< Genesis 10 >

1 (This is/I will now give) a list of the descendants of Noah’s sons, Shem, Ham, and Japheth. They had many children after the flood.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 The sons of Japheth were Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Meshech, and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 The sons of Gomer were Askenaz, Riphath, and Togarmah.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 The sons of Javan were Elishah, Tarshish, Kittim, and Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Those sons and their families who were descended from Javan lived on the islands and on the land close to the [Mediterranean] Sea. Their descendants became tribes, each with its own language and clans and territory.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 The descendants of Ham were Cush, Egypt, Put, and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 The descendants of Cush were Seba, Havilah, Sabtah, Raamah, and Sabteca. The descendants of Raamah were Sheba and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Another one of Cush’s descendants was Nimrod. Nimrod was the first person on earth who became a mighty warrior.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 Yahweh saw that he had become (OR, caused him to become) a great hunter. That is why people say to a great hunter, “Yahweh (sees that you are/has caused you to be) a great hunter like Nimrod.”
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Nimrod became a king who ruled in Babylonia. The first cities over which he ruled were Babel, Erech, Accad, and Calneh.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 From there he went [with others] to Assyria and built the cities of Nineveh, Rehoboth-Ir, Calah,
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 and Resen. Resen was a large city between Nineveh and Calah.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Ham’s son, Egypt, became the ancestor of the Lud, Anam, Lehab and Naphtuh,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 Pathrus, Casluh and Caphtor people-groups. The Philistine people were descended from Casluh.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Ham’s youngest son, Canaan, became the father of Sidon, who was his eldest son, and Heth, his younger son.
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 Canaan was also the ancestor of the Jebus, Amor, Girgash,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Hiv, Ark, Sin,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 Arved, Zemar and Hamath people-groups. Later the descendants of Canaan dispersed over a large area.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 Their land extended from Sidon [city] in the north as far south as Gaza [town], and then to the east as far as Gerar [town], and then farther east to Sodom, Gomorrah, Admah, and Zeboiim [towns], and even as far as Lasha [town].
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Those are the descendants of Ham. They became groups that had their own clans, their own languages, and their own land.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Shem, the older brother of Japheth, became the father of Eber, and the ancestor of all the descendants of Eber.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 The sons of Shem were Elam, Asshur, Arphaxad, Lud, and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 The sons of Aram were Uz, Hul, Gether, and Mash.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Arphaxad became the father of Shelah. Shelah became the father of Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Eber became the father of two sons. One of them was named Peleg, [which means ‘division’], because during the time he lived, people on [MTY] the earth became divided and scattered everywhere. Peleg’s younger brother was Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Joktan became the ancestor of Almodad, Sheleph, Hazarmaveth, Jerah,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Hadoram, Uzal, Diklah,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 Obal, Abimael, Sheba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ophir, Havilah, and Jobab. All those people were descended from Joktan.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 The areas in which they lived extended from Mesha westward to Sephar, which is in the (hill country/area that has a lot of hills).
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 They are descendants of Shem. They became groups that had their own clans, their own languages, and their own land.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 All those groups descended from the sons of Noah. Each group had its own (genealogy/record of people’s ancestors) and each became a separate ethnic group. Those ethnic groups formed after the flood and spread all around the earth.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< Genesis 10 >