< Acts 27 >
1 When [the Governor and those who advised him] decided that it was time for us [(exc)] to get on a ship and go to Italy, they put Paul and some other prisoners into the hands/care of an army captain whose name was Julius. [He was the one who would guard us on the journey]. Julius was [an officer] in charge of [a group of] 100 [soldiers that people called] ‘the Emperor Augustus Group’.
Ilipoamuliwa kwamba tungesafiri kwa njia ya bahari kwenda Italia, Paulo na wafungwa wengine wakakabidhiwa kwa kiongozi mmoja wa askari aliyeitwa Juliasi, aliyekuwa wa Kikosi cha Walinzi wa Kaisari.
2 So we got on a ship that had come from Adramyttium [city in Asia province. The ship] was going to [return there, stopping at] cities along the coast of Asia [province]. Aristarchus, [a fellow believer who was] from Thessalonica [city] in Macedonia [province], went with us.
Tulipanda meli iliyotoka Adramitio, iliyokuwa inakaribia kusafiri kwenda kwenye bandari zilizopo pwani ya Asia, tukaanza safari yetu tukiwa pamoja na Aristarko, Mmakedonia kutoka Thesalonike.
3 The day after [the ship sailed], we arrived at Sidon [city]. Julius kindly told Paul that he could go and see his friends [who lived there], so that they could give him whatever he might need. [So Paul visited the believers there].
Kesho yake tukatia nanga Sidoni, naye Juliasi akamfanyia wema Paulo, akamruhusu aende kwa rafiki zake ili wamtimizie mahitaji yake.
4 Then the ship left [Sidon], but the winds were blowing against us [(exc)], so [the ship] went along [the north] side of Cyprus [Island], the side that is sheltered [from the wind].
Kutoka huko tukaingia baharini tena na tukapita upande wa chini wa kisiwa cha Kipro kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
5 After that, we crossed over the sea close to the coast of Cilicia and Pamphylia [provinces. The ship] arrived at Myra [city, which is] in Lycia [province]. [We got off the ship there].
Baada ya sisi kuvuka bahari iliyoko upande wa Kilikia na Pamfilia, tukafika Mira huko Likia.
6 In Myra, [people told] Julius that a ship [was there that had come] from Alexandria [city] and would [soon] sail to Italy. So he arranged for us to get [on that ship], [and we left].
Huko yule kiongozi wa askari akapata meli ya Iskanderia ikielekea Italia, akatupandisha humo.
7 We sailed slowly for several days and finally arrived close to the coast [of Asia province], near Cnidus [town. After that], the wind [was very strong and] did not allow the ship to move straight ahead [westward. So instead], we sailed [southward] along the side of Crete [Island that is] sheltered [from the wind], and we passed [near Cape] Salmone.
Tukasafiri polepole kwa siku nyingi na kwa shida, hatimaye tukafika karibu na Nido. Kwa kuwa upepo wa mbisho ulituzuia tusiweze kushika mwelekeo tuliokusudia, tukapita chini ya Krete mkabala na Salmone.
8 [The wind was still strong, and it prevented the ship from moving ahead fast]. So we moved slowly along the coast [of Crete], and we arrived at a harbor that was called Fair Havens, near Lasea [town].
Tukaambaa na pwani kwa shida, tukafika sehemu iitwayo Bandari Nzuri, karibu na mji wa Lasea.
9 Much time had passed, so it would have been dangerous if we [(exc)] had traveled [farther] by ship [because after that time of the year] [MTY] [the sea often became very stormy]. So Paul said to the men [on the ship],
Muda mwingi ulikuwa umepotea na kusafiri baharini kulikuwa hatari kwa sababu wakati huu ulikuwa baada ya siku za kufunga. Hivyo Paulo akawaonya akasema,
10 “Men, I perceive that [if we(inc) travel by ship] now, it will be disastrous for us. A storm may destroy the ship and the cargo, and possibly we will drown.”
“Mabwana, naona kuwa hii safari ni yenye maafa na ya kuleta hasara kubwa kwa meli na shehena, pia kwa maisha yetu.”
