< Deuteronomy 25 >

1 “If [two] Israelis have a dispute and they go to a court, the judge will [probably] decide/declare that one of them (is innocent/did not do any wrong) and the other one is guilty.
Iwapo kutakuwa na malumbano kati ya wanaume na wakaenda mahakamani, na waamuzi wakawahukumu, basi watamwachilia mtakatifu na kumhukumu muovu.
2 If the judge says that the guilty person must be punished, he shall command him to lie [with his face] on the ground and be whipped. The number of times he is struck with a whip will depend on [what kind of] crime he committed.
Iwapo mwanamume mwenye hatia anastahili kupigwa, basi muamuzi atamfanya alale chini na kupigwa mbele zake kwa idadi iliyoamriwa kulingana na kosa lake.
3 It is permitted that he be struck as many as 40 times, but no more than that. If he is struck more than 40 times, he would be humiliated publicly.
Muamuzi anaweza kumpatia mapigo arobaini, lakini hapaswi kuvuka idadi hiyo; kwa maana akivuka idadi hiyo na kumpiga kwa mapigo mengi zaidi, basi Muisraeli mwenzako atakuwa kaaibishwa mbele ya macho yenu.
4 When your ox is treading/walking on the grain [to separate the chaff from the grain], do not (muzzle it/put a covering on its mouth) [to prevent it from eating some of the grain].
Haupaswi kumfunga punda wako pua na mdomo anapokuwa akilima shamba lako.
5 If two brothers live on the same property, and one of them who has no son dies, the man’s widow should not marry someone who is not a member of his family. The dead man’s brother must marry her and have sex [EUP] with her. It is his duty to do that.
Iwapo kaka wanaishi pamoja na mmoja wao akafariki bila kuwa na mwana, basi mke wa marehemu hatakiwi kuolewa na mtu nje ya familia. Badala yake, kaka yake mumewe anapaswa kulala naye na kumchukua kuwa mke wake na kutekeleza wajibu wa kaka wa mume kwake.
6 If she later gives birth to a son, that son is to be considered [MTY] the son of the man who died, in order that the dead man’s name will not disappear from Israel.
Hii ni kwamba mtoto wa kwanza atakayezaliwa arithi chini ya jina la kaka yake mwanamume aliyefariki, ili jina lake lisiangamie ndani ya Israeli.
7 “But if the dead man’s brother does not want to marry that woman, she must stand at the (gate/central meeting place) of the town and say to the [town] elders, ‘My husband’s brother will not do (his duty/what he is supposed to do). He refuses to [marry me in order that I may give birth to a son who will] prevent my dead husband’s name from disappearing in Israel.’
Lakini kama mwanamume hataki kumchukua mke wa kaka yake awe wake, basi mke wa kaka yake anapaswa kwenda malangoni mpaka kwa wazee na kusema, “Kaka wa mume wangu amekataa kuwajibika kwa niaba ya jina la kaka yake humu Israeli; hataki kufanya wajibu wa kaka wa mume kwangu”.
8 Then the elders must summon that man and talk to him. If he still refuses to marry that widow,
Kisha wazee wa mji wake wanapaswa kumuita na kuzungumza naye. Lakini tuseme atasisitiza na kusema, “Sitaki kumchukua”.
9 she must go up to him while the elders are watching, and take off one of his sandals [to symbolize/show that he would not receive any of her property], and spit in his face, and say to him, ‘This is what happens to the man who refuses to do what is needed [to allow his dead brother to have a son] in order that our family name does not disappear.’
Basi mke wa kaka yake anatakiwa kuja kwake mbele ya wazee, kumvua ndara zake miguuni mwake, na kumtemea usoni. Anapaswa kumjibu na kusema, “Hivi ndivyo kinachofanyika kwa mwanamume asiyetaka kujenga nyumba ya kaka yake”.
10 After that happens, that man’s family will be known as ‘the family of the man whose sandal was pulled off’.
Jina lake Israeli litaitwa, “Nyumba ya mtu aliyevuliwa ndara zake”.
11 When [two] men are fighting with each other, and the one man’s wife comes near to help her husband by grabbing hold of the other man’s genitals,
Iwapo wanamume wamepigana wao kwa wao, na mke wa mmoja wao kaja kumkomboa mumewe dhidi ya yule aliyempiga, naye akanyosha mkono wake na kumshika sehemu za siri,
12 do not act mercifully toward her; cut off her hand.
basi unapaswa kuukata mkono yake; jicho lako halipaswi kuwa na huruma.
13 “[When you are buying or selling things], do not try to cheat people by having two kinds of weights, [one which you use when you buy something and one which you use when you sell something], and two kinds of measuring baskets, [one which you use when you buy something and one which you use when you sell something].
Haupaswi kuwa na mizani ya uzito tofauti katika mfuko wako, mkubwa na mdogo.
Hautakiwi kuwa na vipimo tofauti ndani ya nyumba yako, vikubwa na vidogo.
15 Always use correct weights and correct measuring baskets, in order that Yahweh our God will allow you to live a long time in the land that he is giving to you.
Unatakiwa kuwa na uzito kamili na wa haki; unatakiwa kuwa na vipimo kamili na vya haki, ili siku zako ziwe ndefu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia.
16 Yahweh hates all those who act dishonestly, [and he will punish them].
Kwa maana wote wanaofanya vitu hivi, wote wanaovunja haki, ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
17 Continue to remember what the Amalek people-group did to your ancestors when they were coming out of Egypt.
Kumbuka ni jambo gani Amaleki alichofanya kwako barabarani ulipokuwa ukitoka Misri,
18 They attacked your ancestors as your ancestors were traveling, when they were weak and exhausted. Those people were not afraid of God at all, so they attacked your ancestors from the rear and killed all those who were unable to walk as fast as the others.
jinsi alivyokutana na wewe barabarani na kuwashambulia kati yenu kwa nyuma, wale waliokuwa wamelegea nyuma, mlipokuwa dhaifu na kuchoka, hakumheshimu Mungu.
19 Therefore, when Yahweh our God has given you the land [that he promised to give you], and when he has enabled you to rest from [fighting] all your enemies around you, kill all the Amalek people-group, with the result that no one will remember them any more. Do not forget [to do this]!”
Kwa hiyo, Yahwe Mungu wako atakapowapa pumziko kutoka kwa maadui zako kila sehemu, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia kumiliki kama urithi, hautakiwi kusahau kuwa unapaswa kufuta kumbukumbu ya Waamaleki chini ya mbingu.

< Deuteronomy 25 >