< Hebrews 8 >

1 The main point of [all] that [I] have written is that we have a Supreme Priest like that. He has sat down to rule [MTY] with God [EUP] at the place of greatest honor in heaven.
Basi jambo tunalotaka kulisema ni hili: Tunaye Kuhani Mkuu ambaye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Aliye Mkuu mbinguni,
2 He ministers in the Most Holy Place, that is, in the true place [of worship in heaven]. That is a place that [Moses’] tent [represented]. The Lord set up the true place of worship. No human [set it up].
yeye ahudumuye katika patakatifu, hema la kweli lililowekwa na Bwana, wala si na mwanadamu.
3 Every Supreme Priest was appointed {[God] appointed every Supreme Priest} to offer [to God] gifts and sacrifices [for people who sinned]. So, since [Christ became a Supreme Priest], he also had to offer something.
Kila kuhani mkuu huwekwa ili atoe sadaka na dhabihu. Vivyo hivyo, ilikuwa jambo muhimu kwa huyu Kuhani naye awe na kitu cha kutoa.
4 Since there are already [Jewish] priests who offer gifts as God’s laws [require], if Christ were [now living] on the earth, he would not be a Supreme Priest.
Kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani, kwa sababu tayari wapo watu watoao sadaka kama ilivyoelekezwa na sheria.
5 The [Jewish] priests perform rituals which are only a model [DOU] of [what Christ would do in heaven] [MTY]. What [God] told Moses when Moses was about to set up the tent [for worshipping him supports the idea that those rituals were only a model. God said], “Be sure that you [(sg)] make everything according to the model that I showed you on [Sinai] Mountain!”
Wanahudumu katika patakatifu palipo mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni. Hii ndiyo sababu Mose alionywa alipokaribia kujenga hema, akiambiwa: “Hakikisha kuwa unavitengeneza vitu vyote kwa mfano ulioonyeshwa kule mlimani.”
6 But now as it is, [Christ] ministers in a more excellent way [than the Jewish priests do]. Likewise, the [new] covenant that he established [between God and people] is better [than the old one. When the new covenant was established] {[God established the new covenant]}, he promised us better things [than the laws that God gave Moses did].
Lakini huduma aliyopewa Yesu ni bora zaidi kuliko yao, kama vile agano ambalo yeye ni mpatanishi wake lilivyo bora zaidi kuliko lile la zamani, nalo limewekwa misingi wa ahadi zilizo bora zaidi.
7 If that first covenant had been perfectly adequate [LIT], God would not have thought that he needed another [covenant/agreement to replace it]. But [it was not adequate, so he needed a new one].
Kwa maana kama hapakuwa na kasoro katika lile agano la kwanza, pasingekuwa na haja ya kutafuta nafasi kwa ajili ya jingine.
8 Because God declared [that the Israelites] were guilty [of not obeying the first covenant, he wanted a new covenant. This is what] ([a prophet/Jeremiah]) [wrote about that]: The Lord says, “Listen! There will soon be a time when I will make a new covenant with the people [MTY] of Israel and the people [MTY] of Judah.
Lakini Mungu aliona kosa kwa watu, naye akasema: “Siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.
9 That covenant will not be like the covenant that I made with their ancestors when I led them out of Egypt [MET] [like a father leads a child] by the hand. They did not continue to [obey] my covenant, so I rejected them,” says the Lord.
Agano langu halitakuwa kama lile nililofanya na baba zao nilipowashika mkono kuwaongoza watoke nchi ya Misri, kwa sababu hawakuendelea kuwa waaminifu katika agano langu, nami nikawaacha, asema Bwana.
10 “This is the covenant that I will make with the Israelites [MTY], after [the first covenant has ended] [MTY],” says the Lord: “I will enable them to understand my laws [MTY], and I will enable them to obey them (OR, truly know them) [MTY] sincerely. I will be their God, and they will be my people [DOU].
Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku zile, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu katika nia zao na kuziandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
11 [As a result], no one will [need to] teach a fellow citizen or tell his fellow kinsmen, ‘[You need to] know the Lord,’ because all [my people] will know me: [My people] of every status [will know me].
Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana,’ kwa sababu wote watanijua mimi, tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana.
12 I will mercifully [forgive them for] the wicked things they have done. I will no longer [consider] that [they are guilty for] [DOU] [their] sins.”
Kwa sababu nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”
13 Since God spoke about a new [covenant], he considered that the first [covenant] was no longer in use, and that it would soon disappear, just like [anything that] gets old [will disappear] [MET, DOU].
Kwa kuliita agano hili “jipya,” Mungu amefanya lile agano la kwanza kuwa kuukuu; nacho kitu kinachoanza kuchakaa na kuwa kikuukuu kiko karibu kutoweka.

< Hebrews 8 >