< Acts 10 >

1 [There was] a man [who lived] in Caesarea [city] whose name was Cornelius. He was an officer who commanded 100 men in a large group of [Roman] soldiers from Italy.
Katika mji wa Kaisaria palikuwa na mtu jina lake Kornelio, ambaye alikuwa jemadari wa kile kilichojulikana kama kikosi cha Kiitalia.
2 He always tried to do what would please God; he and his entire household [MTY] [were non-Jews who] habitually worshipped God. He sometimes gave money to help poor [Jewish] people, and he prayed to God regularly.
Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na wote wa nyumbani mwake. Aliwapa watu sadaka nyingi na kumwomba Mungu daima.
3 [One day] at about three o’clock in the afternoon [Cornelius saw] a vision. He clearly saw an angel whom God [had sent]. The angel came into [his room] and said to him, “Cornelius!”
Siku moja alasiri, yapata saa tisa, aliona maono waziwazi, malaika wa Mungu akimjia na kumwambia, “Kornelio!”
4 Cornelius stared at the angel and became terrified. Then he asked [fearfully], “Sir, what do you [(sg)] want?” The angel answered him, “You [(sg)] have pleased God because you have been praying [regularly to him] and you often give money to [help] poor people. [Those things have been] like a sacrifice [to God].
Kornelio akamkazia macho kwa hofu akasema, “Kuna nini, Bwana?” Malaika akamwambia, “Sala zako na sadaka zako kwa maskini zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.
5 So, now command some men to go to Joppa and [tell them to] bring back a man named Simon whose other name is Peter.
Sasa tuma watu waende Yafa wakamwite mtu mmoja jina lake Simoni aitwaye Petro.
6 He is staying with a man, [also] named Simon, who makes leather. His house is near the ocean.”
Yeye anaishi na Simoni mtengenezaji ngozi ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.”
7 When the angel who spoke to Cornelius had gone, Cornelius summoned two of his household servants and a soldier who served him, one who also worshipped God.
Yule malaika aliyekuwa akizungumza naye alipoondoka, Kornelio akawaita watumishi wake wawili pamoja na askari mmoja mcha Mungu aliyekuwa miongoni mwa wale waliomtumikia.
8 He explained to them everything [that the angel had said. Then] he told them to go to Joppa [to ask Peter to come to Caesarea].
Akawaambia mambo yote yaliyotukia, kisha akawatuma waende Yafa.
9 About noon the next day those [three men] were traveling [along the road] and were coming near [Joppa. As they were approaching Joppa], Peter went up on the [flat] housetop to pray.
Siku ya pili yake, walipokuwa wameukaribia mji, wakati wa adhuhuri, Petro alipanda juu ya nyumba kuomba.
10 He became hungry and wanted something to eat. While someone was preparing the food, [Peter] saw [this] vision:
Alipokuwa akiomba akahisi njaa, akatamani kupata chakula. Lakini wakati walikuwa wakiandaa chakula, akalala usingizi mzito sana.
11 (He saw heaven open/He saw an opening in the sky) and something like a large sheet was being lowered [to the ground]. [It was tied at] its four corners [with ropes].
Akaona mbingu zimefunguka na kitu kama nguo kubwa kikishushwa duniani kwa ncha zake nne.
12 Inside the sheet were all kinds of creatures. [These included animals and birds that the Mosaic laws forbade Jews to eat]. Some had four feet, others scurried across the ground, and others were wild birds.
Ndani yake walikuwepo aina zote za wanyama wenye miguu minne, nao watambaao nchini, na ndege wa angani.
13 Then [he heard] God [SYN] say to him, “Peter, stand up, kill [and cook some of these] and eat [their meat]!”
Ndipo sauti ikamwambia “Petro, ondoka, uchinje na ule.”
14 But Peter replied, “Lord, surely you [(sg)] do not [really want me to do that]! I have never eaten any [meat] that [our Jewish law says] is unacceptable to God or [something that we(exc)] must not eat!”
Petro akajibu, “La hasha Bwana! Sijawahi kamwe kula kitu chochote kilicho najisi.”
15 [Then Peter heard] [MTY] God talk to him a second time. He said, “[I am] God, [so] if I have made something acceptable [to eat], do not say that it is not acceptable [to eat]!”
Ile sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”
16 [This happened] three [times, so Peter knew that he had to think carefully about what it might mean]. Immediately [after God had said that the third time], ([the] sheet [with the animals and birds] was the pulled back into heaven/[someone] pulled the sheet [with the animals and birds] up into the sky again).
Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.
17 While Peter was trying to understand what that vision meant, the men who had been sent by Cornelius {whom Cornelius had sent} [arrived in Joppa. They asked people how to get to] Simon’s house. [So they found his house] and were standing outside the gate.
Wakati Petro akiwa bado anajiuliza kuhusu maana ya maono haya, wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio wakaipata nyumba ya Simoni mtengenezaji wa ngozi wakawa wamesimama mbele ya lango.
