< Exodus 26 >
1 “[Tell the people to] make the Sacred Tent using ten long strips of fine linen. They must take blue, purple, and red thread (OR, weave the strips from blue, purple, and red thread), and [a skilled craftsman] must embroider these strips with [designs that represent] the winged creatures [that are above the chest].
“Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
2 Each strip is to be (14 yards/twelve meters) long and (2 yards/1.8 meters) wide.
Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
3 [Tell them to] sew five strips together to make one set, and sew the other five strips together to make another set.
Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
4 For each set, [they must] make loops of blue [cloth] and fasten them along the outer edge of the strip, at the end of each set.
Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
5 [They must] put 50 loops on the edge of the first set, and 50 loops on the edge of the second set.
Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
6 [Tell them to] make 50 gold clasps/fasteners, to fasten both of the sets together. As a result, the inside of the Sacred Tent will be [as though it was] one piece.
Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
7 Also, [tell them to] make a cover for the Sacred Tent from eleven pieces of cloth made from goats’ hair.
“Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
8 Each piece of cloth is to be (15 yards/13.5 meters) long and (2 yards/1.8 meters) wide.
Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
9 [Tell them to] sew five of these pieces of cloth together to make one set, and sew the other six pieces of cloth together to make another set. [They] must fold the sixth piece [of cloth] in half to make it double over the front of the Sacred Tent.
Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
10 [Tell them to] make 100 loops [of blue cloth], and to fasten 50 of them to the outer edge of the one set and fasten 50 to the outer edge of the other set.
Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
11 [Tell them to] make fifty bronze clasps/fasteners and put them in the cloth loops to join the two sets together. As a result, the cover for the Sacred Tent will be [as though it was] one piece.
Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
12 [Let] the extra part of the cover, the part that extends beyond [the linen cloth], hang over the back of the Sacred Tent.
Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
13 The extra half yard/meter of each cover, the part that extends beyond [the linen cloth] on each side, must hang over the two sides of the Sacred Tent, to protect the sides.
Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
14 [Tell them to] make two more covers for the Sacred Tent. One is to be made from rams’ skins that have been (tanned/dyed red), and the top cover is to be made from goatskin leather.”
Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
15 “[Tell them to] make frames from acacia wood, frames that will be set up [from which to hang the Sacred Tent covers].
“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
16 Each frame is to be (five yards/four meters) long and (27 in./66 cm.) wide.
Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
17 [They] must make two projections at the bottom of each frame. These will be to fasten the frames to the bases underneath them. They must make these projections at the bottom of each frame.
zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
18 Make 20 frames for the south side of the Sacred Tent.
Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
19 [Tell them to] make 40 silver bases to go underneath them. Two bases will go under each frame. The projections [at the bottom] of each frame are [to be made] to fit into the bases.
kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
20 [Similarly], [tell them to] make twenty frames for the north side of the Sacred Tent.
Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
21 [They] must make 40 silver bases for them also, with two bases to be put under each frame.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
22 For the rear of the Sacred Tent, on the west side, [tell them to] make six frames.
Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
23 Also, [tell them to] make two extra frames, one for each corner of the rear of the Sacred Tent, [to provide extra support].
na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
24 The two corner frames must be joined from the bottom to the top (OR, joined at both the bottom and the top). At the top of each of the two corner frames there must be a gold ring for holding the crossbar.
Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
25 In that way, [for the rear of the Sacred Tent] there will be eight frames, and there will be 16 bases, two under each frame.
Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
26 [Tell them to] make 15 crossbars from acacia wood.
“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
27 Five of them will be for the frames on the north side of the Sacred Tent, five will be for the south side, and five for the frames at the rear of the Sacred Tent, the west side.
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
28 Tell them to fasten the crossbars on the north, south, and west sides of the Sacred Tent to the middle of the frames. The two long ones must extend from one end of the Sacred Tent to the other, and the crossbar on the west side must extend from one side of the Sacred Tent to the other.
Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
29 [Tell them to] cover the frames with gold, and make gold rings to fasten the crossbars to the frames. The crossbars must [also] be covered with gold.
Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
30 Erect the Sacred Tent in the way that I have shown you [here] on [this] mountain.”
“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
31 “[Tell them to] make a curtain from fine linen. A skilled craftsman must embroider it with blue, purple, and red yarn/thread, making [designs to represent] the winged creatures [that are above the chest].
“Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
32 [Tell them to] suspend/hang the curtain from four posts made from acacia wood and covered with gold. Set [each] post in a silver base.
Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
33 [They] must suspend/hang the [top of the] curtain by hooks that are fastened to the roof of the Sacred Tent. Behind the curtain, in the [room called the] Very Holy Place, [they] must put the chest containing the [two stone slabs on which I have written my] commandments. That curtain will separate the Holy Place from the Very Holy Place.
Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
34 On top of the chest in the Very Holy Place [they] must put the lid which will be the place where [blood will be sprinkled to] forgive people’s sins.
Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
35 [In the room that is] outside of the Very Holy Place, [they] must put the table [for the sacred] bread on the north side, and put the lampstand on the south side.
Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
36 [Tell them to] make a curtain to [cover] the entrance of the Sacred Tent. They must make it from fine linen, and a skilled weaver must embroider it with blue, purple, and red yarn/thread.
“Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
37 To hold up this curtain, [they] must make five posts from acacia wood. [They] must cover them with gold, and fasten gold clasps/fasteners to them. Also [they] must make a bronze base for each of these posts.”
Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.