< Amos 1 >

1 This is the message that [Yahweh] gave to [me], Amos. I am a (shepherd/man who takes care of sheep). I am from [near] Tekoa [town south of Jerusalem]. I received this message about Israel in a vision two years before the [big] earthquake. It was when Uzziah was the king of Judah, and Jeroboam, the son of [King] Jehoash, was the king of Israel.
Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
2 This is what Yahweh said: “I will roar [like a lion] [MET]; when I speak from Zion [Hill in] Jerusalem [DOU], my voice will [resemble the sound of] thunder. [When that happens], the pastures where you shepherds [take care of] your sheep will dry up, and [the grass] on top of Carmel [Mountain] will (wither/become brown) [because I will cause that no rain will fall].”
Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
3 This is [also] what Yahweh said [to me]: “[I will punish the people of] Damascus, [the capital of Syria, ] because of the many sins that they have committed; I will not [change my mind about punishing them] [MTY], because [the cruel things that they did to the people of the] Gilead [region] [were like] [MET] people threshing grain using sledges [that have (iron teeth/sharp iron nails) in them].
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
4 I will cause a fire to burn the palace [that King] Hazael [built and lived in], the fortress where [his son King] Ben-Hadad [also] lived.
Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
5 I will cause the gates of Damascus to be broken [down]; I will get rid of the king who rules in Aven Valley and the one who rules in Beth Eden. And the people of Syria will be captured and taken to the Kir [region where they originally lived].”
Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
6 Yahweh [also] said this [to me]: “[I will punish the people of the cities in Philistia]: [I will punish the people of] Gaza [city] because of the many sins that they have committed; I will not change my mind about punishing them, because they captured large groups of people and took them to Edom and sold them to become the slaves of [the people of] Edom.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
7 I will cause a fire to completely burn the walls of Gaza and [also] destroy its fortresses.
nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
8 I will get rid of the king of Ashdod [city] and the king who rules [MTY] in Ashkelon [city]. I will [also] strike/punish [the people of] Ekron [city], and [all] the people of Philistia who are still alive will be killed.”
Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
9 Yahweh [also] said this [to me]: “[I will punish the people of] Tyre [city] because of the many sins that they have committed; I will not change my mind about punishing them, because they [also] captured large groups of our people and took them to Edom, disregarding the treaty of friendship that they had made [with your rulers].
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
10 So I will cause a fire to completely burn the walls of Tyre and [also] destroy its fortresses.”
Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
11 Yahweh [also] said this [to me]: “I will punish [the people of] Edom because of the many sins that they have committed; I will not change my mind about punishing them, because they pursued the people [of Israel], who descended from Esau’s [brother Jacob, and killed them] with swords; they did not act mercifully toward them at all. They were extremely angry [with the people of Israel], and they continued to be angry [with them].
Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
12 I will cause a fire to burn Teman [district in Edom] and completely burn the fortresses of Bozrah, [the biggest city in Edom].”
Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
13 Yahweh [also] said this [to me]: “I will punish [the people of] Ammon because of the many sins that [they] have committed; I will not change my mind about punishing them, because [their soldiers even] ripped open [the bellies of] pregnant women [when their army attacked] the Gilead [region] to gain more territory.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
14 I will cause a fire to [completely] burn the walls around Rabbah [city] and completely burn its fortresses. During that battle, [their enemies] will shout loudly and the fighting will be [like] [MET] a fierce/raging wind/storm.
Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
15 [After the battle], the king [of Ammon] and his officials will be (exiled/forced to go to another country).”
Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.

< Amos 1 >