< Exodus 34 >

1 Yahweh said to Moses/me, “Cut two slabs of stone that will be like the first slabs, the ones that you broke. Then I will engrave on them the words that were on the first slabs.
Bwana akamwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
2 Get ready tomorrow morning, and come up to the top of Sinai Mountain again to talk with me there.
Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
3 Do not allow anyone to come up with you. I do not want anyone [else] to be anywhere on the mountain. Do not allow any sheep or cattle to graze (at the base of/near) the mountain.”
Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane mtu popote juu ya mlima, wala kondoo na mbuzi au ngʼombe wasilishe karibu mbele ya huo mlima.”
4 So Moses/I cut two slabs of stone that were like the first ones. He/I arose early the next morning. He/I took the slabs and carried them in his/my hands up to the top of Sinai Mountain, as Yahweh had commanded.
Kwa hiyo Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Bwana alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
5 Then Yahweh descended in the [tall] cloud and stood with Moses/me there. He proclaimed that it was he, Yahweh, [who was going to speak to Moses/me].
Kisha Bwana akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Bwana.
6 Then Yahweh passed in front of him/me and proclaimed, “I am Yahweh God. I always act mercifully and kindly [toward people]. I do not get angry quickly. I [truly] love [people] and I do what I promise to do for them, without changing.
Bwana akapita mbele ya Mose, akitangaza, “Bwana, Bwana, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
7 I love people for thousands of generations. I forgive people for all kinds of sins [TRI]. But I will certainly punish [LIT] those who are guilty. I will punish not only them, but I will punish (their descendants, down to the third and fourth generation/their children and grandchildren and great-grandchildren).”
akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
8 Moses/I quickly prostrated himself/myself on the ground and worshiped [Yahweh].
Mara Mose akasujudu na kuabudu.
9 He/I said, “Yahweh, if you are now pleased with me, I ask that you go with us. These people are very stubborn [IDM], but forgive us for all our sins [DOU], and accept us to be people who belong to you [forever].”
Mose akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
10 Yahweh replied, “Note this: I am going to make a solemn agreement [with the Israeli people]. As they are watching, I will perform great miracles. They will be miracles that no one has ever done on the earth in any nation. All the people who are near you will see the great things that I, Yahweh, will do. I will do awesome things for you [all].
Kisha Bwana akasema: “Tazama ninafanya Agano mbele ya watu wako wote. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza ile kazi nitakayowafanyia mimi Bwana wenu.
11 [Each Israeli] person must obey what I am commanding you this day. Do not forget that [if you obey me], I will expel the Amor, Canaan, Heth, Periz, Hiv, and Jebus people-groups [from the land]. But be careful that you do not make any [peace] agreements with any of the people who live in the land into which you are going, because if you do that, [you will begin to do the evil things that they do]. It will be [like] falling into a trap.
Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
13 You must tear down their altars, destroy their sacred pillars, and cut down [the poles that they use to worship their female goddess] Asherah.
Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia na ukatekate nguzo zao za Ashera.
14 You must worship only me, [and] not worship any other god, because I, Yahweh, cannot endure any rivals.
Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
15 Do not make peace agreements with [any group] that lives in that land. When they worship their gods and offer sacrifices to their gods, and they invite you to join them, do not join them. If [you join them], you will eat the food that they sacrifice to their gods, and [you will not be faithful to me. You will be like people who] commit adultery, [who are not being faithful to their spouses] [MET].
“Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe nawe utakula sadaka za matambiko yao.
16 If you take some of their women to be wives for your sons, and these women worship their own gods, they will persuade your sons also to worship their gods.
Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
17 Do not pour melted metal into molds to make statues for you to worship.
“Usijifanyie sanamu za kusubu.
18 [Each year], during the month [of/named] Abib, celebrate the Festival of Eating Bread Made Without Yeast. [During that festival], for seven days you must not eat bread made with yeast, as I commanded you, because it was in that month that you left Egypt.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
19 Your firstborn sons and the firstborn [male] animals of your cattle and sheep [and goats] belong to me.
“Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ngʼombe au wa kondoo au mbuzi.
20 The firstborn of your [male] donkeys [also belong to me]. But you may buy them back by [offering to me] lambs [in their place]. If you do not do that, you must [kill these animals by] breaking their necks. You must also buy back your firstborn sons. You must bring an offering to me [LIT] each time you come to [worship] me.
Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
21 [Each week] you may work for six days, but on the seventh day you must rest. [Even] during the times when you plow [the ground] and harvest [your crops], you must rest [on the seventh day].
“Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
22 [Each year] celebrate the Harvest Festival, when you begin to harvest the first crop of wheat, and also celebrate the Festival of Living in Temporary Shelters, when you finish harvesting [the grain and fruit].
“Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
23 Three times each year all the men must come to worship me, Yahweh, the God of the Israeli people.
Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
24 I will expel the people-groups that live in the land [where you will be], and I will cause your territory to become very large. As a result, no group will try to conquer your country if you come to worship me each year during those three festivals.
Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapokwenda mara tatu kila mwaka kuonana na Bwana Mungu wako.
25 When you sacrifice an animal [MTY] to me, do not offer with it bread that is made with yeast. And during the Passover Festival, when you sacrifice lambs, do not keep any of the meat until the next morning.
“Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka mpaka asubuhi.
26 I am Yahweh God. You must bring to my Sacred Tent the first part of the grain that you harvest each year. When you kill a young animal/kid [either a lamb or a calf], do not [prepare to eat it by] boiling it in its mother’s milk.”
“Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
27 Yahweh also said to Moses/me, “Write down the words that I have told you. By giving you these commands, I have made a solemn agreement with you and with the [other] Israeli people.”
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.”
28 Moses/I was there [on the top of the mountain] with Yahweh for 40 days and nights. During that time he/I did not eat or drink anything [SYN]. He/I engraved on the stone slabs the words of the Ten Commandments, [which were part of Yahweh’s] solemn agreement.
Mose alikuwa huko pamoja na Bwana kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi.
29 When Moses/I came back down the mountain, carrying in his/my hand the two stone slabs on which were written the Ten Commandments, his/my face was shining because he/I had been talking with Yahweh, but he/I did not know that his/my face was shining.
Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Bwana.
30 When Aaron and the [other] Israeli people saw Moses/me, they were amazed/surprised that his/my face was shining. So they were afraid to come near him/me.
Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia.
31 But Moses/I called to them. Then Aaron and the other Israeli leaders came to him/me, and he/I talked with them.
Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
32 Afterwards, all the other Israeli people came near, and he/I told them all the laws that Yahweh had given to him/me on Sinai Mountain.
Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Bwana alizompa katika Mlima wa Sinai.
33 When Moses/I finished talking to the people, he/I put a veil over his/my face.
Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
34 But whenever Moses/I entered the Sacred Tent to talk with Yahweh, he/I removed the veil. When he/I came back out, he/I would always tell to the Israeli people everything that Yahweh had commanded him/me [to tell them].
Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za Bwana kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
35 The Israeli people would see that Moses’/my face was [still] shining. Then he/I would put the veil back on his/my face again until the next time that he/I went into [the Sacred Tent] to talk with Yahweh.
waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na Bwana.

< Exodus 34 >