< Genesis 8 >

1 But God (did not forget/thought) about Noah and all the wild animals and all the kinds of livestock that were with him in the boat. So one day God sent a wind to blow across the earth, and the wind caused the water [to begin] to recede.
Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
2 God caused the water that was under the earth to stop bursting forth, and he caused the floodgates of water from the sky to close so that it stopped raining.
Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
3 The water on the earth gradually receded. 150 days after the flood began,
Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
4 (on the 17th day of the seventh month [of that year/late in March]), the boat came to rest on one of the mountains in the Ararat region.
katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
5 The water continued to recede until, on the first day of the tenth month [of that year], the tops of other mountains became visible.
Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
6 40 days later, Noah opened the window that he had made in the side of the boat, and sent out a raven.
Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina
7 The raven flew back and forth [to and from the boat] until the water was completely gone.
na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi.
8 Then Noah sent out a dove to find out if the water had all receded on the ground.
Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi.
9 But the dove did not find any place to perch, so it flew back to Noah in the boat, because there was still water all over the surface of the earth. So Noah reached out his hand and took the dove back inside the boat.
Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina.
10 Noah waited seven more days. Then he sent the dove out of the boat again.
Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina.
11 This time the dove returned to him in the evening and, [surprisingly], in its beak there was a leaf from an olive tree that the dove had just plucked. Then Noah knew that the water had truly receded from the surface of the ground.
Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia.
12 Noah waited seven more days. Then he sent the dove out again, but this time it did not return to him.
Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.
13 Noah was now 601 years old. By the first day of the first month [of the Jewish year], the water had completely drained away from the ground. Noah removed the covering on top of the ark, and he was surprised to see that the surface of the ground was drying.
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka.
14 By the 27th day of the next month, the ground was completely dry.
Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.
15 Then God said to Noah,
Ndipo Mungu akamwambia Noa,
16 “Leave the boat, along with your wife and your sons and their wives.
“Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao.
17 Bring out with you all the birds, the animals, and all the creatures that scurry across the ground, in order that they can spread all over the earth and become very numerous.”
Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”
18 So Noah left the boat, along with his wife and his sons and their wives.
Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao.
19 And every kind of creature, including all those that scurry across the ground, all the birds, every creature that moves on the earth, left the boat. They left the boat in groups of their own species.
Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.
20 Then Noah built a (stone altar/place for offering sacrifices) to Yahweh. Then he took some of the animals that Yahweh had said were acceptable as sacrifices and killed them. Then he burned them whole on the altar.
Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
21 When Yahweh smelled the pleasant odor, he was pleased with the sacrifice. Then he said to himself, “I will never again devastate everything on the earth because of the sinful things people do. Even though everything that people think is evil from the time they are young, I will not destroy all the living creatures again, as I did this time.
Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.
22 As long as the earth exists, each year there will be seasons for planting seeds and seasons for harvesting crops. Each year there will be times when it is cold and times when it is hot, summer and winter (OR, rainy season and dry season). Each day there will be daytime and nighttime.”
“Kwa muda dunia idumupo, wakati wa kupanda na wa kuvuna, wakati wa baridi na wa joto, wakati wa kiangazi na wa masika, usiku na mchana kamwe havitakoma.”

< Genesis 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark