< Exodus 29 >

1 “This is what you must do to dedicate Aaron and his sons to serve me [by being] priests: Select one young bull and two rams that do not have any defects.
“Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
2 Bake three [kinds of bread] using finely-ground wheat flour, but without yeast: Bake some loaves that do not have any olive oil in them, bake some loaves that have olive oil in the dough, and bake some thin wafers that will be smeared with olive oil [after they are baked].
Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
3 Put them in a basket and offer them [to me] when you sacrifice the young bull and the two rams.
Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
4 Take Aaron and his sons to the entrance of the Sacred Tent, and wash them [ritually].
Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
5 Then put the special clothes on Aaron—the long-sleeved tunic/gown, the robe that will be worn underneath the sacred apron, the sacred apron, the sacred pouch, and the sash/waistband.
Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
6 Place the turban on his head, and fasten to the turban the ornament that has the words ‘Dedicated to Yahweh’ engraved on it.
Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
7 Then take the oil and pour some on his head to (dedicate him/set him apart).
Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
8 Then bring his sons and put the long-sleeved tunics/gowns on them.
Walete wanawe na uwavike makoti,
9 Put the sashes/waistbands around their waists and the caps on their heads. That is the ritual by which you are to (dedicate them/set them apart) to be priests. Aaron and his male descendants must serve me [by being] priests forever.
pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
10 “Then bring the young bull to the entrance of the Sacred Tent. Tell Aaron and his sons to put their hands on the head of the young bull.
“Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
11 Then, while they do that, kill the young bull [by slitting its throat], and catch/drain the blood in a bowl.
Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
12 Take some of that blood with your finger and smear it on the projections of the altar. Throw/Splash the rest of the blood against the base of the altar.
Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
13 Take all the fat that covers the inner organs of the young bull, the best part of the liver, and the two kidneys with the fat on them, and burn all these on the altar [as an offering to me].
Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
14 But the meat of the young bull and its hide and intestines must be burned outside the camp. That will be an offering to forgive the guilt of your sins.
Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
15 “Then select one of the rams, and tell Aaron and his sons to put their hands on the head of the ram.
“Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
16 Then kill the ram [by slitting its throat]. Catch/Drain some of the blood and splash it against all four sides of the altar.
Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
17 Then cut the ram into pieces. Wash its inner organs and its rear legs and put those with the head
Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
18 and burn those pieces [completely] on the altar with the rest of the ram. That will be an offering to me, Yahweh, and the smell will please me.
Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
19 “Take the other ram [that was selected for these rituals], and tell Aaron and his sons to put their hands on the ram’s head.
“Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
20 Then kill the ram by slitting its throat, and drain the blood [into a bowl]. Smear some of the blood on the lobe of the right ears of Aaron and his sons, and on the thumbs of their right hands, and on the big toes of their right feet. Throw/Splash the rest of the blood against the four sides of the altar.
Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
21 Wipe up some of the blood that is on the altar, mix it with some of the oil for anointing, and sprinkle it on Aaron and his clothes, and on his sons and their clothes. By doing that, you will dedicate them and their clothes [to me].
Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
22 “Also, cut off the ram’s fat and its fat tail and the fat that covers the inner organs, the best part of the liver, the two kidneys with the fat on them, and the right thigh.
“Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
23 Take also one of each of the kinds of bread [that was baked]—one made with no oil, one with oil, and one thin wafer.
Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
24 Put all these things in the hands of Aaron and his sons. [Then tell them to] lift them up [high] to dedicate them to me.
Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 Then take them from their hands and burn them on the altar, on top of the other things [that were placed there]. That [also] will be an offering to me, and its smell will please me.
Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
26 Then take the meat of the ribs of the second ram that was killed, and lift it up [high] as an offering to me. But then this part of the animal will be for you [to eat].
Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
27 Then take the meat of the ribs, the other thigh of the first ram that was sacrificed to (dedicate/set apart) the priests, and the ram whose other parts were lifted high to show that they were an offering to me; and set the meat of the ribs and thigh apart for Aaron and his sons, for them to eat.
“Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
28 In the future, whenever the Israeli people present to me, Yahweh, offerings to maintain fellowship with me, the ribs and the thigh [of animals that they sacrifice] will be for Aaron and his male descendants [to eat].
Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
29 “After Aaron [dies], the special clothes that he wore will belong to his sons. They are to wear those clothes when they are (set apart/dedicated) [to become priests].
“Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
30 Aaron’s son who becomes The Supreme Priest and enters the Sacred Tent and performs rituals in the Holy Place must [stay in the Sacred Tent], wearing these special clothes, for seven days.
Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
31 “Take the meat of the other ram that was sacrificed to (set apart/dedicate) Aaron and his sons, and boil it in the courtyard.
“Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
32 After it is cooked, Aaron and his sons must eat it, along with the bread that is left in the basket, at the entrance of the Sacred Tent.
Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
33 They must eat the meat of the ram that was sacrificed to forgive them for [their sins] when they were dedicated to do this work. They are the only ones who are permitted to eat this meat. [Those who are not priests are not allowed to eat it], because it is dedicated to me.
Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
34 If any of this meat or some of the bread is not eaten that night, no one is permitted to eat any of it the next day. It must be completely burned, because it is sacred/dedicated to me.
Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
35 “Those are the rituals that you(sg) must perform during those seven days when you dedicate Aaron and his sons for this work. You must do everything that I have commanded you.
“Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
36 Each of those seven days you must also sacrifice a young bull as an offering to me, in order that I may forgive sins. Also, you must make another offering (to make the altar pure in my sight/in order that I will consider the altar to be pure). You must also anoint the altar with olive oil, to (set it apart/dedicate it).
Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
37 Perform these rituals every day for seven days, to (set apart/dedicate) the altar and make it pure. If you do not do that, anyone or anything that touches the altar will become taboo.
Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
38 “You must also sacrifice lambs and burn them on the altar. Each of those [seven] days you must sacrifice two lambs.
“Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
39 One lamb must be sacrificed in the morning, and one must be sacrificed in the evening.
Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
40 With the first lamb, also offer (2 pounds/1 kilogram) of finely-ground wheat flour mixed with one quart/liter of the best kind of olive oil, and one quart/liter of wine as an offering.
Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
41 In the evening, when you sacrifice the other lamb, offer the same amounts of flour, olive oil, and wine as you did in the morning. This will be an offering to me, Yahweh, that will be burned, and its smell will please me.
Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
42 You [and your descendants] must continue making these offerings to me, Yahweh, throughout all future generations. You must offer them at the entrance of the Sacred Tent. That is where I will meet with you and speak to you.
“Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
43 That is where I will meet with the Israeli people, and the brilliant light of my presence will cause that place to be holy/sacred.
Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
44 I will dedicate the Sacred Tent and the altar. I will also dedicate Aaron and his sons to serve me [by being] priests.
“Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
45 I will live among the Israeli people, and I will be their God.
Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
46 They will know that I, Yahweh their God, am the one who brought them out of Egypt in order that I might live among them.”
Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.

< Exodus 29 >