< Ezekiel 1 >

1 [I am] Ezekiel, a priest, the son of Buzi. When I was 30 years [old], I [living] among [Israeli] people who had been (exiled from/forced to leave) [and had come to Babylon]. I was living along the Kebar River/ [south of Babylon]. Almost five years after King Jehoiachin had been (exiled/forced to leave Judah), on the fifth day of the fourth [of that year, it was as though] the sky was opened and I saw visions from God. On that day,
Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
2
Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
3 God gave me [in visions here] in Babylonia, and I felt the power [MTY] of Yahweh on me.
neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
4 [In one of the visions, I saw a] windstorm coming from the north. There was a huge cloud, and lightning was flashing continually, and a brilliant light surrounded the cloud. In the center of where the lightning was flashing there was something that resembled glowing bronze.
Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
5 In the center of the storm I saw what resembled four living creatures. They resembled humans,
Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
6 but each of them had four faces and four wings [DOU].
lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
7 Their legs were straight. Their feet resembled the hooves of calves, and the creatures shone like polished bronze.
Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
8 On their four sides under their wings there were hands like humans have.
Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
9 As the four [stood there, they formed a circle/square], with their wings touching each other. They did not turn when they were moving; they went straight ahead.
nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
10 [of the creatures had four faces]. The face that was in front [of each one was a face that] resembled a human face. The face on the right side resembled a lion’s face. The face on the left side resembled an ox’s face. The face in back resembled an eagle’s face.
Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
11 Two of each creature’s wings were lifted up and touched the wings of the creatures that were on each side. The other two wings were folded against the creature’s body.
Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
12 The creatures went straight ahead in whatever direction the [that controlled/guided them] wanted them to go, without changing directions while they were moving.
Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
13 [four] creatures resembled burning coals or torches. A blazing fire moved back and forth among the creatures, and lighting flashed from among them.
Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
14 The creatures moved back and [extremely rapidly], like [SIM] flashes of lightning.
Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
15 While I looked at the four living creatures, I saw a wheel on the ground beside each of them.
Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
16 Each of the wheels was the same, and they all shone like [SIM] (chrysolite/a valuable green stone). Each seemed to have one wheel inside another wheel.
Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
17 Whenever they moved, they would go straight in one of the four directions that they faced; they did not [in another direction] while they moved.
Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
18 The rims of the wheels were covered with eyes.
Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
19 Whenever the living creatures moved, the wheels moved with them. [So] whenever the creatures rose from the ground, the [also] rose up.
Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
20 Wherever the [that controlled the creatures] wanted the creatures to go, they went, and the wheels went with them, because the [that controlled/guided them] was in the wheels [DOU].
Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
21 Whenever the creatures moved, the wheels moved. Whenever the creatures [still], the wheels stopped. Whenever the creatures rose up from the ground, the wheels rose up with them.
Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
22 Above the heads of the creatures there was something that resembled a dome. It shone like ice (OR, crystal) shines, and it was awesome.
Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
23 Under the dome, the creatures stretched out their wings. Each one had two wings; [each wing] stretched towards the creature [was next to] it, and two wings that were against the creature’s body.
Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
24 Whenever the creatures moved, their wings made a sound that resembled the roar made by a rushing stream. It also sounded like the voice of Almighty God, and like [SIM] the noise of a huge army marching. Whenever the creatures stood [on the ground], they lowered their wings.
Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
25 While they [on the ground] with their wings lowered, there was a voice from the dome that was over their heads.
Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
26 Above the dome was something that resembled [huge] [that was made of a huge] (sapphire/valuable blue stone). Sitting on the throne was someone that resembled a human.
Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
27 I saw that above his waist his body resembled metal that was glowing as though it [a very hot] fire inside it. And I saw that below his waist there was a very brilliant light that surrounded him.
Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
28 [shone] like [SIM] a rainbow shines in the clouds on a rainy day. That was the brilliant light that represented the presence of Yahweh. When I saw it, I prostrated myself on the ground, and I heard him speak.
Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

< Ezekiel 1 >