< Ezekiel 40 >
1 Almost 25 years after we had been [to Babylonia], on the tenth day of the first month of that year, almost 14years after Jerusalem had been destroyed, in a vision [I felt] the power [MTY] of Yahweh on me, and he took me to Israel.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya mji kuchukuliwa-katika siku hiyo hiyo, mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu na alinichukua huko.
2 He set me on a very high mountain. On the south side of that mountain there were some buildings that appeared to be [part of] a city.
Katika maono ya Mungu akanileta hata nchi ya Israeli. Akanileta kupumzika juu ya kila mlima mrefu sana; upande wa kusini kulikuwa na monekano kana kwamba majengo ya mji.
3 When he took there, I saw a man whose face was like [SIM] bronze. He was standing in the entrance [of a building]. He had a linen cord and a measuring stick in his hand.
Kisha akanileta huko. Tazama, kulikuwa na mtu! Mwonekano wake ulikuwa kama mwonekano wa shaba. Alikuwa na uzi wa kitani na mwanzi wa kupimia mkononi mwake, na alisimama katika lango la mji.
4 He said to me, “You human, look carefully at everything that I am going to show you, and pay attention to everything that I say and everything that I will show you, because that is why you have been brought here. [And then later] you must tell the Israeli people everything that you have seen [here].”
Huyo mtu akanambia, “Mwanadamu, tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako, na elekeza moyo wako juu ya yote ninayokufunulia, kwa kuwa ulinileta hapa ili niweze kukufunulia haya wewe. Toa taarifa ya kila kitu utakachokiona kwa nyumba ya Israeli.
5 [In the vision I saw that] there was a wall that completely surrounded the temple area. The measuring stick in the man’s hand was (10-1/2 feet/3.3 meters) long. He measured the wall: It was (10-1/2 feet/3.3 meters) thick and (10-1/2 feet/3.3 meters) high.
Kulikuwa ukuta uliokuwa umezunguka eneo la hekalu. Urefu wa kipimo cha mwanzi katika mkono wa mtu ulikuwa dhiraa sita urefu, kila urefu wa dhiraa ulikuwa dhiraa moja na kipimo cha kiganja cha mkono urefu. Aliupima ukuta; ulikuwa kipimo cha mwanzi mmoja na ufito mmoja urefu.
6 Then he went to the entryway on the east [side of the temple]. He climbed the steps and measured the outer threshold/opening for the entryway: It was (10-1/2 feet/3.3 meters) deep.
Kisha akaenda hata kwenye lango la hekalu lililokuwa limeelekea mashariki. Akapanda ngazi na kuipima kizingiti cha lango-mwanzi mmoja upana.
7 Next, there was an entry hallway with [three] (alcoves/very small rooms) along each side [where the guards stood]. Each of the alcoves was (10-1/2 feet/3.3 meters) on each side. There was a dividing wall between each alcove that was (8-3/4 feet/2.7 meters) wide. At the end of the entry hallway was the inner threshold/opening for the entryway, (10-1/2 feet/3.3 meters) deep. It led to the entry room [to the inner courtyard] and faced the temple.
Vyumba vya ulinzi vilikuwa kila mwanzi mmoja urefu na mwanzi mmoja upana; kulikuwa na dhiraa tano katika kila vyumba viwili, na kizingiti cha lango la hekalu karibu na tawa la hekalu kilikuwa mwanzi mmoja urefu.
8 Then he measured the entry room at the end of the entry hallway.
Akapima tawa la lango; ulikuwa mwanzi mmoja urefu.
9 It was about (14 feet/4.2 meters) long, and its supporting columns were (3-1/2 feet/1.1 meters) thick. The entry room of the entryway was at the end of the entry hallway that faced the temple [and extended into the courtyard].
Akapima tawa la lango. Ilikuwa mwanzi mmoja kwenda chini. Mihimili ilikuwa dhiraa mbili upana. Hili lilikuwa tawa la lango kuelekea hekalu.
10 Inside the east entryway there were three alcoves on each side of the entry hallway. They each had the same length and width. And the measurements of the walls that divided the alcoves were all identical.
Kulikuwa na vyumba vitatu vya ulinzi pande zote za lango la mashariki, na yote yalikuwa na kipimo kile kile, na kuta zilizokuwa zimezigawanya zilikuwa na kipimo kile kile.
11 Then he measured the threshold/opening for the entryway: It was (17-1/2 feet/5.3 meters) wide, and the entry hallway [between the alcoves] was (22-3/4 feet/6.9 meters) wide.