18 They called and were asking if a man named Simon, whose other name was Peter, was staying there.
Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.
19 While Peter was still trying to understand [what] the vision [meant], [God’s] Spirit said to him, “Three men [are here who] want to see you.
Wakati Petro akiwa anafikiria juu ya yale maono, Roho Mtakatifu akamwambia, “Simoni, wako watu watatu wanaokutafuta.
20 So get up and go downstairs and go with them! Do not think that you [(sg)] should not go with them [because of their being non-Jews], because I have sent them [here]!”
Inuka na ushuke, usisite kwenda nao kwa kuwa mimi nimewatuma.”
21 So Peter went down to the men and said to them, “[Greetings!] I am [the man] you are looking for. Why have you come?”
Petro akashuka na kuwaambia wale watu waliokuwa wametumwa kutoka kwa Kornelio, “Mimi ndiye mnayenitafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
22 One of them replied, “Cornelius, who is a [Roman] army officer, [sent us here]. He is a righteous man who worships God, and all of the Jewish people [HYP] [who know about him] say that he is a very good man. An angel (who was sent from God/whom God sent) said to him, ‘Tell some men to [go to Joppa to see Simon Peter and] bring him here, so that you [(sg)] can hear what he has to say.’”
Wale watu wakamjibu, “Tumetumwa na Kornelio yule jemadari. Yeye ni mtu mwema anayemcha Mungu, na anaheshimiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagizwa na malaika mtakatifu akukaribishe nyumbani kwake, ili asikilize maneno utakayomwambia.”
23 So Peter [said that he would go with them, and then he] invited them into [the house] and told them that they could stay [there that night]. Acts 10:23b-26 The next day Peter got ready and went with the men. Several of the believers from Joppa went with him.
Basi Petro akawakaribisha wakafuatana naye ndani, akawapa pa kulala. Kesho yake akaondoka pamoja nao, na baadhi ya ndugu kutoka Yafa wakafuatana naye.
24 The day after that, they arrived in Caesarea. Cornelius was waiting for them. He had also invited his relatives and close friends [to come to his house, so they were there, too].
Siku iliyofuata wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangoja pamoja na jamaa yake na marafiki zake wa karibu.
25 When Peter entered the house, Cornelius met him and bowed low in front of him to worship him.
Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akaanguka miguuni pake kwa heshima.
26 But Peter [grasped Cornelius by the hand and] lifted him to his feet. He said, “Stand up! [Do not revere/worship me] I myself am only human, [like you]!”
Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama, mimi ni mwanadamu tu.”
27 While he was talking to Cornelius, Peter [and the others] entered [a large room inside the house]. Peter saw that many people had gathered together [there].
Petro alipokuwa akizungumza naye akaingia ndani na kukuta watu wengi wamekusanyika.
28 Then Peter said to them, “You all know that any [of us] Jews think we are disobeying [our Jewish] laws if we [(exc)] associate with a non-Jewish person or [if we even] visit him. However, God has shown me [in a vision] that I should not say about anyone that God will not accept him.
Akawaambia, “Mnajua kabisa kwamba ni kinyume cha sheria yetu Myahudi kuchangamana na mtu wa Mataifa au kumtembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwite mtu yeyote kuwa najisi au asiye safi.
29 So when you sent [some men] to ask me to come [here], I came [right away. I] did not say that I could not go [with non-Jewish people. So, please tell me], why have you asked me to come [here]?”
Ndiyo sababu ulipotuma niitwe nilikuja bila kupinga lolote. Basi sasa naomba unieleze kwa nini umeniita?”
30 Cornelius replied, “About this time four days ago I was praying [to God] in my house, [as I regularly do] at three o’clock in the afternoon. Suddenly a man whose clothes [shone] brightly stood in front of me,
Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa alasiri. Ghafula mtu aliyevaa nguo zilizongʼaa akasimama mbele yangu,
31 and said, ‘Cornelius, when you [(sg)] have prayed, you have been heard by God {God has heard [when] you [(sg)] have prayed [to him]}. He has also noticed that you have [often] given money to [help] poor people, [and he is pleased with that].
akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na sadaka zako kwa maskini zimekumbukwa mbele za Mungu.
32 So now, send [messengers to go] to Joppa, [in order] to ask Simon whose other name is Peter to come [here]. He is staying near the ocean in a house that belongs to [another] man named Simon, who makes leather. [When Simon Peter comes, he will tell you a message from God].’
Basi tuma watu waende Yafa wakaulize mtu mmoja Simoni aitwaye Petro, yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi, ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.’
33 So I immediately sent [some men who asked] you [(sg) to come here], and I [certainly] thank you for coming. Now we [(exc)] all are gathered [here, knowing that] God is with us, in order to hear all the things that the Lord [God] has commanded you [to say. So please speak to us].”
Nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vyema kuja. Basi sasa sisi sote tuko hapa mbele za Mungu kuyasikiliza yote ambayo Bwana amekuamuru kutuambia.”
34 So Peter began to speak [MTY] to them. He said, “[Now] I understand that it is true that God does not favor only certain groups [of people].
Ndipo Petro akafungua kinywa chake akasema, “Mungu hana upendeleo,
35 Instead, from every group of people he accepts [everyone who] honors him and who does what pleases him.
Lakini katika kila taifa, kila mtu amchaye na kutenda yaliyo haki hukubaliwa naye.
36 [You know] the message that God sent to [us] Israelis. [He] proclaimed [to us the good news that he] would cause [people] to have peace [with him] because of what Jesus Christ [has done]. This [Jesus is Lord not only over us Israelis. He] is [also the] Lord [who rules] over all [people].
Ninyi mnajua ule ujumbe uliotumwa kwa Israeli, ukitangaza habari njema za amani kwa Yesu Kristo. Yeye ni Bwana wa wote.
37 You know what [he] did throughout the land of Judea, beginning in Galilee. He began [to do those things] after John had been proclaiming [to people that they should turn away from their sinful behavior before] he baptized them.
Mnajua yale yaliyotukia katika Uyahudi wote kuanzia Galilaya baada ya mahubiri ya Yohana Mbatizaji:
38 You know that God gave [MTY] his Holy Spirit to Jesus, [the Man] from Nazareth [town], and gave him the power [to do miracles. You also know] how Jesus went to many places, always doing good deeds and healing [people. Specifically], he was continually healing all the people whom the devil was causing to suffer. [Jesus was able to do those things] because God was always helping him.”
Jinsi Mungu alivyomtia Yesu wa Nazareti mafuta katika Roho Mtakatifu na jinsi alivyokwenda huku na huko akitenda mema na kuponya wote waliokuwa wameonewa na nguvu za ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.
39 “We [apostles] tell people about all the things that [we saw Jesus] do in Jerusalem and in the [rest of] Israel. [The leaders in Jerusalem] had him killed by being nailed to a cross.
“Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika Uyahudi na Yerusalemu. Wakamuua kwa kumtundika msalabani.
40 However, God caused him to become alive again on the third day [after he had died]. God [also] enabled [some of us(exc)] to see him [so that we would know that he was alive again].
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamwezesha kuonekana na watu.
41 God [did] not [let] all the [Jewish] people see him. Instead, he had chosen us [apostles] beforehand to see [Jesus after he became alive again], and to tell others [about him]. We [apostles are the people] who ate meals with him (after he had become alive [again]/after he had risen from the dead).
Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwetu sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa mashahidi, ambao tulikula na kunywa naye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
42 God commanded us to preach to the people and tell them that Jesus is the one whom he has appointed to judge [everyone some day. He will judge all] those who will [still] be living and all those who will have died [by that time].
Naye alituamuru kuhubiri kwa watu wote na kushuhudia kwamba ndiye alitiwa mafuta na Mungu kuwa hakimu wa walio hai na wafu.
43 All of the prophets [who wrote about the Messiah long ago] told [people] about him. [They wrote] that if people believe in the Messiah [MTY], God would forgive [them for] their sins, because of what [the Messiah would do] for them.”
Manabii wote walishuhudia juu yake kwamba kila mtu amwaminiye hupokea msamaha wa dhambi katika Jina lake.”
44 While Peter was still speaking those words, suddenly the Holy Spirit (came down on/began to control) all [those non-Jewish people] who were listening to the message.
Wakati Petro alikuwa akisema maneno haya, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wakisikiliza ule ujumbe.
45 The Jewish believers who had come with Peter [from Joppa] were amazed that [God] had generously given the Holy Spirit to the non-Jewish people, too.
Wale wa tohara walioamini waliokuja na Petro walishangaa kwa kuona kuwa kipawa cha Roho Mtakatifu kimemwagwa juu ya watu wa Mataifa.
46 [The Jewish believers knew that God had done that] because they were hearing those people speaking languages [MTY] [that they had not learned] and telling how great God is.
Kwa kuwa waliwasikia wakinena kwa lugha mpya na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akasema,
47 Then Peter said [to the other Jewish believers who were there], “[God] has given them the Holy Spirit just like [he gave him] to us [Jewish believers], so (surely all of you would agree that [we(exc)] should baptize these people!/would any of you forbid that these people should be baptized?) [RHQ]”
“Je, kuna mtu yeyote anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea.”
48 Then Peter told those [non-Jewish] people that they should be baptized [to show that they had believed] [MTY] in the [Lord] Jesus Christ. [So they baptized all of them. After they were baptized], they requested that Peter stay [with them] several days. [So Peter and the other Jewish believers did that].
Kwa hiyo akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Wakamsihi Petro akae nao kwa siku chache.

< Acts 10 >