< Exodus 8 >

1 Then Yahweh said to Moses/me, “Go back to the king and tell him, ‘Yahweh says that you must let my people go, in order that they can worship me [in the desert].
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
2 But if you refuse to let them go, I will punish you by sending frogs to cover your country.
Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura.
3 [Not only] will the Nile [River] be full of frogs, [but] the frogs will come up [out of the river] into your palace. They will come into your bedroom and onto your bed. They will be in the houses of your officials and all [the rest of] your people. They will even get into your ovens and your pans for mixing the materials for baking bread.
Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga.
4 The frogs will jump up on you and your officials and [all the rest of] your people.’”
Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’”
5 Yahweh [also] said to Moses/me, “Say this to Aaron: ‘Hold your stick in your hand and stretch it out [as though you were stretching it] over the river, the canals, and over the pools, and cause frogs to come up [from all this water and] cover the land of Egypt.’”
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’”
6 [After Moses/I told that to] Aaron, he stretched out his hand [as though he were stretching it] over all the water in Egypt. And the frogs came up [from the water and] covered Egypt.
Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi.
7 But the men who performed magic did the same thing, and they caused [more] frogs to come up [from the water onto the land].
Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.
8 Then the king summoned Moses/me and said, “Ask Yahweh to take away these frogs from me and my people. After that happens, I will allow your people to go, in order that they can offer sacrifices to Yahweh.”
Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
9 Moses/I said to the king, “I will be glad to pray for you and for your officials and for [the rest of] your people. [I will ask Yahweh] to get rid of the frogs from all your houses. The only frogs left will be [those] in the Nile [River]. Just tell me when I should pray.”
Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”
10 He replied, “Tomorrow.” So Moses/I said, “[I will do] what you say, and then you will know that Yahweh God, the one we [worship, is the only true god], and that there is no other god like him.
Farao akasema, “Kesho.” Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu.
11 The frogs will leave you and your officials and all [the rest of] your people. The only ones left will be in the Nile [River].”
Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”
12 Aaron and Moses/I left the king. Then Moses/I prayed to Yahweh, [asking him to take away] all the frogs he had [brought to the king’s land].
Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao.
13 And Yahweh did just what Moses/I [asked him to do]. As a result, all the frogs in the houses, in their courtyards, and in the fields died.
Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani.
14 The people gathered together all the dead frogs into big piles, and the land stank [from the smell].
Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka.
15 But when the king saw that [the problem] was ended, he became stubborn [IDM] [again]. And just as Yahweh had predicted, he would not pay attention to what Aaron and Moses/we told him.
Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
16 Then Yahweh said to Moses/me, “Tell Aaron to strike the ground with his stick. [When he does that], all the fine particles of ground/dust will become gnats, all over the land of Egypt.”
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.”
17 So they/we did that. Aaron struck the ground with his stick, and all over Egypt, the fine particles of ground/dirt became gnats. The gnats covered the people and all [their] animals.
Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto.
18 The men who worked magic tried to cause gnats to appear, but they were unable to do it. So the gnats [stayed] on the Egyptian people and on their animals.
Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.
19 The men who worked magic said to the king, “It is God who has done this with his power [MTY]!” But the king continued to be stubborn [IDM], and he would not pay attention to us, just as Yahweh had predicted.
Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.
20 Then Yahweh said to Moses/me, “Get up early [tomorrow] morning. [Go down] to the river and wait for the king. [When he comes to bathe] [MTY], say to him, ‘This is what Yahweh says to you: “Let my people go, in order that they may worship me [in the desert].
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu.
21 [I warn you that] if you do not let my people go, I will send swarms of flies to you. They will come down on you and on your officials and on [the rest of] your people. The houses of all you Egyptians will be full of flies. They will [even] cover the ground.
Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.
22 But when that happens, I will treat the Goshen region, where my people live, differently. There will be no swarms of flies there. In that way, you will know that I, Yahweh, am doing these things [here] in this land.
“‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii.
23 I will distinguish clearly between [how I act toward] my people and [how I act toward] your people. And this plague is going to happen tomorrow!”’”
Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’”
24 [Early the next morning, Moses/I told that to the king, but the king would not pay any attention]. So Yahweh did what he said he would do. He sent great swarms of flies into the palace of the king and into the houses of his officials. The whole country of Egypt was ruined by the flies.
Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.
25 Then the king summoned Aaron and Moses/me and said, “You Israeli people can go and offer sacrifices to your god, [but you must do it] here in [this] land.”
Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”
26 But Moses/I replied, “It would not be right [for us] to do that, because we will be offering sacrifices that are very offensive to the Egyptian people. If we offer sacrifices that the Egyptian people think are disgusting, they will kill us by throwing stones at us [RHQ]!
Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe?
27 No, we need to travel for three days into the desert. There we will offer sacrifices to Yahweh, the God we worship, just as he commands (OR, has commanded) us.”
Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”
28 So the king said, “I will let your people go to offer sacrifices to Yahweh, your god, in the desert. But you must not go very far. [Now] pray for me!”
Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”
29 Moses/I said, “Listen [to me]! After I leave you, I will pray to Yahweh, [asking] that tomorrow [he will cause] the swarms of flies to leave you and your officials and [the rest of] your people. But do not deceive us again by refusing to let our people go to offer sacrifices to Yahweh!”
Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”
30 Then Moses/I left the king and prayed to Yahweh.
Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana,
31 And Yahweh did what Moses/I asked, and he got rid of the swarms of flies from [around] the king and his officials and [the rest of] his people. No flies remained.
naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia.
32 But the king was stubborn [IDM] this time also, and he did not allow the Israeli people to go.
Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.

< Exodus 8 >