Kisha yule mtu akapima upana wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi; na akapima urefu wa njia ya lango la kuingia-dhiraa kumi na tatu.
12 In front of each alcove was a low wall about (21 inches/53 cm.) high, and the alcoves were (10-1/2 feet/3.3 meters) on each side.
Akaupima ukuta uliokuwa mpaka mbele ya vyumba-dhiraa moja urefu. Vyumba vilipimwa dhiraa sita kila upande.
13 Then he measured the width of the roof of the entrance hallway, the distance between the rear wall of one alcove to the rear wall of the opposite alcove, [including the supporting walls along each side]. It was (43-3/4 feet/13.3 meters).
Kisha akapima lango la njia kutoka kwenye paa ya chumba kimoja kuelekea chumba kingine-dhiraa ishirini na tano, kutoka lango la kuingia chumba cha kwanza kuelekea kile cha pili.
14 Then he measured all along the dividing walls between the alcoves all along the inside of the entry hallway: It was (105 feet/31.8 meters). He measured as far as the entry room of the entryway.
Kisha akapima ukuta uliokuwa umeenda kati ya vyumba vya ulinzi-dhiraa sitini urefu; alipima kwa mbali na tawa la lango.
15 The length from [outer] opening of the entryway to the far end of the entry room was (87-1/2 feet/26.5 meters).
Lango la kuingia kutoka lango la mbele kuelekea lango jingine la tawa la mwisho lilikuwa dhiraa hamsini.
16 There were [small] windows in the outside walls of all the alcoves, and also in the inner dividing walls between the alcoves. There were also small windows in the entry room. The dividing walls were decorated with [carvings of] palm trees.
Kulikuwa na madirisha yaliyokuwa yamefungwa kuelekea vyumba na kuelekea nguzo zake kati ya malango kuzunguka kote; na vivyo hivyo kwa mabaraza. Kulikuwa na madirisha pande zote za ndani, na kila mhimili ulikuwa umepambwa kwa mitende.
17 Then [in the vision] he brought me to the outer courtyard. There I saw some rooms, and a stone path/pavement along the walls around the courtyard. There were thirty rooms along the path.
Kisha huyo mtu akanileta hata ua wa nje mwa hekalu. Tazama, kulikuwa na vyumba, na kulikuwa na kibamba katika ua, pamoja na vyumba thelathini baada ya kibamba.
18 The stone path was all around the courtyard, and it extended out from the walls into the courtyard for the same distance as the entry room [of the entryway]. That was the lower path.
Kibamba kilienda juu hata upande wa malango, na upana wake ulikuwa sawsawa na urefu wa malango. Hiki kilikuwa kibamba cha chini.
19 Then the man measured the distance [across the outer courtyard of the temple], between the inner [entrance of] the entryway and [the wall surrounding the] inner courtyard: It was (175 feet/53 meters) [on the east side and on the north side of the courtyard].
Kisha huyo mtu akapima umbali kutoka mebele ya lango la chini hata mbele ya lango la ndani; ilikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki, na sawasawa na upande wa kaskazini.
20 Then he measured how long and how wide was the entryway that was on the north side, the entrance into the outer courtyard [of the temple].
Kisha akapima urefu na upana wa lango lililokuwa upande wa kaskazini mwa ua wa nje.
21 There were three alcoves on each side of the entryway hall. The measurements of the alcoves, the dividing walls between the alcoves, and the entry room were the same as as those in the first entryway. The length from [outer] opening of the entryway to the far end of the entry room was (87-1/2 feet/26.5 meters). The entryway was (43-3/4 feet/13.3 meters) wide.
Kulikuwa na vyumba vitatu pande zote za lango, na lango na matawa yake yalipimwa sawa na lango kubwa-dhiraa hamsini upana wote na dhiraa ishirini na tano upana.
22 Its windows and the entry room and the palm tree [decorations all] measured the same as the ones on the east [side]. There were seven steps up to the outer threshold/opening for the entryway, and an entry room was at the other end of the entryway.
Madirisha yake, tawa, vyumba, na mitende yake vilikabiliana na lango ambalo linaloelekea mashariki. Ngazi saba kuupandia juu hata kwenye tawa lake.
23 There was an entryway to the inner courtyard that faces the north entryway, like there was on the east [side]. The man measured [the distance] from [the north] entryway to the entryway [on the other side]; it was (175 feet/53 meters).
