< Exodus 36 >

1 “Bezalel and Oholiab, and all the other men to whom Yahweh has given ability and enabled them to understand how to do all the work to make the Sacred Tent, must make everything just as Yahweh has commanded.”
Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
2 So Moses/I summoned Bezalel and Oholiab and all the other skilled men to whom Yahweh had given special ability and who wanted to do some of the work.
Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
3 Moses/I gave them all the things that the people had brought as offerings to Yahweh for making the Sacred Tent. But the people continued bringing more things every morning.
Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
4 As a result, the skilled men who were doing various things to make the Sacred Tent came to Moses/me
Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
5 and said, “The people are bringing more than we need to do the work that Yahweh has commanded us!”
wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
6 So Moses/I gave the skilled men this message that was proclaimed throughout the camp: “No one should bring anything more as an offering to make the Sacred Tent!” When the people [heard that], they did not bring anything more.
Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
7 What they had already brought was enough to do all the work. [In fact], it was more than was needed!
kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
8 All the most skilled men among the workmen made the Sacred Tent. They made it from ten strips of fine linen, and carefully embroidered it using blue, purple, and red yarn/thread to make figures that resembled the winged creatures.
Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
9 Each strip was (14 yards/twelve meters) long and (2 yards/1.8 meters) wide.
Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
10 They sewed five strips together to make one set, and they sewed the other five strips together to make the other set.
Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
11 For each set, they made loops of blue [cloth] and fastened them on the outer edge of the strip, at the end of each set.
Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
12 They put 50 loops on the edge of the first set, and 50 loops on the edge of the second set.
Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
13 They made 50 gold clasps/fasteners, to fasten both of the sets together. In that way, the inside of the Sacred Tent was [as though it was] one piece.
Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
14 They made a cover for the Sacred Tent from eleven pieces of cloth made from goats’ hair.
Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
15 Each piece of cloth was (15 yards/13.5 meters) long and (2 yards/1.8 meters) wide.
Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
16 They sewed five of these pieces of cloth together to make one set, and they sewed the other six pieces of cloth together to make another set.
Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
17 They made 100 loops [of blue cloth]. They fastened 50 of them to the outer edge of the one set and they fastened 50 to the outer edge of the other set.
Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
18 They made 50 bronze clasps/fasteners and joined the two sets together with them. In that way it formed one cover.
Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
19 They made two more covers for the Sacred Tent. They made one from rams’ skins that had been (tanned/dyed red), and they made the top cover from goatskin leather.
Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
20 They made frames from acacia wood and set them up [to support the covers for the Sacred Tent].
Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
21 Each frame was (15 feet/4.5 meters) long and (27 in./66 cm.) wide.
Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
22 They made two projections at the bottom of each frame. These were for fastening the frames to the bases underneath them. Each frame had these projections.
zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
23 The skilled workmen made twenty frames for the south side of the Sacred Tent.
Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
24 They made 40 silver bases to go underneath them. Two bases went under each frame. The projections on each frame fit into these bases.
na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
25 [Similarly], they made 20 frames for the north side of the Sacred Tent.
Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
26 They made 40 silver bases for them also, with two bases for under each frame.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
27 For the rear of the Sacred Tent, on the west side, they made six frames.
Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
28 They also made two extra frames, one for each corner of the rear of the Sacred Tent, [to provide extra support].
na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
29 The two corner frames were joined from the bottom to the top (OR, joined at both the bottom and the top). At the top of each of the two corner frames they fastened a gold ring for holding the crossbar.
Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
30 In that way, [for the rear of the Sacred Tent] there were eight frames, and there were 16 bases, two bases under each frame.
Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
31 The workmen made 15 crossbars from acacia wood.
Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
32 Five of them were for the frames on the north side of the Sacred Tent, five for the south side, and five for the frames at the rear of the Sacred Tent, the west side.
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
33 The crossbars on the north, south, and west sides of the Sacred Tent were fastened to the middle of the frames. The two long crossbars extended from one end of the Sacred Tent to the other, and the crossbar on the west side extended from one side of the Sacred Tent to the other side.
Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
34 The workmen covered the frames with gold and fastened gold rings to the poles. The crossbars [were put] into the rings. The crossbars were [also] covered with gold.
Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
35 They made a curtain from fine white linen. Skilled craftsmen embroidered it with blue, purple, and red yarn/thread, making designs [that resembled] the winged creatures.
Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
36 They suspended/hung the curtain from four posts that were made from acacia [wood] and covered with gold. They set [each] post in a silver base.
Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
37 They made a curtain to [cover] the entrance of the Sacred Tent. They made it from fine linen, and a skilled weaver embroidered it with blue, purple, and red yarn/thread.
Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
38 [To support this curtain], they also made five posts from acacia wood and fastened gold clasps/fasteners to them. They completely covered the posts with gold. They also made a bronze base for each of those posts.
Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.

< Exodus 36 >