< Daniel 8 >
1 During the third year that Belshazzar was the King [of Babylonia], I had another vision.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
2 In that vision I was in Susa, the capital city of Elam Province. I was [standing] alongside the Ulai Canal.
Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
3 I looked up and saw a ram that was standing alongside the canal. It had two [long] horns, but the newest one was longer than the other one.
Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
4 The ram butted/knocked away [with its horns] everything that was west and everything that was north and everything that was south of it. There were no [other] animals that were able to oppose it, and none that could rescue/save [other animals] from its power. The ram did whatever it wanted to do and became very powerful.
Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
5 While I was thinking [about what I had seen, in the vision] I saw a goat come from the west. It ran across the land so quickly, that [it seemed like] its feet did not touch the ground. This goat had one very large horn between its eyes.
Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
6 It was very angry, and it ran [straight] toward the ram that I had seen [previously, the ram] that was standing alongside the canal.
Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
7 The goat struck the ram furiously and broke off its two horns, with the result that the ram was unable [to defend itself]. [So] the goat knocked the ram down and trampled on it. No one could rescue the ram from the goat’s power.
Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
8 The goat became very powerful. But when its power was very great, its horn was broken off. But four [other] large horns took its place. They each pointed in a different direction.
Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
9 [Then] from one of those [large horns] appeared a little horn, which became very big, [and pointed] toward the south and [then] toward the east and [then] toward the beautiful land [of Israel].
Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
10 [The man who was represented by] that horn became very strong, with the result that he attacked some of the [soldiers of the] army of heaven, and (OR, meaning) the stars in the sky [which represented God’s people]. He threw some of them to the ground and trampled on them.
Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
11 He (defied/considered himself to be greater than) the leader of the army [of heaven], and prevented [priests from] offering sacrifices to him. He also (defiled the temple/caused the temple to become unholy).
Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
12 Then God’s people allowed the [man who was represented by] that horn to control/rule them, with the result that they sinned by offering sacrifices to him. And he threw to the ground the [laws that contained the] true religion. Everything that he did was successful.
Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
13 Then I heard two angels who were talking to each other. One of them asked, “How long will the things/events that were in this vision continue? How long will the man who rebels against God and causes [the temple] to be defiled be able to prevent [priests from] offering sacrifices? How long will he trample on the temple and on the armies of heaven?”
Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
14 The other angel replied, “[It will continue] for 1,150 days. During all of that time, [people will not be permitted to offer sacrifices] in the morning or in the evening. After that, the temple will be purified.”
Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
15 While I, Daniel, was trying to understand what the vision meant, suddenly [an angel] who resembled a man stood/appeared in front of me.
Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
16 And I heard a man call out from [the other side of] the Ulai Canal, saying, “Gabriel, explain to him the meaning of the vision [that he saw]!”
Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
17 So Gabriel came and stood beside me. I was very terrified, with the result that I fell onto the ground. But he said to me, “You human, it is necessary for you to understand that [the events that you saw in] the vision will occur [near] the time that [the world] will end.”
Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
18 While he was speaking, I fainted. I lay there, unconscious, with my face still on the ground. But Gabriel put his hand on me and lifted me up in order that I could stand again.
Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
19 Then he said, “I [have come here to] tell you what will happen because of [God] being angry. These things will happen near the time when [the world] will end.
Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
20 As for the ram with two horns that you saw, those horns [represent] the kingdoms of Media and Persia.
Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
21 The goat [that you saw represents] the kingdom of Greece, and the horn that appeared between its eyes [represents] its first king.
Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 As for the four horns that grew after the first horn was broken off, they [represent] four kingdoms into which that first kingdom will be divided [after the first king dies]. Those four kingdoms will not be as strong/powerful as the first kingdom was.
Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
23 The people [in those kingdoms] will become very wicked, with the result that it will be necessary for them to be punished. But near the time when those kingdoms will end, one of those kingdoms will have a king who will be very proud/defiant [IDM]. He will [also] be very fierce and very deceitful.
Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
24 He will become very powerful, but it will not be because of what he himself does. He will terribly destroy things in many places, and he will succeed in doing everything that he wants to. He will get rid of [many] powerful men, and [also] some of God’s people.
Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
25 Because he is very cunning/clever, he will succeed by doing things that deceive many people. He will be proud of himself. He will destroy many people when they think that they are safe. He will also rebel against [God] [EUP], who is the greatest king. But [God] will destroy him, without the help [MTY] of any human being.
Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
26 What you saw in the vision about [priests being prevented from making] sacrifices in the morning and in the evening, which [I] explained [to you], will surely happen. But [for the present time], do not reveal the vision [to others], because it will be many years before those things happen.”
Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
27 Then I, Daniel, became weak, and I was sick for several days. Then I arose and [returned to] doing the work that the king [had given to me], but I was perplexed/confused about the vision, and I could not understand it.
Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.