< Exodus 12 >

1 Yahweh said to Aaron and Moses/me there in Egypt,
Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
2 “[From now on], this month [will be] the first month of the year for you.
“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
3 Tell all the Israeli people that in each family, the man who heads the family must select a lamb or a young goat for his household.
Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
4 If there are not enough people in his family to eat a whole [cooked] lamb, then his family and the family that lives next door may share one animal. Decide how many lambs you need according to the number of people in each family, and according to how much each person can eat.
Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
5 The lambs or goats that you choose must be males, one-year-old, and they must not have any defects.
Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
6 You must take [special] care of these animals until the 14th day of the month. On that day, all the Israeli people must slaughter the lambs [or goats] in the evening.
Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
7 Then they must take some of the blood [from the lambs or goats], and they must smear it on the doorposts and the (lintels/horizontal beams above the doorways) of the houses in which they will eat the meat.
Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
8 They must roast the animals immediately and eat the meat that night. They must eat it with bread that is baked without yeast and with bitter herbs.
Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
9 You must not eat any of the meat raw, and you must not boil the meat. You must roast it [whole], without cutting off the head or the legs or removing the internal parts.
Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
10 You must eat all the meat that evening; do not let any of the meat remain [to be eaten] the next morning. If any of the meat is left until the next morning, you must [completely] burn it.
Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
11 When you eat it, you must be dressed ready to travel, and you must eat it quickly. You must have your sandals on your feet and your walking stick in your hands. It will be a festival [called] Passover to [honor] me, Yahweh.
Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
12 On that night I will go through all the country of Egypt, and I will kill all the oldest males in Egypt, both humans and animals. [By doing this] I will show that all the gods in Egypt are worthless. [I can do this], because I am Yahweh, [the all-powerful God].
“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
13 The blood [that you smear on the doorways will be a mark to indicate] the houses in which you [Israelis] live. When I see the blood, I will [ignore and] pass by those houses, and I will not harm you [Israelis who live there], when I punish the Egyptians.
Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
14 [Each year], you must celebrate this festival on this day, to remember [what I], Yahweh, [have done for you]. In all the generations to come, [each year] you must celebrate [this festival]. [It must continue] forever.
“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
15 For seven days you must eat bread that has no yeast in it. On the first day of that week you must get rid of all the yeast that is in your houses. During those seven days, if anyone eats bread that is baked with yeast in it, [you must consider] that person to be no longer an Israeli.
Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
16 On the first day [of that week], you must (have a holy meeting/gather together to [worship] me). You must do the same thing on the seventh day. People must not work on those two days. The only work they may do is to prepare food for you to eat.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
17 [Every year] you must keep celebrating this festival of eating bread that has no yeast in it, because it will remind you that it was on this day that I brought all your tribal groups out of Egypt. So [every year], in all the generations to come, you must celebrate this day as a festival. It must continue forever.
“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
18 In the first month of the year, on the 14th day of that month, the only bread you may eat is bread that has no yeast in it. You must keep doing that each day until the 21st day of that month. For those seven days you must not have any yeast in your house. [During that time], if anyone, either an Israeli or a foreigner, eats bread made with yeast, you must consider that person no longer to be an Israeli.
Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
20 In your houses, do not eat anything that has yeast in it during those seven days.”
Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 Then Moses/I summoned all the leaders of the Israeli people. He/I said to them, “Each family should select a lamb and kill it, [in order that you may eat it to celebrate the festival that will be called] ‘Passover’.
Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
22 Let the lamb’s blood [drain into] a basin. Get a bunch/sprig of (hyssop/a very leafy plant) and dip it in the blood. Then smear some of the blood on the doorposts and the (lintels/beams above the doorways) [of your houses]. The people in each house must all stay inside the house until the next morning.
Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
23 When Yahweh goes throughout Egypt to kill the [oldest male in each] Egyptian family, he will see the blood on the (lintels/beams of your doorways), and he will [ignore and] pass by those houses. He will not allow the angel who causes people to die to enter your houses and kill [any of] your [oldest sons].
Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
24 You and your descendants must celebrate this festival forever.
“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
25 And when you arrive in the land that Yahweh will be giving to you as he promised, you must keep celebrating this ritual [every year].
Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
26 When your children ask you, ‘What does this ritual mean?’,
Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
27 you must tell them, ‘This ritual is [to remember how our ancestors] sacrificed [lambs] on the night that Yahweh’s angel passed by the houses of the Israeli people [when they were] in Egypt. He killed the [oldest males/sons in all] the Egyptian houses, but he spared [the sons in] [MTY] our houses.’” After Moses/I told them this, they all bowed their heads and worshiped [Yahweh].
Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
28 Then the Israeli people did what Yahweh had told Aaron and Moses/me [to tell them to do].
Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
29 At midnight Yahweh killed all the oldest sons of the Egyptian people, all over Egypt. That included the king’s oldest son, the oldest sons of the prisoners in the dungeon/jail, and [the oldest sons of everyone else]. He also killed the oldest males of all the Egyptians’ livestock.
Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
30 That night the king, all his officials, and [all the rest of] the Egyptian people awoke [and discovered what had happened]. They wailed loudly all over Egypt, because in every house, someone’s son had died.
Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
31 That night the king summoned Aaron and Moses/me and said, “You and all the [other] Israeli people, must leave my country [immediately]! Go and worship Yahweh, as you requested!
Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
32 Take your flocks [of sheep and goats] and herds [of cattle], and leave! And ask Yahweh to bless me, also!”
Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
33 Then the Israeli people did as Moses/I had told them. They [went to] their Egyptian [neighbors] and asked them for silver and gold jewelry and clothing.
Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
34 Yahweh caused the Egyptian people to greatly respect the [Israeli] people, so they gave them what they asked for. In that way, they carried away the wealth of the Egyptian people.
Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
35 The Egyptians urged the [Israeli] people to leave their country quickly. They said, “[If you do not do that], we will all die!”
Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
36 So the [Israeli] people [prepared to leave at once]. They took the bowls in which they mixed the dough to make bread, and the dough that was in the bowls without any yeast in it, and they wrapped the bowls in their cloaks. They put the bowls on their shoulders [and left].
Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
37 The Israeli people traveled from Rameses [city] to Succoth [town]. There were about 600,000 men who went, in addition to the women and children.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
38 Many other people who were not Israelis went along with them. There were also livestock, the flocks [of sheep and goats] and herds [of cattle].
Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
39 On their way, they baked bread with the dough that they carried with them when they had been expelled from Egypt. The dough did not have yeast in it, because they were told to leave Egypt so quickly that they did not have enough time to get food ready to take with them, or enough time to mix yeast in the dough.
Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
40 The Israeli people had lived in Egypt 430 years.
Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
41 On the day that those 430 years ended, on that very day, all the tribes of Yahweh’s people left Egypt.
Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
42 It was a night when Yahweh (protected/guarded over) them as he brought them out of Egypt. So this same night every year is a night that is dedicated to Yahweh, a night when the Israeli people in every generation [remember how] Yahweh protected our ancestors.
Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
43 Then Yahweh said this to Aaron and Moses/me: “These are my instructions about the Passover ritual: Do not let foreigners eat [the Passover meal]. But any male slaves that you have bought may eat it after you have circumcised them.
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45 Do not let people who are living among you temporarily, or servants whom you have hired, eat [the Passover meal].
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46 Each family must eat the Passover meal inside their own house. Do not take any of the food outside the house. And do not break any of the bones of the lamb that is sacrificed.
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47 All the Israeli people must celebrate this festival.
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48 When someone from another country comes to live with you and wants to celebrate the Passover Festival, circumcise all the males in his household. Then they may eat the Passover meal, and you should treat those people as though they were born as Israelis. But do not allow men who have not been circumcised to eat the Passover meal.
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49 These rules apply to people who were born as Israelis and to foreigners who come and live among you.”
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 All the Israeli people obeyed Aaron and Moses/me and did what Yahweh had commanded.
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51 On that very day Yahweh brought all the tribes of the Israeli people out of Egypt.
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.

< Exodus 12 >