< 2 Samuel 13 >

1 David’s son Absalom had a beautiful sister named Tamar. Another of David’s sons, Amnon, was attracted to Tamar.
Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
2 He wanted [to have sex with] [EUP] his half-sister very much, with the result that he made himself sick [thinking about her all the time]. But it was not possible for Amnon to get her, because she was a virgin, [so they kept men away from her].
Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
3 But Amnon had a friend named Jonadab, who was the son of David’s brother Shimeah. Jonadab was a very crafty/shrewd man.
Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
4 [One day] Jonadab said to Amnon, “You are the king’s son, but every day I see that [RHQ] you seem very depressed/sad. What is your problem?” Amnon replied, “I (am in love/want to sleep) [EUP] with Tamar, my half-brother Absalom’s sister.”
Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
5 Jonadab said to him, “Lie down on your bed, and pretend that you are sick. When your father comes to see you, say to him, ‘Allow my half-sister Tamar to come and give me some food to eat. She can prepare the food while I am watching her. Then she can serve it to me herself.’”
Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
6 So Amnon lay down, and pretended that he was sick. When the king came to see him, Amnon said to him, “[I am sick; ] please allow my half-sister Tamar to come and make a couple scones/dumplings for me while I am watching, and then she can serve them to me.”
Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
7 So David sent a message to Tamar in the palace, saying “Amnon [is sick and he wants you to] go to his house and prepare some food for him.”
Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
8 So Tamar went to Amnon’s house, where he was lying in bed. She took some dough and kneaded it, and formed it into some scones/dumplings while he was watching her. Then she baked them.
Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
9 She took them out of the pan and put them [on a plate] in front of him, but he refused to eat them. Then he said to everyone else in the room, “All the rest of you, leave me now!” So all the others left his [room].
Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
10 Then Amnon said to Tamar, “Bring the food into my room and serve it to me.” So Tamar took into his room the scones/dumplings that she had made.
Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
11 But when she brought them close for him to eat them, he grabbed her and said to her, “Come to bed with me!”
Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
12 She replied, “No, do not force me to do such a disgraceful thing! We never do things like that in Israel! That would be awful/terrible!
Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
13 As for me, if I did that, I would not be able to [RHQ] endure being disgraced by having done that. And as for you, everyone in Israel would condemn you for having done such a disgraceful deed. So I plead with you, talk to the king. I am sure that he will allow me to marry you.”
Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
14 But he would not listen to her. He was stronger than she was, so he forced her to have sex with him.
Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
15 Then Amnon hated her very much. He hated her much more than he had desired her. He said to her, “Get up and get out of here!”
Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
16 But she said to him, “No! It would be very wrong for you to send me away. It would be worse than what you just did to me!” But he would not listen to her.
Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
17 He summoned his personal servant and said to him, “Take this woman outside, away from me, and lock the door [so that she cannot come in again]!”
Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
18 So the servant put her outside and locked the door. Tamar was wearing a long robe with long sleeves, which was the clothing that was usually worn by the unmarried daughters of the king at that time.
Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
19 But Tamar tore the long robe that she was wearing, and put ashes on her head [to show that she was very sad]. Then she put her hands on her head [to show that she was grieving], and she went away, crying.
Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
20 Her brother Absalom [saw her and] said to her, “Has your half-brother Amnon [DOU] forced you to have sex with him [EUP]? Please, my sister, do not tell anyone, and do not become depressed/sad.” So Tamar went to live in Absalom’s house, and she was very sad and lonely.
Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
21 When King David heard about all that, he became very angry.
Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
22 And Absalom hated Amnon, because he had raped his sister, so he would not speak to Amnon about anything.
Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
23 Two years later, Absalom’s servants were shearing sheep at Baal-Hazor, which is near [a town named] Ephraim. [When they finished shearing the sheep, they celebrated], and Absalom invited all the king’s sons [to come and celebrate].
Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
24 Absalom went to the king and said to him, “Sir, my servants have been shearing my sheep. Please come with your officials [to celebrate] with us!”
Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
25 But the king replied, “No, my son, it would not be good for all of us to go, because it would cause you to do a lot of work and spend a lot of money for food.” Absalom continued urging him, but the king would not go. Instead, he said that he hoped/desired that God would bless them [while they celebrated].
Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
26 Then Absalom said, “If you will not go, please allow my half-brother Amnon to go with us.” But the king replied, “Why [do you want] him to go with you?”
Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
27 But Absalom continued to insist, so finally the king permitted Amnon and all David’s other sons to go with Absalom.
Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
28 [So they all went. And at the celebration], Absalom commanded his servants, “Notice when Amnon has become a bit drunk from the wine. Then when I signal to you, kill him. Do not be afraid; you will be doing this [only] because I told you [RHQ] to do it. So be courageous and do it!”
Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
29 So Absalom’s servants did what Absalom told them to do. [They killed Amnon]. All the rest of David’s sons [saw what happened and] fled, riding on their mules.
Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
30 While they were on their way home, someone [went quickly and] reported to David, “Absalom has killed all of your other sons; none of them is still alive!”
Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
31 The king stood up, tore his clothes [because he was extremely sad], and then he threw himself down on the ground. All the servants who were there also tore their clothes.
Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
32 But Jonadab, the son of David’s brother Shimeah, said, “Your Majesty, [I am sure that] they have not killed all your sons. [I am sure that] only Amnon is dead, because Absalom has determined to do this ever since the day that Amnon raped [EUP] his half-sister Tamar.
Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
33 So, your majesty, do not believe the report that all your sons are dead. [I am sure that] only Amnon is dead.”
Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
34 In the meantime, Absalom ran away. Just then, the soldier/sentry [who was standing on the city wall] saw a large crowd of people coming down the hill along the road from Horonaim. [He ran and told the king what he had seen].
Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
35 Jonadab said to the king, “Aha! What I told you is true. Your other sons [are alive and] have come!”
Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
36 And as soon as he said that, David’s sons came in. They all started crying, and David and all his officials also cried very much.
Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
37 But Absalom had fled. He went to stay with the king of [the] Geshur [region], who was Talmai the son of Ammihud. Absalom stayed there for three years. David mourned for his son Amnon for a long time,
Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
39 but after that, he desired very much to see Absalom, because he was no longer grieving about Amnon being dead.
Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.

< 2 Samuel 13 >