< Genesis 24 >

1 Abraham was now a very old man. Yahweh had blessed Abraham in many ways.
Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
2 One day Abraham said to the chief servant of his household, the man who was in charge of everything Abraham owned, “Put your hand between my thighs to solemnly promise you will do what I tell you.
Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
3 Knowing that Yahweh God [who created] the heavens and the earth is listening, promise that you will not get a wife for my son, Isaac, from the women here in Canaan.
Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
4 Instead, go back to my country and to my relatives and get a wife for my son Isaac from among them.”
bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
5 The servant asked him, “If I find a woman among your relatives, what if she is not willing to come back with me to this land? Shall I take your son back there to the country you came from, [so he can find a wife and live there]?”
Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
6 Abraham replied to him, “No! Be certain that you don’t take my son there!
Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
7 Yahweh God, who created the heavens, brought me here. He brought me from my father’s household, and from the land where my relatives lived. He spoke to me and made a solemn promise to me, saying, ‘I will give this land [of Canaan] to your descendants.’ He will send an angel who will go there ahead of you, and enable you to get a wife for my son [there and bring her to live here].
Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
8 But if the woman you find will not come back with you, you are free to disregard the promise you are making. The only thing that you must not do is to take my son to live there!”
Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
9 So the servant put his hand between Abraham’s thighs and made a solemn promise about the matter.
Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
10 Then the servant took ten of his master’s camels and loaded them with all kinds of goods that his master gave him to take along. Then he left to go to Aram-Naharaim, [which is in (northern Mesopotamia/Syria)]. He arrived in Nahor city.
Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
11 It was late in the afternoon, at the time when the women go to the well to get water, when he arrived there. He made the camels kneel down near the well, which was outside the city.
Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
12 The servant prayed, “Yahweh God whom my master Abraham worships, enable me to be successful today! Act kindly to my master, Abraham!
Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
13 Listen to me. I am standing near a well of water, and the young women of the city are coming to get water.
Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
14 I am asking you this: ‘I will say to some girl, “Please lower your jar so that I may drink some water.” If she says, “Drink some, and I will draw some water [from the well] for your camels, too,” I will know that she is the woman whom you chose to be a wife for your servant, Isaac, and I will know that you have been kind to my master.’”
Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
15 Before he finished praying, [amazingly], Rebekah arrived there, carrying a jar on her shoulder. She was the daughter of Bethuel, who was the son of Milcah, the wife of Abraham’s younger brother Nahor.
Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
16 She was very beautiful and still a virgin. She went down to the edge of the well, filled her jar with water, and then came back up.
Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
17 Abraham’s servant immediately ran to meet her, and said, “Please give me a little water from your jar.”
Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
18 She replied, “Drink some, sir!” She lowered her jar from her shoulder to her hands and gave him a drink.
Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
19 After she had finished giving him a drink, she said, “I will also get some water for your camels, until they have had enough to drink.”
Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
20 She quickly emptied the water in her jar into the trough [for giving water to animals], and then ran back to the well, and kept getting water for all the camels.
Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
21 The servant just watched her, without saying anything. He wanted to know if Yahweh had caused his trip to be successful or not.
Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
22 Finally, after the camels finished drinking, the servant took out a gold nose ring that weighed (two ounces/6 grams), and two large gold bracelets for her arms, and gave them to Rebekah [and told her to put them on].
Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
23 Then he said, “Tell me whose daughter you are. Also, tell me, is there room in your father’s house for me and my men to sleep there tonight?”
Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
24 She replied, “My father’s name is Bethuel. He is the son of Nahor and his wife Milcah.
Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
25 Yes, we have room where you all can sleep tonight, and we also have plenty of straw and grain to feed the camels.”
Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
26 The servant bowed and worshiped Yahweh.
Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
27 He said, “I thank you, Yahweh God, whom my master Abraham worships. You have continued to be kind and faithful to my master. You led me on this journey straight/directly to the house of my master’s relatives!”
akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
28 The girl ran and told everyone in her mother’s household about what had happened.
Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
29 Rebekah had a brother whose name was Laban. Laban went quickly to Abraham’s servant, who was still by the well.
Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
30 He was surprised to have seen the bracelets on his sister’s arms and the nose ring and to have heard Rebekah tell what the man had said to her. So he went out and saw the man standing near the camels, close to the well.
Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
31 He said to the man, “You who have been blessed by Yahweh, come with me! (Why are standing out here?/You should not keep standing out here!) [RHQ] I have prepared a room for you in the house, and a place for the camels to stay.”
Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
32 So the servant went to the house, and Laban’s servants unloaded the camels, and brought straw and grain for the camels, and water for him and the men with him to wash their feet.
Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
33 They set food in front of him for him to eat, but he said, “I will not eat until I tell you (what I need to tell you/why I have come).” So Laban said, “Tell us!”
Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
34 So the servant said, “I am Abraham’s servant.
Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
35 Yahweh has greatly blessed my master so that he has become very rich. Yahweh has given him many sheep and cattle, a lot of gold and silver, male and female servants, camels and donkeys.
Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
36 My master’s wife, Sarah, bore a son for him when she was very old, and my master has given to his son everything he owns.
Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
37 My master made me solemnly promise, saying, ‘Do not get a wife for my son from the women here in Canaan.
Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
38 Instead, go back to my father’s family, to my own clan, and get from them a wife for my son.’
ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
39 Then I asked my master, ‘What shall I do if the woman you show me will not come back with me?’
“Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
40 He replied, ‘Yahweh, whom I have always obeyed [MTY], will send his angel with you, and he will cause your journey to be successful, with the result that you can get a wife for my son from my clan, from my father’s family.
“Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
41 But if my clan refuses to allow her to return with you, you will be freed from being cursed because of not obeying me.’
Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
42 “When I came today to the well, I prayed, ‘Yahweh God whom my master, Abraham worships, if you are willing, please allow this journey of mine to be successful.
“Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
43 Listen to me. I am standing beside a well. A young woman may come to draw water. I will say to her, “Please, give me a little water to drink from your jar.”
Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
44 If she says to me, “Certainly, drink some! And I will also draw some water for your camels,” that will be the woman whom you have chosen for my master’s son!’
naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
45 Before I finished praying, [amazingly], Rebekah approached with her water jar on her shoulder. She went down to the well and got some water. I said to her, ‘Please give me a drink!’
“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
46 She quickly lowered her jar and said, ‘Drink some! And I will draw water [from the well] for your camels, too.’ So I drank some water, and she also got water for the camels.
“Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
47 Then I asked her, ‘Whose daughter are you?’ She said, ‘The daughter of Bethuel, the son of Nahor and his wife, Milcah.’ I had [a ring and bracelets with me, and] I put the ring in her nose and put the bracelets on her arms.
“Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
48 Then I bowed and worshiped Yahweh, and I thanked Yahweh God, the one my master Abraham worships, the one who led me on the right road to get the granddaughter of my master’s brother to be a wife for my master’s son.
nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
49 Now, if you are kind and faithful to my master, tell me that you will do what I am asking. If you will not do that, tell me that also, so I may know what to do [MTY].”
Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
50 Laban and Bethuel answered, “It is clear that Yahweh has caused this to happen. So we two cannot say anything more.
Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
51 Rebekah is here in front of you. Take her and go, and let her be a wife for your master’s son, just as Yahweh has indicated.”
Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
52 When Abraham’s servant heard these words, he bowed down to the ground to [thank] Yahweh.
Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
53 Then the servant brought out silver and gold jewelry and clothes, and gave them to Rebekah. And he gave gifts to her brother Laban and to her mother.
Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
54 Then they ate a meal together. The men who were with Abraham’s servant also slept there that night. The next morning, the servant said, “Allow me now to return to my master.”
Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
55 But her brother and her mother replied, “Let the girl remain with us for about ten days. After that, you may take her and go.”
Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
56 But he replied to them, “Yahweh has made my journey successful, so do not detain me. Let me take her back to my master now!”
Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
57 They said, “Let’s call Rebekah and ask her what she wants to do.” [MTY]
Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
58 So they summoned Rebekah and asked her, “Will you go with this man now?” She replied, “Yes, I will go.”
Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
59 So they allowed Rebekah, a woman who had taken care of her when she was very young, Abraham’s servant, and the men who had come with him. to go.
Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
60 Before they all left, they [asked God to] bless Rebekah, and said to her, “Our sister, we ask that Yahweh will cause you to have millions of descendants, and allow them to completely defeat [MET] all those that hate them.”
Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
61 Then Rebekah and her maid servants got ready and got on their camels and went with Abraham’s servant.
Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
62 At that time, Isaac was living in the Negev desert. He had gone there from Beer-Lahai-Roi.
Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
63 One evening he went out into the field to meditate as he walked. He looked up and [was surprised to] see some camels coming.
Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
64 Rebekah also looked up and saw Isaac. She got off the camel,
Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
65 and asked the servant, “Who is that man who is approaching?” The servant replied, “That is Isaac, my master, [the man you will be marrying].” So she took her veil and covered her face, which was the custom for a woman who was about to be married.
na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
66 The servant told Isaac everything that had happened.
Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
67 Then Isaac took Rebekah into the tent that belonged to his mother, Sarah, and she became his wife. And he loved her. So Isaac was comforted about his mother’s death.
Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.

< Genesis 24 >