11 But the officer [did not listen to] what Paul said. Instead, he decided to do what the pilot [of the ship] and the owner of the ship advised.
Lakini badala ya yule kiongozi wa askari kusikiliza yale Paulo aliyosema, akafuata zaidi ushauri wa nahodha na mwenye meli.
12 The harbor where the ship had stopped was not a good place to remain during the winter [when the weather frequently becomes stormy. So most of the people on the ship decided that we(exc) should leave there, because they hoped that we] could stay at Phoenix [port] during the winter, if we could possibly arrive there. That harbor was open to the sea in two directions, [but the strong winds did not blow there].
Kwa kuwa ile bandari ilikuwa haifai kukaa wakati wa majira ya baridi, wengi wakashauri kwamba tuendelee na safari wakitarajia kufika Foinike na kukaa huko kwa majira ya baridi. Hii ilikuwa bandari iliyoko katika kisiwa cha Krete ikikabili upande wa kusini-magharibi na kaskazini-magharibi.
13 Then a gentle wind began to blow [from the south], and the [crew members] thought that they could travel as they had decided [to do. So] they lifted [the anchor up out of the sea], and the ship sailed [westward] along the [southern] shore of Crete [Island].
Upepo mtulivu ulipoanza kuvuma toka kusini, wakadhani kuwa wangeweza kufikia lengo lao, hivyo wakangʼoa nanga na kusafiri wakipita kandokando ya pwani ya kisiwa cha Krete.
14 But after a while, a wind that was very strong blew across the island [from the north side and hit the ship. That wind was called] {[People] called that wind} “the Northeast Wind.”
Lakini baada ya muda mfupi ikavuma tufani kubwa iitwayo “Eurakilo” toka kisiwa cha Krete.
15 It blew strongly against the [front of] the ship. The result was that we could not keep going in the direction [in which we had been going]. So the sailors let the wind move the ship in the direction [that the wind] was blowing.
Meli ikapigwa na dhoruba na haikuweza kushindana na ule upepo, tukarudishwa baharini upepo ulikokuwa unaelekea.
16 The ship then passed a small island named Cauda. We passed along the side [of the island that] sheltered [the ship from the wind]. Then [while the ship was moving along], the sailors lifted the lifeboat up [out of the water] and tied it [on the deck. But the strong wind made it] difficult even to do that.
Hatimaye tukisafiri kupita chini ya kisiwa kidogo kiitwacho Kauda, ambapo kwa kuwa tulikuwa tumekingiwa upepo na hicho kisiwa, tuliweza kwa shida kuifunga mashua ya kuokolea watu.
17 After the sailors [hoisted/lifted] the lifeboat onto the ship, they tied ropes around the ship’s hull to strengthen the ship. The sailors were afraid that, [because the wind was pushing the ship], it might run onto the sandbanks off the coast of Libya to the south [and get stuck there. So] they lowered the largest sail [so that the ship would move slower. Even so], the wind continued to move the ship along. [The wind and the waves] continued to toss the ship about roughly, so on the next day the sailors began to throw overboard the things that the ship was carrying.
Watu walipokwisha kuivuta mashua hiyo na kuiingiza katika meli, waliifunga kwa kamba chini ya meli yenyewe ili kuzishikanisha pamoja. Wakiogopa kupelekwa kwenye mchanga karibu na pwani ya Sirti, wakashusha matanga wakaiacha meli isukumwe na huo upepo.
Tulikuwa tunapigwa na dhoruba kwa nguvu, kiasi kwamba kesho yake walianza kutupa shehena toka melini.
19 On the third [day after the stormy wind had begun to blow], the sailors/we [MTY] threw overboard [most of] the sails, ropes, and poles, [in order to make the ship lighter].
Siku ya tatu, wakatupa vyombo vya meli baharini kwa mikono yao wenyewe.
20 The wind continued to blow very strongly, [and the sky was full of dark clouds] day and night. We could not see the sun or the stars for many days, [so we could not determine where we were. And the wind] continued to blow violently. So we [(exc)] finally thought that we would drown in the sea.