Kulikuwa na lango kwenye ua wa ndani mbele kuelekea mashariki; huyo mtu alipima kutoka lango moja hadi lango jingine-dhiraa mia moja umbali.
24 Then he brought me through the south entryway [into the outer courtyard], and he measured it. It measured the same as the other entryways. Its alcoves, its dividing walls between the alcoves, and its entry room measured the same as the ones on the other sides.
Kisha huyo mtu akanileta hata kwenye lango la kuingia la kusini, na kuta zake na tawa vilipimwa sawa kama malango mengine ya nje.
25 The alcoves and the entry room had [narrow] windows along the walls, like on the other [sides]. The length [of the outer opening of the] entryway [to the far end of the entry room was] was (87-1/2 feet/26.5 meters) and the entryway was (43-3/4 feet/13.3 meters) wide.
Kulikuwa na madirisha yaliyofungwa katika lango la njia na tawa lake kama lile lango. Lango la kusini na tawa lake vilipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
26 There were seven steps up to the outer threshold/opening for the entryway, and an entry room was (opposite it/at the end of the entryway facing the courtyard). It [also] had [carvings of] palm trees on the dividing walls that were between the alcoves.
Kulikuwa na ngazi saba hadi kwenye lango na matawa yake, na kulikuwa na mitende iliyochongoka juu ya kuta pande zote.
27 The inner courtyard also had an entryway on the south [side]. He measured from that entryway to the entrance on the south [side of the outer courtyard; it was also] (175 feet/53 meters).
Kulikuwa na lango la ua wa ndani upande wa kusini, na yule mtu akapima kutoka hilo lango hata lango la kuingia upande wa kusini-dhiraa mia moja umbali.
28 Then [in the vision] he brought me through the south entryway into the inner courtyard, and he measured the south entryway. It measured the same as the other [entryways].
Kishi huyo mtu akanileta hata ua wa ndani karibu na lango lake la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo vile vile kama malango mengine.
29 Its alcoves [along the entry hallway], its dividing walls [between the alcoves], and its entry room measured the same as [the ones on] the other [sides]. The alcoves and the entry room had windows. The length [of the outer opening of the] entryway [to the far end of the entry room was] was (87-1/2 feet/26.5 meters) and the entryway was (43-3/4 feet/13.3 meters) wide.
Vyumba vyake, kuta, na matao vilipimwa sawa kama malango mengine; kulikuwa na madirisha kuzunguka matao yote. Lango la ndani na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
30 The entry rooms around [the inner courtyard] were (43-3/4 feet/13.3 meters) wide and (8.7 feet/2.6 meters) long.
Pia kulikuwa na matao pande zote za kuta za ndani; haya yalikuwa dhiraa ishirini na tano urefu na dhiraa tano upana.
31 The entry room faced the outer courtyard. There were [carvings of] palm trees that decorated the columns, and there were eight steps [up] to the entryway.
Hili tawa lilielekea ua wa nje pamoja na mitende iliyochongwa juu ya kuta zake na ngazi nane kuupandia.
32 Then he led me to the east side of the inner courtyard, and he measured the entrance. It had the same measurements as the other [entrances]
Kisha yule mtu akanileta hata kwenye ua wa ndani karibu na njia ya kaskazini na kulipima lango, ambalo lilikuwa na vipimo sawa kama malango mengine.
33 Its alcoves and dividing walls and entry room measured the same as the others.
Vyumba vyake, kuta, na matawa yalikuwa na kipima sawa kama cha malango, na kulikuwa na madirisha pande zote. Laango la ndani na matawa yake yalikuwa dhiraa hamsini urefu na dhiraa ishirini na tano upana.
34 Its entry room faced the outer courtyard. It also had carvings of palm trees that decorated the walls, and it had eight steps up to it.
Matawa yake yalielekea nje ya ua; ilikuwa na mitende pande zote za hiyo na ngazi nane za kuupandia.
35 Then he led me to the entrance on the north side and measured it. It measured the same as the other entrances.
Kisha huyo mtu akanileta hata lango la kaskazini na kulipima; likapimwa vivyo hivyo kama malango mengine.
36 And its alcoves and walls between them and the entry room all had [small] windows in the walls. It was (87-1/2 feet/26.5 meters) long and (43.7 feet/13.3 meters) wide.
Vyumba vyake, kuta, na ukumbi vilipimwa sawa na malango mengine, na kulikuwa na madirisha pande zote. Njia ya lango na matao yake yalipimwa dhiraa hamsini urefu na upana dhiraa ishirini na tano.
