< Genesis 19 >

1 That evening, the two angels arrived in Sodom. Lot was sitting at the gateway of the city. When he saw them, he got up to greet them, and prostrated himself with his face on the ground.
Malaika wale wawili wakafika Sodoma wakati wa jioni, naye Loti alikuwa ameketi kwenye lango la mji. Wakati alipowaona, aliondoka kwenda kuwalaki na kuwasujudia hadi chini.
2 He said to them, “Gentlemen, please stay in my house tonight. You can wash your feet, and tomorrow you can continue your journey.” But they said, “No, we will just sleep in the city square.”
Akasema, “Bwana zangu, tafadhali karibuni kwenye nyumba ya mtumishi wenu. Mnaweza kunawa miguu na kulala hapa kisha asubuhi na mapema mwendelee na safari yenu.” Wakamjibu, “La hasha, tutalala hapa nje uwanjani.”
3 But Lot kept insisting strongly that they sleep in his house. So they entered his house with him, and he prepared a meal for them. He baked some bread without yeast, and they ate it.
Lakini akasisitiza kwa nguvu kwamba waingie pamoja naye nyumbani kwake. Akawaandalia chakula, mikate isiyotiwa chachu, nao wakala.
4 After they finished eating, before they went to bed, the men of Sodom [city], all of them, from the young ones to the old ones, surrounded the house.
Kabla hawajaenda kulala, watu wote kutoka kila sehemu ya mji wa Sodoma, vijana kwa wazee, waliizunguka nyumba.
5 They called out to Lot, saying, “Where are the men who came to your house this evening? Bring them out, so that we can have sex with them!” [EUP]
Wakamwita Loti wakisema, “Wako wapi wale watu ambao walikuja kwako jioni hii? Watoe nje kwetu ili tuweze kuwalawiti.”
6 Lot went outside the house and shut the door behind him, so that they could not go inside.
Loti akatoka nje kuonana nao, akaufunga mlango nyuma yake,
7 He said to them, “My friends, don’t do such an evil thing!
akasema, “La hasha, rafiki zangu. Msifanye jambo hili ovu.
8 Listen to me. I have two daughters who have never had sex with any man. Let me bring them out to you now, and you can do with them whatever pleases you. But don’t do anything to these men, because they are guests in my house, [so I must protect them]!”
Tazama, ninao binti wawili ambao kamwe hawajakutana kimwili na mwanaume. Acha niwatoe nje kwenu, nanyi mnaweza kuwafanyia lolote mnalotaka. Lakini msiwafanyie chochote watu hawa, kwa sababu wako kwenye ulinzi chini ya dari langu.”
9 But they replied, “Get out of our way! You are a foreigner; so you have no right to tell us what is right! [If you don’t get out of our way], we will do worse things to you than we will do to them!” Then they lunged towards Lot, and tried forcefully to break down the door.
Wakamjibu, “Tuondokee mbali.” Wakaendelea kusema, “Huyu mtu alikuja hapa kama mgeni na sasa anataka kuwa mwamuzi wetu! Tutakutenda vibaya kuliko wao.” Waliendelea kumlazimisha Loti na kusonga mbele ili kuvunja mlango.
10 But the two angels opened the door carefully, reached out their hands, and pulled Lot to them inside the house. Then they quickly shut the door.
Lakini watu wale waliokuwa ndani wakanyoosha mkono wakamvuta Loti ndani ya nyumba na kufunga mlango.
11 Then they caused all the men who were outside the door of the house, young and old, to become blind, so that they could not find the door.
Kisha wakawapiga kwa upofu wale watu waliokuwa mlangoni mwa ile nyumba, vijana kwa wazee, hivyo hawakuweza kuupata mlango.
12 Then the two angels said to Lot, “Who else is with you here? If you have sons or sons-in-law or daughters or anyone else in the city who is related to you, take them out of the city,
Wale watu wawili wakamwambia Loti, “Una mtu mwingine yeyote hapa, wakwe zako, wana au binti, ama yeyote mwingine aliye wako katika mji huu? Waondoe hapa,
13 because we are the ones who are going to destroy this place. Yahweh considers that these people are so evil that he sent us to destroy the city.”
kwa sababu tunapaangamiza mahali hapa. Kilio kwa Bwana dhidi ya watu wa hapa ni kikubwa kiasi kwamba ametutuma kupaangamiza.”
