< 2 Timothy 4 >
1 Christ Jesus [is going to come back and] judge those who are living [when he comes] and those who will have died. He will judge them [concerning what rewards they deserve, and] he will rule everyone. So, [knowing that] he and God are watching [everything that we do], I solemnly/earnestly command you
Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:
2 that you proclaim the [true] message to people. Always be ready/prepared [to proclaim it], whether people want to hear it or not. [Some people are saying things that are not correct]; (refute their teaching/show why their teaching is wrong). Rebuke them when they are doing wrong. Tell them what they ought to do. Be very patient while you teach them.
Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.
3 [Do these things] because there will be a time when people will not listen to good teaching. Instead, they will bring in many teachers for themselves who will tell them just what they want to hear [IDM]. [The reason that they will bring in such teachers is] that they want to do the evil things that they desire.
Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.
4 That is, they will not listen to [MTY] what is true, but will listen instead to [strange] stories from our ancestors.
Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.
5 [Furthermore, I command that] you always control what you think and do. [Be willing] to endure hardships/suffering. Your work should be telling people the message [about Christ Jesus]. As you serve [the Lord], do everything that [God has told] you to do.
Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.
6 [Timothy, I say these things to] you because as for me, [it is as though] [MET] [they are now about to kill me. It is as though my blood will] be poured out {they will kill me} [as a sacrifice on the altar]; that is, [I know] that it is the time for me to die [EUP].
Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.
7 [And as to telling people the] good [message and defending it], I have (exerted myself thoroughly/done it with all my energy) [MET], [like a boxer does. As to doing] the work that God gave me to do, I have completed it, [like a runner who finishes] [MET] the race. [As to] what we believe, I (have been loyal to it/continue to believe it).
Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
8 [So, like people award] a prize [MET] [to the winner of a race], the Lord, who judges rightly, will give me a reward [because I have lived] righteously. He will give me that reward when [MTY] [he judges people]. And not only [will he reward] me, but he will also reward all those who very much want him to come back.
Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.
9 (Do your best/Try hard) to come to me soon.
Jitahidi kuja kwangu upesi
10 [I say that] because Demas has left me. He wanted very much [the good things that he might enjoy] [MTY] in this world [right now], and so he went to Thessalonica [city]. Crescens [went to serve the Lord] in Galatia [province], and Titus went to Dalmatia [district]. (aiōn )
kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn )
11 Luke is the only one who is still with me [of those who were helping me. And when you come], bring Mark with you, because he is useful to help me in my work.
Ni Luka peke yake aliye hapa pamoja nami. Mtafute Marko uje naye kwa sababu ananifaa sana katika huduma yangu.
12 Tychicus [cannot help me because] I sent him to Ephesus [city].
Nimemtuma Tikiko huko Efeso.
13 And when you come, bring the coat that I left with Carpus in Troas [city]. Also, bring the books, but (most of all/especially) [I want] (the parchments/the animal skins) [on which important things are written].
Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.
14 Alexander, the man who makes things from metal, did many evil/harmful things to me. The Lord will punish him for what he did.
Aleksanda yule mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Bwana atamlipa kwa ajili ya yale aliyotenda.
15 So you, too, must beware of him. [He will try to destroy your work if he can], because he very much opposes the message that we [proclaim].
Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
16 When I first defended myself [in court here], no one came along [to help defend] me. Instead, they all left me. [I pray] that it will not be counted against {[God] will forgive} them [LIT] [for leaving me].
Katika utetezi wangu wa mara ya kwanza, hakuna hata mmoja aliyeniunga mkono, bali kila mmoja aliniacha. Namwomba Mungu wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
17 Nevertheless, the Lord was with me and strengthened me. He enabled me to fully preach the message, and all the non-Jewish people [in the court] (OR, people from many nations) heard it. And I was rescued [by the Lord] {[the Lord] rescued me} [from great danger, as if I were taken] [MET] out of a lion’s (OR, wild animal’s) mouth.
Lakini Bwana alisimama upande wangu akanitia nguvu, ili kupitia kwangu lile Neno lihubiriwe kwa ukamilifu, watu wote Mataifa wapate kulisikia. Mimi niliokolewa kutoka kinywa cha simba.
18 [Therefore, I am sure that] the Lord will rescue me from everything that is truly evil and will bring me safely to heaven, where he rules. Praise him forever! (Amen!/May it be so!) (aiōn )
Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
19 Greet [for me] Priscilla and [her husband] Aquila and the family of Onesiphorus.
Wasalimu Prisila na Akila, na wote wa nyumbani kwa Onesiforo.
20 Erastus stayed in Corinth [city]. Trophimus, I left in Miletus [city] because he was sick.
Erasto alibaki Korintho. Nami nikamwacha Trofimo huko Mileto akiwa mgonjwa.
21 (Do your best/Try hard) to come to me before (the stormy season/winter). Eubulus, Pudens, Linus, Claudia, and many other fellow believers [in this city] (send their greetings to/say that they are thinking affectionately about) you.
Jitahidi ufike huku kabla ya majira ya baridi. Eubulo anakusalimu, vivyo hivyo Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.
22 [I pray that] the Lord will [help you in] your spirit, [Timothy, and] that [he] will act kindly toward all of you [believers who are there].
Bwana awe pamoja na roho yako. Neema iwe pamoja nanyi. Amen.