken away the treasures of other countries [DOU]. The people were not like birds that would flap their wings or chirp loudly [to protest about their eggs being stolen]; the people did not object at all [to their treasures being stolen].’
Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
15 [But I, Yahweh, say that] an axe certainly cannot [RHQ] boast about being stronger than the person who uses it, and a saw is not greater than the person who uses it. A rod cannot control the one who holds it [RHQ], and a wooden club cannot lift up a person [RHQ]. [So the king of Assyria should not boast that he has done these things with his own wisdom and strength].
Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
16 And [I], the Commander of the armies of angels, will send a plague among the proud soldiers of Assyria; it will be like [MET] a fire that will kill them and get rid of their glory/wealth.
Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
17 [I], Yahweh, who am like [MET] a light for the people of Israel, will be the fire; [I], the Holy One, will be like a flame. [The soldiers of Assyria are like] [MET] thorns and briers, and I will burn them up in one night.
Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
18 There are glorious forests and fertile farmlands in Assyria, but I will completely destroy them; they will be like [SIM] a [very] sick person who shrivels up and then dies.
Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
19 There will be very few trees left in those forests; even a child will be able to count them.”
Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
20 In the future there will be only a few people left in Israel; not many descendants of Jacob will still be alive. [But] they will no longer rely on [the king of Assyria], [the king of the nation] that tried to destroy them. Instead, they will faithfully/sincerely trust in Yahweh, the Holy One of Israel.
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21 Those Israelis will return to their mighty God.
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22 [Now], the people of Israel are as numerous as the grains of sand on the seashore, but only a few of them will return [from the countries to which they were exiled]. Yahweh has decided to destroy [most of the Israelis] and that is what [he must do because he is completely] just/righteous.
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23 [Yes, ] the Commander of the armies of angels has [already] decided to destroy the entire land [of Israel].
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
24 This is what the Commander of the armies of angels says: “My people in Jerusalem, do not be afraid of the army of Assyria when they beat you with rods and clubs, like the men of Egypt did [to your ancestors long ago].
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
25 Soon I will no longer be angry with you, and [then] I will be angry with the people of Assyria and destroy them!”
Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
26 The Commander of the armies of angels will whip them. He will do to them like he did when he helped Gideon [and his 300 soldiers] to defeat the [army of the] Midian people-group, and like he did when he showed his mighty power [MTY] [by causing the army of Egypt to drown] in the [Red] Sea.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
27 Some day, Yahweh will cause the army of Assyria to stop oppressing you, [his people]; he will end your suffering and your being slaves of the people of Assyria [MET]; he will take away the load that you people of Judah have been carrying, and cause things to go well for you.
Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
28 [The army of Assyria will enter northern Judah] near Aiath [town], they will go through Migron [town] and store their supplies at Micmash [town north of Jerusalem].
Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
29 They will cross through a mountain pass and set up their tents at Geba [town]. [People in] Ramah [town] will tremble [because of being afraid]. [The people of] Gibeah [town], where King Saul [was born], will [all] run away.
Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
30 You people of Gallim [town] will cry out [for help]. You will shout to [the people of] Laish [city near Jerusalem] to warn them! [The people of] Anathoth [town] will suffer a lot.
Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
31 [The people of] Madmenah [town north of Jerusalem will all] be running away, and [the people of] Gebim [town close to Jerusalem] will be trying to hide.
Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
32 The soldiers of Assyria will stop at Nob [city outside Jerusalem]. They will shake their fists [as they threaten the people] on Zion Hill in Jerusalem.
Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
33 But listen to this! The Commander of the armies of angels with his great power will destroy [MET] the mighty army of Assyria. [It is as though they are] a huge tree [MET] that he will cut down.
Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
34 He will destroy the [soldiers of Assyria] like men use big axes to cut down the tall trees in the forests of Lebanon.
Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

< Isaiah 10 >