< 2 Samuel 6 >

1 Then David chose 30,000 Israeli men and gathered them together.
Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
2 He led them to the place in Judah [formerly] called Baalah, [now called Kiriath-Jearim]. They went in order to bring from there [to Jerusalem] the sacred chest, which had the name of Yahweh, the leader of the armies of [the angels in] heaven, written on it, and which had the [statues of the] winged creatures on top of it. Between those statues was where Yahweh spoke messages about ruling his people [MTY].
Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
3 The sacred chest was in the house of Abinadab, on top of a hill. They went there, and they put the chest on a new cart. Uzzah and Ahio, the two sons of Abinadab, were guiding [the oxen that were pulling the cart].
Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
4 Uzzah walked alongside the cart, and Ahio walked in front of it.
likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
5 David and all the Israeli men were celebrating in God’s presence, singing with all their strength and [playing] lyres and harps, and beating tambourines, and clashing castanets and cymbals.
Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
6 But when they came to the place where Nacon threshed grain, the oxen stumbled. So Uzzah put his hand on the sacred chest to (steady it/prevent it from falling [off the cart]).
Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
7 Yahweh immediately became very angry with Uzzah, and he killed him right there alongside the sacred chest, because he had touched the chest, [and Yahweh had commanded that only the descendants of Levi who help the priests should touch the sacred chest].
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
8 David was angry because Yahweh had punished Uzzah. So ever since that time, that place has been called ‘The Punishment of Uzzah’.
Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
9 David was [also] afraid of [what else] Yahweh [would do to punish them], so he said, “(How can I take the sacred chest with me [to Jerusalem]?/I am afraid to take the sacred chest with me [to Jerusalem].)” [RHQ]
Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
10 So he did not want to take the sacred chest to Jerusalem. Instead, they took it to another place; they took it to the house of Obed-Edom, from Gath [city].
Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
11 They left the sacred chest in the house of Obed-Edom for three months, and [during that time] Yahweh blessed Obed-Edom and his family.
Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
12 Later, people told David, “Yahweh has blessed Obed-Edom and his family because [he is taking care] of the sacred chest!” When David heard that, he [and some other men] went to Obed-Edom’s house, and very joyfully brought the sacred chest from there to Jerusalem.
Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
13 [This time, descendants of Levi] were carrying the sacred chest, but when they had walked only six steps, they stopped, and there David killed a bull and a fat calf, and offered them to Yahweh for a sacrifice.
Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
14 David was wearing [only] a linen cloth wrapped around his waist, and was dancing very energetically to honor Yahweh.
Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
15 David and the Israeli men took the sacred chest up [to Jerusalem], shouting [loudly] and blowing trumpets.
wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
16 While they were carrying the sacred chest into the city, [David’s wife] Michal, who was Saul’s daughter, looked out the window [of her house]. She saw King David leaping and dancing to honor Yahweh. So she was disgusted with him.
Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
17 They brought the sacred chest into the tent that David had erected for it. Then David gave to Yahweh offerings to be completely burned [on an altar], and other offerings to maintain fellowship with Yahweh.
Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
18 When David had finished offering those sacrifices, he asked Yahweh, the Commander of the armies [of the angels], to bless the people.
Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
19 He also distributed food to all the people. To each Israeli man and woman he gave a loaf of bread, some meat, and a raisin cake. Then all the people returned to their homes.
Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
20 When David went home to [ask Yahweh to] bless his family, his wife Michal came out to meet him. She said to him, “Maybe you, the king of Israel, [think that you] [IRO] were honoring yourself today, but really, you acted like a fool, uncovering yourself while the female servants of your officials were watching!”
Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
21 David replied to Michal, “[I was doing that] to honor Yahweh, who chose me instead of your father and other members of his family, to be the king of the Israeli people, the people who belong to Yahweh. And I will [continue to] dance to honor Yahweh!
Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
22 [Even though you think that what I did] was disgraceful, I will continue to do it even more. You may despise me [because of what I did], but the women whom you were talking about will honor me!”
Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
23 [As a result, ] Saul’s daughter Michal never gave birth to any children.
Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.

< 2 Samuel 6 >