Kulipokuwa hakuna kuonekana kwa jua wala nyota kwa siku nyingi, nayo dhoruba ikiwa inaendelea kuwa kali, hatimaye tulikata kabisa tamaa ya kuokoka.
21 None of us on the ship had eaten for many days. [Then one day], Paul stood up in front of us and said, “[Friends], you should have listened to me [when I said] that we [(inc)] should not sail from Crete. Then we would have been safe, and the ship and its cargo would be in good condition [LIT].
Baada ya watu kukaa siku nyingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao akasema, “Enyi watu, iliwapasa kunisikiliza na kuacha kusafiri baharini kutoka Krete, ndipo ninyi mngekuwa mmejinusuru na uharibifu huu na hasara hii.
22 But now, I urge you, do not be afraid, because none of us will die. [The storm] will destroy the ship but not us.
Sasa ninawasihi sana, jipeni moyo mkuu kwa kuwa hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake, ila meli itaangamia.
23 I [know this], because last night God, the one to whom I belong and whom I serve, [sent] an angel [who came and] stood by me.
Jana usiku, malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake na ambaye ninamwabudu alisimama karibu nami,
24 The angel said to me, ‘Paul, do not be afraid! You [(sg)] must [go to Rome] and stand before the Emperor there [so that he can judge you]. I want you to know that God has made it clear to me that all those who are traveling by ship with you [will also survive].’
naye akasema, ‘Paulo usiogope, kwa kuwa ni lazima usimame mbele ya Kaisari, naye Mungu amekupa kwa neema uhai wa wote wanaosafiri pamoja nawe.
25 So cheer up, [my] friends, because I believe that God will make this happen, exactly as [the angel] told me.
Hivyo jipeni moyo, enyi watu, kwa kuwa ninamwamini Mungu kwamba yatakuwa kama vile alivyoniambia.’
26 However, [the ship] will crash on some island, [and] we [(inc)] will go ashore [there].”
Lakini hata hivyo meli yetu itakwama kwenye kisiwa fulani.”
27 On the fourteenth night [after the storm had begun, the ship] was still being blown {the wind was still blowing [the ship]} across the Adriatic sea. About midnight, the sailors sensed that the ship was getting close to land.
Usiku wa kumi na nne ulipofika, tulikuwa bado tunasukumwa na upepo katika Bahari ya Adria. Ilipokuwa yapata usiku wa manane, mabaharia wakahisi kwamba walikuwa wanakaribia nchi kavu.
28 So they lowered [a weight on a rope] to measure how deep [the water was]. When they pulled the rope up again, they measured it and saw that the water was (120 ft./37 meters) deep. They went a little farther and lowered the rope again. [That time], they saw that the water was [only] about (90 ft./28 meters) deep.
Kwa hiyo wakapima kina cha maji na kukuta kilikuwa pima ishirini, baada ya kuendelea mbele kidogo wakapima tena wakapata kina cha pima kumi na tano.
29 They were afraid that the [ship] might go onto some rocks, so they threw out four anchors from the [ship’s] stern/back and continued to wish/pray that it would soon be dawn [so that they could see where the ship was going].
Wakiogopa kwamba meli yetu ingegonga kwenye miamba, wakashusha nanga nne za nyuma ya meli, wakawa wanaomba kupambazuke.
30 Some of the sailors were planning to escape from the ship, so they lowered the lifeboat into the sea. In order [that no one would know what they planned to do], they pretended [that] they wanted to lower some anchors from the [ship’s] front/bow.
Katika jaribio la kutoroka kutoka kwenye meli, mabaharia wakashusha mashua ya kuokolea watu baharini, wakijifanya kwamba wanakwenda kushusha nanga za omo.
31 But Paul said to the army officer and soldiers, “If the sailors do not stay in the ship, you have no hope of being saved.”
Ndipo Paulo akamwambia yule jemadari na askari, “Hawa watu wasipobaki katika meli, hamtaweza kuokoka.”
32 So the soldiers cut the ropes and let the lifeboat fall into the water.
Hivyo basi wale askari wakakata kamba zilizoshikilia ile mashua ya kuokolea watu kwenye meli, wakaiacha ianguke humo baharini.
