< Ezekiel 39 >

1 [Yahweh said to me], “You human, prophesy about [more terrible things that will happen] to Gog, and say this [to him]: ‘Gog, I am opposed to you who rule Meshech and Tubal.
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
2 I will turn you around and drag you [and your armies] from far north [of Israel] and send you to [fight on] the mountains in Israel.
Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
3 When you are there, I will snatch your bows from your left hands and cause your arrows to fall from your right hands.
Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
4 You and all the soldiers that are with you will die on the mountains in Israel. I will give your [corpses] to be food for the birds that eat [dead] flesh, and to the wild animals.
Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
5 You will die in the open fields. [That will surely happen because] I, Yahweh the Lord, [have said that it will happen].
Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
6 I will cause [many] fires to burn in Magog and among [all] those who live safely in the areas along their coasts, and they will know that it is I, Yahweh, [who have the power to do what I say that I will do].
Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 I will enable my Israeli people to know that I am holy. I will no longer allow people to damage my reputation, and [people in other] nations will know that I, Yahweh the Lord, am the Holy One in Israel.
“‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 [I], Yahweh the Lord, declare that it will soon be the day that those things will happen. It will be the day that I have spoken [to you] about.
Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
9 At that time, those Israelis who live in the towns will go out and gather the weapons [from your dead soldiers], and use them to make fires [to cook their food]. They will burn the small and large shields, the bows and arrows, the war clubs, and spears. There will be enough weapons to use as firewood for seven years.
“‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
10 They will not need to gather firewood in the fields or cut wood from trees in the forests, because those weapons will be all the firewood [that they will need]. And they will take valuable things from those who took valuable things from them, and steal things from people who stole things from them. [That is what I], Yahweh the Lord, declare [will happen].
Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
11 At that time I will create a graveyard for you, Gog, [and your soldiers], in the valley east of the [Dead] Sea. That graveyard will block the road that travelers [usually walk on], because you, Gog and all [the soldiers] of your huge army will be buried there. [So] it will be named ‘the Valley of Gog’s Huge Army’.
“‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
12 For seven months the people of Israel will be burying those corpses. [It will be necessary to bury all of them], in order that the land will not be (defiled/considered unacceptable to me) [because of any unburied corpses].
“‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
13 All the people of Israel will [do the work of] burying them. The day when I [win that victory] they will honor me.
Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
14 After those seven months are ended, the Israeli people will appoint men to go throughout the land to bury corpses, in order that the land will not remain defiled.
“‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
15 When they go through the land, when one of them sees a human bone, he will set up a marker beside it. [When] the gravediggers [see the markers, they will pick up the bones] and bury them in the Valley of Gog’s Huge Army.
Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
16 There will be a city there named Hamonah, [which means ‘huge army’]. And by doing this [work of burying the corpses], they will (cleanse the land/cause the land to be acceptable to me again).’”
(Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
17 [Yahweh said to me], “You human, this is what [I], Yahweh the Lord, say: Summon every kind of bird and wild animal. Say to them, ‘Gather together from everywhere and come to the feast that Yahweh is preparing for you. [It will be] a great feast on the mountains in Israel. [There] you will eat [men’s] flesh and drink their blood.
“Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
18 You will eat the flesh of strong soldiers and drink the blood of kings [as if they were] fat animals—rams and lambs, goats and bulls—from the Bashan [region].
Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
19 At that feast that Yahweh is preparing for you, you will eat fat until your [stomachs] are full, and you will drink blood until [it is as though] you are drunk.
Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
20 [It will be as though] you are eating at a table that I [have set up for you. You will eat all you want of the flesh] of horses and their riders, strong soldiers [DOU] of every kind.’ [That is what I], Yahweh the Lord, declare.
Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
21 I will show [people of] many nations that I am glorious, and all those nations will see how I punish them [DOU].
“Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
22 After that time, the Israeli people will know that I, Yahweh their God, [have the power to do what I say that I will do].
Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
23 And the [people of other] nations will know that the Israeli people had been forced to go to other countries because they sinned by not being faithful to me. I (turned away from/abandoned) them, and allowed their enemies to capture them [IDM], and many [HYP] of them were killed by [their enemies’] swords.
Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
24 I punished them like they deserved to be punished because of their disgusting behavior and sins, and I turned away from them [MTY].
Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
25 Therefore, this is [now] what I, Yahweh the Lord, say: I will now bring back from exile/Babylonia [the descendants of] Jacob; I will pity all the Israeli people, and I will [also] jealously protect my reputation.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
26 When the Israeli people [are back in their own country, they will] live safely in their land, with no one to cause them to be afraid, but they will be ashamed when they think about the disgraceful and unfaithful things that they did [previously].
Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
27 When I have brought them back from their enemies’ countries and gathered them together [in Israel], the people of many nations will know that I am holy.
Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
28 And the Israeli people will know that I, Yahweh their Lord, [have the power to do what I say that I will do]. They will know that because [even though] I forced them to go to [other] countries, I will gather them together in their own country. I will not leave any of them in those countries.
Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
29 I will no longer turn away from them; I will pour out my Spirit on the Israeli people. [That will surely happen because I], Yahweh, have said it.”
Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 39 >