< Genesis 41 >

1 Two complete years later, the king of Egypt had a dream. In the dream, he was standing alongside the Nile [River].
Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
2 Suddenly seven healthy fat cows come up out of the river. They started eating the grass that was on the riverbank.
wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
3 Soon seven other cows, unhealthy-looking and thin, came up behind them from the Nile [River]. They stood alongside the fat cows that were on the riverbank.
Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
4 Then the unhealthy thin cows ate the seven healthy fat cows. And then the king woke up.
Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
5 The king went to sleep again, and he had another dream. This time he saw seven heads of grain that were full of kernels of grain and ripe, and all growing on one stalk.
Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
6 After that, the king saw that seven other heads of grain sprouted on that (OR, on another) stalk. They were thin and had been dried up by the hot east wind.
Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
7 Then the thin heads of grain swallowed up the seven ripe full heads. Then the king woke up. He realized that he had been dreaming.
Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
8 But the next morning he was worried about the meaning of the dream. So he summoned all the magicians and wise men who lived in Egypt. He told them what he had dreamed, but none of them could tell him the meaning of the two dreams.
Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
9 Then the chief drink-server said to the king, “Now I remember something that I should have told you! I made a mistake by forgetting to tell it to you.
Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
10 One time you were angry with two of us. So you put me and the chief baker in the prison in the house of the captain of the palace guards.
Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
11 While we were there, one night each of us had a dream, and the dreams had different meanings.
Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
12 There was a young Hebrew man there with us. He was a servant of the captain of the palace guards. We told him what we had dreamed, and he told us what our dreams meant. He told each of us the meaning of our dreams.
Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
13 And what happened was exactly the same as the meanings that he told us: You said I could have my previous job again, but the other man was killed by being hanged. [The Hebrew man’s name was Joseph].”
Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
14 When the king heard that, he told some servants to bring Joseph to him, and they quickly brought Joseph out of the prison. Joseph shaved and put on better clothes, and then he went and stood in front of the king.
Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
15 The king said to Joseph, “I had two dreams, and no one can tell me what they mean. But someone told me that when you hear someone tell about a dream he has had, you can tell that person what the dream means.”
Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
16 But Joseph replied to the king, “No, I cannot do that. It is God who knows the meaning of dreams, but he will enable me to tell you their meaning, and they will mean something good.”
Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
17 The king said to Joseph, “In my first dream I was standing on the bank of the Nile [River].
Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
18 Suddenly seven healthy fat cows came up out of the river, and they started eating the grass that was on the riverbank.
nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
19 Soon seven other cows, ugly and thin ones, came up behind them from the river. I never saw such ugly cows in all the land of Egypt!
Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
20 The thin ugly cows ate the seven fat cows that came up first.
Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
21 But afterwards, no one would have known that the thin cows ate them, because they were just as ugly as they were before. Then I woke up.
Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
22 Then I had another dream. I saw seven heads of grain. They were full of kernels of grain and ripe, and they were all growing on one stalk.
“Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
23 Then [to my surprise] I saw seven other heads of grain that sprouted. They were thin and had been dried up by the hot east wind.
Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
24 The thin heads of grain swallowed the seven good heads. I told these dreams to the magicians, but none of them could explain to me what they meant.”
Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
25 Then Joseph said to the king, “Both your dreams have the same meaning. God is revealing to you in your dreams what he is about to do.
Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
26 The seven healthy cows represent seven years. The seven good heads of grain also represent seven years. The two dreams both have the same meaning.
Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
27 The seven thin ugly cows that came up behind them and the seven worthless heads of grain that were dried up by the hot east wind each represent seven years (of famine/when food will be very scarce).
Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
28 It will happen just as I have told you, because God has revealed to you what he is about to do.
“Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
29 There will be seven years in which there will be plenty of food throughout the land of Egypt,
Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
30 but after that there will be seven years (of famine/when food will be very scarce). Then people will forget all the years when there was plenty of food, because the famine that will come afterward will ruin the country.
lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
31 The people will forget how plentiful food was previously, because the famine will be very terrible.
“Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
32 The reason God gave to you two dreams is that he [wants you to know] that this will happen, and he will cause it to happen very soon.
Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
33 “Now I suggest that you should choose a man who is wise and can make good decisions. I suggest that you appoint him to direct the affairs of the whole country.
“Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
34 You should also appoint supervisors over the country, in order that they can arrange to collect one-fifth of all the grain that is harvested during the seven years when food is plentiful.
Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
35 They should collect this amount of grain during those seven years that are coming, when there will be plenty of food. You should supervise them as they store it in the cities.
Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
36 This grain should be stored so that it can be eaten during the seven years when there will be a famine here in Egypt, so that the people in this country will not die from hunger.”
Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
37 The king and his officials thought that this would be a good plan.
Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
38 So the king said to them, “(Can we find any other man like Joseph, a man to whom God has given his Spirit?/It is not likely that we will find another man like this man, one to whom God has given his Spirit!)” [RHQ]
Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
39 Then the king said to Joseph, “Because God has revealed all this to you, it seems to me that there is no one who is as wise as you and who can decide wisely about things.
Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
40 So I will put you in charge of everything in my palace. All the people here in Egypt must obey what you command. Only because I am king [MTY] will I have more authority than you.”
Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
41 Then the king said to Joseph, “I am now putting you in charge of the whole country of Egypt.”
Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
42 The king took from his finger the ring that had his seal on it, and he put it on Joseph’s finger. He put robes made of fine linen on him, and he put a gold chain around his neck.
Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
43 Then he arranged for Joseph to ride around in the chariot [that showed that he was] the second-most important man in the country. When Joseph rode in the chariot, men shouted to the people who were on the road in front of him, “Get off the road!” So the king put Joseph in charge of everything in the country.
Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
44 The king said to Joseph, “I am the king, but no one in the whole land of Egypt will do anything [IDM] if you do not permit them to do it.”
Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
45 The king gave Joseph a new name, Zaphenath-Paneah. He also gave him Asenath to be his wife. She was the daughter of Potiphera, who was a priest in a temple in On [city]. Then Joseph became known (OR, traveled) through all the land of Egypt.
Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
46 Joseph was 30 years old when he started to work for the king of Egypt. To do his work, he left the king’s palace and traveled throughout Egypt.
Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
47 During the next seven years, the land produced abundant crops, so there was plenty of food.
Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
48 As Joseph supervised them, his helpers collected one-fifth of all the grain that was produced during those years, and stored it in the cities. In each city, he had his helpers store up the grain that was grown in the fields that surrounded that city.
Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
49 Joseph had them store up a huge amount of grain. It looked as plentiful as the sand on the seashore. There was so much grain that after a while they stopped keeping records of how much grain was stored, because there was more grain than they could measure.
Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
50 Before the seven years of famine started, Joseph’s wife Asenath gave birth to two sons.
Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
51 Joseph named the first one Manasseh, [which sounds like the Hebrew word that means ‘forget]’, because, he said, “God has caused me to forget all my troubles and all my father’s family.”
Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
52 He named his second son Ephraim, [which means ‘to have children]’, because, he said, “God has given me children here in this land where I have suffered.”
Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
53 Finally the seven years in which there was plenty of food ended.
Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
54 Then the seven years of famine started, just as Joseph had predicted. There was also a famine in all the other nearby lands, but although the crops did not grow, there was food everywhere in Egypt, because of the grain they had stored up in the cities.
nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
55 When all the people of [MTY] Egypt had eaten all of their own food and were still hungry, they begged the king for food. So the king told all the people of Egypt, “Go to Joseph, and do what he tells you to do.”
Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
56 When the famine was very bad throughout the whole country, Joseph ordered his helpers to open the storehouses. Then they sold the grain in the storehouses to the people of Egypt, because the famine was very severe all over Egypt.
Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
57 And people from many [HYP] nearby countries came to Egypt to buy grain from Joseph, because the famine was very severe everywhere [HYP].
Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.

< Genesis 41 >