33 Just before dawn, Paul urged everyone [on the ship] to eat some food. He said, “For the past 14 days you have been waiting and watching and not eating anything.
Kabla ya mapambazuko, Paulo akawasihi watu wote wale chakula akisema, “Leo ni siku ya kumi na nne mmekuwa katika wasiwasi mkiwa mmefunga na bila kula chochote.
34 So, [now] I urge you to eat some food. We [(inc)] need to do that in order to stay alive. I [tell you to do that because I know that] none of you will drown [IDM].”
Kwa hiyo nawasihi mle chakula, kwa maana itawasaidia ili mweze kuishi. Kwa kuwa hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza unywele hata mmoja kutoka kichwani mwake.”
35 After Paul had said that, while everyone was watching, he took some bread and thanked God [for it. Then he broke the bread and began to eat some of it].
Baada ya kusema maneno haya, Paulo akachukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega akaanza kula.
36 The [rest of us] became encouraged, so we [(exc)] all ate some food.
Ndipo wote wakatiwa moyo, wakaanza kula chakula.
37 Altogether there were 276 of us [SYN] on the ship.
Ndani ya meli tulikuwa jumla ya watu 276.
38 When everyone had eaten as much as they wanted, they threw the grain [that the ship was carrying] into the sea, and this made the ship lighter.
Baada ya watu wote kula chakula cha kutosha, wakapunguza uzito wa meli kwa kutupa ngano baharini.
39 At dawn, [we(exc) could see] land, [but the sailors] did not recognize [the place]. However, they could see that there was a bay and [a wide area of] sand at the water’s edge. They planned that, if it was possible, they would steer the ship onto [the beach].
Kulipopambazuka, mabaharia hawakuitambua ile nchi, lakini waliona ghuba yenye ufuko wa mchanga, ambako waliamua kuipweleza meli kama ingewezekana.
40 [So some of the sailors] cut the anchor [ropes and] let the anchors fall into the sea. At the same time, [other sailors] untied the [ropes that] fastened the rudders, [so that they could steer the ship again]. Then [the sailors] raised the sail at the front/bow of the ship so that the wind [would blow the ship forward], and the ship headed towards the shore.
Kwa hiyo wakatupa nanga zote na kuziacha baharini, na wakati huo huo wakalegeza kamba zilizokuwa zikishikilia usukani wa meli. Kisha wakatweka tanga la mbele lishike upepo na kuisukuma meli kuelekea pwani.
41 But the ship hit a sandbank. The front of the ship stuck there and could not move, and big waves beat against the back of the ship and it began to break apart.
Lakini wakafika mahali ambapo bahari mbili zinakutana, wakaipweleza meli ufuoni, omo ikakwama sana, ikawa haiwezi kuondolewa, lakini sehemu ya shetri ikavunjika vipande vipande kwa kule kupiga kwa mawimbi yenye nguvu.
42 The soldiers said [to one another, “Let’s] kill [all] the prisoners [on the ship], so that they will not [be able to] swim [away and] escape.” [They planned to do that because they were sure] that officials [would order them to be executed if they let the prisoners escape].
Wale askari wakapanga kuwaua wale wafungwa ili kuzuia hata mmoja wao asiogelee na kutoroka.
43 But [Julius], the army captain, wanted to save Paul, so he stopped the soldiers from doing what they planned to do. Instead, he [commanded] first that everyone who could swim should jump into the water and swim to land.
Lakini yule jemadari alitaka kuokoa maisha ya Paulo, basi akawazuia askari wasitekeleze mpango wao. Akaamuru wale wanaoweza kuogelea wajitupe baharini kwanza, waogelee mpaka nchi kavu.
44 [Then he told] the others [to hold] onto planks or pieces from the ship [and go towards shore. We(exc) did what he said, and] in that way all of us arrived safely on land.
Waliosalia wangefika nchi kavu kwa kutumia mbao au vipande vya meli iliyovunjika, hivyo ikatimia kwamba wote wakaokoka na kufika nchi kavu salama.