< Exodus 28 >
1 “Summon your [older] brother Aaron and his sons—Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar. ([Set them apart/They are the ones whom I have chosen]) from [the rest of] the Israeli people, in order that they can serve me [by being] priests.
“Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
2 [Tell the people to] make beautiful clothes for Aaron, clothes that are [suitable for one who] has this dignified and sacred [work].
Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
3 Talk to all the skilled workmen, those to whom I have given special ability. [Tell them] to make clothes for Aaron, for him to wear when he is (set apart/dedicated) [to become] a priest to serve me.
Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
4 These are the clothes that they are to make: A sacred pouch for Aaron to wear over his chest, a sacred apron, a robe, an embroidered tunic/gown, a (turban/cloth to wrap around his head), and a sash/waistband. These are the clothes that your [older] brother Aaron and his sons must wear as they serve me [by doing the work that] priests do.
Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
5 The skilled workmen must use fine linen and blue, purple, and red yarn/thread to make these clothes.”
Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
6 “The skilled workmen must make the sacred apron from fine linen, and skillfully embroider it with blue, purple, and red yarn/thread.
“Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
7 It must have two shoulder straps, to join the front part to the back part.
Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
8 A carefully-woven sash, which must be made from the same materials as the sacred apron, must be [sewn] onto the sacred apron.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
9 [A skilled workman] must take two [expensive] onyx stones and engrave on them the names of the twelve sons of Jacob.
“Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
10 He must engrave the names in the order in which Jacob’s sons were born. He must engrave six names on one stone, and the other six names on the other stone.
kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
11 A gem-cutter should engrave these names on the stones. Then he should enclose the stones in (settings/tiny gold frames).
Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
12 Then he should fasten the stones onto the shoulder straps [of the sacred apron], to represent the twelve Israeli tribes. In that way, Aaron will carry the names of the tribes on his shoulders in order that [I], Yahweh, will never forget [my people] (OR, in order that [he will always] remember that [those tribes belong to] Yahweh).
na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
13 The settings for the stones must be made from gold.
Tengeneza vijalizo vya dhahabu
14 [Tell them to] make two tiny chains that are braided like cords, and fasten the chains to the settings.”
na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
15 “[Tell the skilled workman to] make a sacred pouch for Aaron to wear over his chest. [He will use the things he puts into the pouch] to determine [my answers to the questions he asks]. It must be made of the same materials as the sacred apron, and embroidered in the same way.
“Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
16 It is to be square, and the material must be folded double, so that it is (9 in./22 cm.) on each side.
Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
17 [The skilled workman must] fasten four rows of valuable stones onto the pouch. In the first row he must put a [red] ruby, a [yellow] topaz, and a [red] garnet.
Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
18 In the second row he must put a [green] emerald, a [blue] sapphire, and a [clear/white] diamond.
katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
19 In the third row he must put a [red] jacinth, a [white] agate, and a [purple] amethyst.
safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
20 In the fourth row he must put a [yellow] beryl, a [red] carnelian, and a [green] jasper.
na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
21 A gem-cutter should engrave on each of these twelve stones the name of one of the sons of Jacob. These names will represent the twelve Israeli tribes.
Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
22 The two [chains] that are made from pure gold and braided like cords are for [attaching] the sacred pouch [to the sacred apron].
“Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
23 [The workman must] make two gold rings, and attach them to the upper corners of the sacred pouch.
Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
24 [He must make] two gold cords, and fasten one end of each cord to one of the rings.
Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
25 He must fasten the other end of each cord to the two settings [that enclose the stones]. In that way, the sacred pouch will be attached to the shoulder straps of the sacred apron.
nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
26 Then [he must] make two more gold rings, and attach them to the lower corners of the sacred pouch, on the inside edges, next to the sacred apron.
Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
27 [He must] make two more gold rings, and attach them to the lower part of the front of the shoulder straps, near to where [the shoulder straps] are joined [to the sacred apron], just above the carefully-woven sash/waistband.
Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
28 The skilled workman must tie the rings on the sacred pouch to the rings on the sacred apron with a blue cord, so that the sacred pouch is above the sash/waistband and does not come loose from the sacred apron.
Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
29 In that way, Aaron will have the names of the twelve Israeli tribes in the sacred pouch close to his chest when he enters the Holy Place. This will remind him that I, Yahweh, [will never forget my people] (OR, [that he represents my people when he talks to me, Yahweh]).
“Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
30 Put into the sacred pouch the two things that the priest will use to determine my answers to the questions he asks. In that way, they will be close to his chest when he enters [the Holy Place to talk] to me. He will use them to find out what is my will for the Israeli people.”
Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
31 “[Tell the workmen to] use only blue [cloth] to make the robe that is to be worn underneath the priest’s sacred apron.
“Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
32 It is to have an opening through which [the priest] can put his head. They must sew a border around this opening, to keep the material from tearing.
na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
33 At the lower edge on the robe, they must fasten [decorations that look like] pomegranate fruit. They must be [woven from] blue, purple, and red yarn/thread.
Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
34 Between each of these decorations, they must fasten a tiny gold bell.
Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
35 When Aaron enters the Holy Place [in the Sacred Tent] to do his work as a priest and when he leaves the Sacred Tent, the bells will ring [as he walks]. As a result, he will not die [because of disobeying my instructions].
Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
36 “[Tell them to] make a tiny ornament of pure gold, and tell a (skilled workman/gem-cutter) to engrave on it the words, ‘Dedicated to Yahweh.’
“Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
37 They should fasten this ornament to the front of the turban by a blue cord.
Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
38 Aaron must always wear this on his forehead. In that way, Aaron himself will show [that he accepts] the guilt if the Israeli people offer [their sacrifices] to me in a way that is not correct, and I, Yahweh, will accept their sacrifices.
Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
39 “[Tell them to] weave the long-sleeved tunic/gown from fine linen. Also, they must make from fine linen a turban and a sash/waistband, and embroider [designs on it].
“Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
40 “[Tell them to] make beautiful long-sleeved tunics/gowns, sashes, and caps for Aaron’s sons. Make ones that will be suitable for those who have this dignified work.
Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
41 Put these clothes on your [older] brother Aaron and on his sons. Then (set them apart/dedicate them) for this work by anointing them [with olive oil], in order that they may serve me [by being] priests.
Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
42 Also [tell them to] make linen undershorts for them. The undershorts should extend from their waists to their thighs, in order that no one can see their private parts.
“Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
43 Aaron and his sons must always wear those undershorts when they enter the Sacred Tent or when they come near to the altar to offer sacrifices in the Holy Place. If they do not obey this command, I will cause them to die. Aaron and all his male descendants must obey this rule forever.”
Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.