37 Its entry room faced the outer courtyard. There were [carvings of] palm trees that decorated its walls, and there were eight steps [up] to the entryway.
Tatawa lake lilielekea ua wa nje; ilikuwa na mitende pande zote za huo na ngazi nane kuupandia.
38 [In the vision, I saw that] in the inner entry room of the north entryway there was a door to a side room. That side room was where the [carcasses of the] animals that would be burned completely [on the altar] were washed.
Kulikuwa na chumba pamoja na mlango karibu na kila lango la ndani. Hapa ndipo ambako walipooshea sadaka za kutekezwa.
39 In the entry room, there were two tables on each side [of the room]. On those tables would be slaughtered the animals that would be completely burned, and the animals for offerings for sins that people had committed, and offerings to cause people to longer be guilty for having sinned.
Kulikuwa na meza mbili kila upande wa kila ukumbi, ambako sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa, na pia sadaka ya dhambi na sadaka ya hatia.
40 Along the outside wall of the entry room, on each side of the steps at the opening to the entryway on the north side, were two tables.
Karibu na ukuta wa ua, kuelekea juu kwenye lango kuelekea kaskazini, kulikuwa na meza mbili. Pia kwa upande mwingine kulikuwa na meza mbili kwenye lango la ukumbi.
41 [So] there were four tables outside the entrance and four tables inside the entry room, on which the [animals to be] sacrificed were slaughtered.
Kulikuwa na meza nne pande zote karibu na lango; wakachinja wanyama juu ya meza nane.
42 There were also four tables of cut stone for the offerings to be completely burned, (31-1/2 in./80 cm.) on each side and (21 in./53 cm.) high. On those stone tables would be placed the tools for slaughtering all the animals for the sacrifices.
Kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, dhiraa moja na nusu urefu, dhiraa moja na nusu upana, na kimo dhiraa moja. Juu yake waliweka vyombo pamoja ambavyo walivichinjia sadaka za kuteketezwa kwa ajili ya sadaka.
43 The meat for the offerings would be placed on [stone] tables. There were hooks [on which the meat was hung], each with two prongs, each (3 in./8 cm.) long, fastened to the walls [of the entry room].
Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote, na nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza.
44 Outside the inner entryway, inside the inner courtyard, were two rooms, one on the north side and one on the south side.
Karibu na lango la ndani, katika ua wa ndani, kulikuwa na vyumba vya waimbaji. Moja ya hivi vyumba kilikuwa upande wa kaskazini, na kingine kusini.
45 The man said to me, “The room whose door faces south is for the priests who are in charge of the work in the temple.
Kisha yule mtu akanambia, “Hiki chumba kinachoelekea kusini ni kwa ajili ya makuhani walio zamu katika hekalu.
46 The room whose door faces north is for the priests who are in charge of [the work at] the altar. They are the descendants of Zadok; they are the only descendants of Levi who are permitted to approach Yahweh while they work for him.”
Chumba kilichoelekea kaskazini kilikuwa kwa ajili ya makuhani waliokuwa zamu kwenye madhabahu. Hawa ni wana wa Sadoki ambaye huja humkaribia Yahwe kumtumikia; ambao ni miongoni mwa wana wa Lawi.”
47 Then he measured the courtyard: It was square, (175 feet/53 meters) long and (175 feet/53 meters) wide. The altar was in front of the temple.
Kisha akaupima ule ua-dhiraa mia moja urefu na dhiraa mia moja upana mraba, pamoja na madhabahu mbele ya nyumba.
48 Then [in the vision] he brought me to the entry room of the temple, and measured the walls on each side of the entrance: They were (8-3/4 feet/2.6 meters) thick. The entrance was (24-1/2 feet/7.4 meters) wide, and the walls on each side of the entrance were (5-1/4 feet/1.6 meters) long.
Kisha yule mtu akanileta hata kwenye varanda ya nyumba na kupima mwimo wa milango yake-ilikuwa dhiraa tano unene upande huu. Njia ya kuingilia yenyewe ilikuwa dhiraa kumi na nne, na kuta pande zote za huo zilikuwa dhraa tatu upana.
49 The entry room was (35 feet/10.6 meters) wide on each side. There were ten steps up to it, and there were pillars on each side of the entrance.
Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake ulikuwa dhiraa kumi na moja. Kulikuwa na ngazi zilizokuwa zimepanda juu na nguzo zilizokuwa zimesimama pande zote za huo.