14 So Lot went and spoke to the men who had pledged to marry his daughters. He said to them, “Hurry! Get out of this city, because Yahweh is about to destroy it!” But his future sons-in-law thought he was joking.
Kwa hiyo Loti alitoka ili kuzungumza na wakwe zake, waliokuwa wamewaposa binti zake. Akawaambia, “Fanyeni haraka kuondoka mahali hapa, kwa kuwa Bwana yu karibu kuangamiza mji huu!” Lakini wakwe zake walifikiri kwamba alikuwa akitania.
15 As it was about to dawn the next morning, the two angels urged Lot, saying, “Get up quickly! Take your wife and your two daughters who are here with you and leave! If you don’t, you will die when [we destroy/Yahweh destroys] the city!”
Kunako mapambazuko, malaika wakamhimiza Loti, wakamwambia, “Fanya haraka! Mchukue mke wako na binti zako wawili walioko hapa, la sivyo utaangamizwa wakati mji utakapoadhibiwa.”
16 When Lot hesitated, the angels grasped his hand and his wife’s hand and the hands of his two daughters. They led them outside the city safely. The angels did that because Yahweh was acting mercifully toward them.
Alipositasita, wale watu wakamshika mkono wake na mikono ya mke wake na binti zake wawili na kuwaongoza salama nje ya mji, kwa kuwa Bwana alikuwa na huruma kwao.
17 When they were outside the city, one of the angels said, “[If you want to remain alive], run away quickly! Don’t look back! And don’t stop anywhere in the valley! Flee to the hills! If you don’t, you will die!”
Mara walipokwisha kuwatoa nje, mmoja wao akawaambia, “Mkimbie kwa usalama wenu! Msitazame nyuma, wala msisimame popote katika nchi tambarare! Kimbilieni milimani, ama sivyo mtaangamizwa!”
18 But Lot said to one of the angels, “No, sir, don’t make me do that!
Lakini Loti akawajibu, “La hasha, bwana zangu, tafadhalini!
19 Please, listen. You have been pleased with me and have been very kind to me and spared my life. But I cannot flee to the mountain. If I try to do that, I will die in this disaster [PRS].
Mtumishi wenu amepata kibali mbele ya macho yenu, nanyi mmeonyesha wema mkubwa kwangu kwa kuokoa maisha yangu. Lakini siwezi kukimbilia milimani, janga hili litanikumba, nami nitakufa.
20 But listen to me. There is a town nearby. Let me run to that small town. Let me go there now. It is a small town, but our lives will be saved if we go there.”
Tazama, hapa kuna mji karibu wa kukimbilia, nao ni mdogo. Niruhusuni nikimbilie humo, ni mdogo sana, ama sivyo? Ndipo maisha yangu yatasalimika.”
21 One of the angels said to Lot, “I will allow you to do what you have requested [MTY]. I will not destroy the little town you are speaking about.
Akamwambia, “Vema sana, nitalikubali hili ombi pia, sitauangamiza mji ulioutaja.
22 But hurry! Run there, because I cannot destroy anything until you arrive there.” People later called the name of the town Zoar [which means ‘small’, ] because Lot said it was small.
Lakini ukimbilie huko haraka, kwa sababu sitaweza kufanya lolote mpaka ufike huko.” (Ndiyo maana mji huo ukaitwa Soari.)
23 As the sun was rising, Lot and his family arrived in the town which is now called Zoar.
Wakati Loti alipofika Soari, jua lilikuwa limechomoza katika nchi.
24 Then Yahweh caused fire and [burning] sulfur to fall down on Sodom and Gomorrah like rain.
Ndipo Bwana akanyesha moto wa kiberiti uliotoka mbinguni kwa Bwana juu ya Sodoma na Gomora.
25 In that way, he destroyed those cities and all the people who were living in those cities. He also destroyed everything in the valley, including all the plants/vegetation.
