< Genesis 35 >
1 [Some time later] God said to Jacob, “Go up to Bethel, and live there. Build an altar to worship me, God, who appeared to you when you were fleeing from your older brother Esau.”
Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”
2 So Jacob said to his household and to all the others who were with him, “Get rid of the idols you brought from Mesopotamia. Also, bathe yourselves and put on clean clothes.
Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu.
3 Then we will get ready and go up to Bethel. There I will make an altar to worship God. He is the one who helped me at the time when I was greatly distressed and afraid, and he has been with me wherever I have gone.”
Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.”
4 So they gave to Jacob all the idols that they had brought, and all their earrings. Jacob buried them in the ground under the big oak tree that was near Shechem [town].
Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu.
5 As they prepared to leave there, God caused the people who lived in the cities around them to be extremely afraid of Jacob’s family [PRS], so that they did not pursue and attack them.
Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.
6 Jacob and all those who were with him came to Luz, which is now called Bethel, in the Canaan region.
Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani.
7 There he built an altar. He named the place El-Bethel, [which means ‘God of Bethel]’, because it was there that God revealed himself to Jacob when he was fleeing from his older brother Esau.
Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli, kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
8 Deborah, who had taken care of Isaac’s wife Rebekah when Rebekah was a small girl, was now very old. She died and was buried under an oak tree south of Bethel. So they named that place Allon-Bacuth, [which means ‘oak of weeping’].
Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.
9 After Jacob and his family returned from Paddan-Aram/Mesopotamia, while they were still at Bethel, God appeared to Jacob again and blessed him.
Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki.
10 God said to him again, “Your name will no longer be Jacob. It will be Israel.” So Jacob was then called ‘Israel’.
Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.
11 Then God said to him, “I am God Almighty. Produce many children. Your descendants will become many nations, and some of your descendants will be kings.
Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi, ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako.
12 The land that I promised to give to [your grandfather] Abraham and [your father] Isaac, I will give to you. I will also give it to your descendants.”
Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.”
13 When God finished talking there with Jacob, he left him.
Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.
14 Jacob set up a large stone at the place where God had talked with him. He poured some wine and some [olive] oil on it to dedicate it to God.
Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake.
15 Jacob named that place Bethel, [which means ‘house of God]’, because God had spoken to him there.
Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.
16 Jacob and his family left Bethel and traveled south toward Ephrath [town]. When they were still some distance from Ephrath, Rachel began to have severe childbirth pains.
Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu.
17 When her pain was the most severe, the (midwife/woman who helped her to give birth) said to Rachel, “Do not be afraid, because now you have given birth to another son!”
Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.”
18 But she was dying, and with her last breath she said, “Name him Benoni,” [which means ‘son of my sorrow]’, but his father named him Benjamin, [which means ‘son of my right hand]’.
Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni. Lakini babaye akamwita Benyamini.
19 After Rachel died, she was buried alongside the road to Ephrath, which is [now called] Bethlehem.
Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
20 Jacob set up a large stone over her grave, and it is still there, showing where Rachel’s grave is.
Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.
21 Jacob, whose new name was Israel, continued traveling with his family, and he set up his tents on the south side of the watchtower at Eder [town].
Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi.
22 While they were living in that area, Jacob’s son Reuben had sex [EUP] with Bilhah, one of his father’s (concubines/female slaves whom he had taken as a secondary wife). Someone told Jacob about it, and it made him very angry. (I will now give you/Here is) a list of Jacob’s twelve sons.
Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:
23 The sons of Leah were Reuben, who was Jacob’s oldest son, then Simeon, Levi, Judah, Issachar and Zebulon.
Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.
24 The sons of Rachel were Joseph and Benjamin.
Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini.
25 The sons of Rachel’s female slave Bilhah were Dan and Naphtali.
Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali.
26 The sons of Leah’s female slave Zilpah were Gad and Asher. All those sons of Jacob, except Benjamin, were born while he was living in Paddan-Aram/Mesopotamia.
Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.
27 Jacob had returned back home to see his father Isaac at Mamre, which is also named Kiriath-Arba, and which is now named Hebron. Isaac’s father Abraham had also lived there.
Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki.
28 Isaac lived until he was 180 years old.
Isaki aliishi miaka 180.
29 He was very old when he died, joining his ancestors who had died previously. His sons Esau and Jacob buried his body.
Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.