Hivyo akaiteketeza miji ile na eneo lote la tambarare, pamoja na wote waliokuwa wanaishi katika miji, hata pia mimea yote katika nchi.
26 But Lot’s wife stopped and looked back [to see what was happening], so she died, and her body [later] became a pillar of salt.
Lakini mke wa Loti akatazama nyuma, hivyo akawa nguzo ya chumvi.
27 That morning, Abraham got up and went to the place where he had stood in front of Yahweh.
Asubuhi na mapema siku iliyofuata, Abrahamu akaamka na kurudi mahali pale aliposimama mbele za Bwana.
28 He looked down toward Sodom and Gomorrah, and he [was surprised to] see that all over the valley, smoke was rising, like the smoke of a huge furnace.
Akatazama upande wa Sodoma na Gomora, kuelekea nchi yote ya tambarare, akaona moshi mzito ukipanda kutoka kwenye nchi, kama moshi utokao kwenye tanuru.
29 So, when God destroyed those cities in the valley, he remembered what he had promised Abraham, and he rescued Lot from the disaster that occurred in the cities where Lot had lived.
Kwa hiyo Mungu alipoiangamiza miji ya tambarare alimkumbuka Abrahamu, akamtoa Loti kutoka kwenye lile janga lililoharibu miji ile ambamo Loti alikuwa ameishi.
30 Lot was afraid to stay in Zoar, so he left there and moved with his two daughters to the mountain, and they lived in a cave.
Loti na binti zake wawili waliondoka Soari na kufanya makao yao kule milimani, kwa maana aliogopa kukaa Soari. Yeye na binti zake wawili waliishi katika pango.
31 One day the older daughter said to (the younger daughter/her sister), “Our father is old, and there is no man in this area who can have sex [EUP] with us, as people all over the earth do.
Siku moja binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee na hakuna mwanaume mahali hapa atakayekutana na sisi kimwili, kama ilivyo desturi ya mahali pote duniani.
32 Let’s make our father drink wine until he gets drunk. Then we can have sex with him [EUP] [without him knowing it]. In that way [he will cause us to become pregnant] and we can bear children.”
Tumnyweshe baba yetu mvinyo kisha tukutane naye kimwili ili tuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
33 So that night they caused their father to become drunk. And the older daughter went in and lay in bed with her father, and he had sex with her, but he was so drunk that he did not know when she lay down with him or when she got up.
Usiku ule walimnywesha baba yao mvinyo, alipolewa binti yake mkubwa akaingia na kukutana naye kimwili. Baba yao hakujua wakati binti yake alipoingia kulala naye wala alipotoka.
34 The next day, his older daughter said to (his younger daughter/her sister), “Listen to me. Last night I slept with our father. Let’s cause him to become drunk again tonight! This time you can go and sleep with him. If he has sex with you, you can become pregnant, and that way you can have a child, too.”
Siku iliyofuata binti mkubwa akamwambia yule mdogo, “Usiku uliopita mimi nilikutana kimwili na baba yangu. Tumnyweshe divai tena, usiku huu nawe ukutane naye kimwili ili tuweze kuhifadhi uzao wetu kupitia baba yetu.”
35 So that night, they caused their father to become drunk with wine again, and then his younger daughter went and slept with him. But again, he was so drunk that he did not know when she lay down with him or when she got up.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo tena usiku ule, naye binti yake mdogo akaingia, akakutana naye kimwili. Kwa mara nyingine baba yao hakujua binti yake alipolala naye wala alipoondoka.
36 So Lot caused his two daughters to become pregnant.
Hivyo binti wawili wa Loti wakapata mimba kwa baba yao.
37 The older one later gave birth to a son, whom she named Moab. He became the ancestor of the Moab people-group.
Binti mkubwa akamzaa mwana, akamwita jina lake Moabu; ndio baba wa Wamoabu hata leo.
38 The younger one also gave birth to a son, whom she named Ben-Ammi. He became the ancestor of the Ammon people-group.
Binti mdogo naye pia akamzaa mwana, naye akamwita Benami; ndiye baba wa Waamoni hata leo.

< Genesis 19 >