< 2 Samuel 10 >

1 Some time later, the king of the Ammon people-group died, and his son Hanun became their king.
Baada ya muda, mfalme wa Waamoni akafa, naye Hanuni mwanawe akaingia mahali pake.
2 David thought, “Nahash was kind to me, so I will be kind to his son.” So David sent some officials there, to tell Hanun that David was sorry that Hanun’s father [had died]. When those messengers arrived in the land where the Ammon people-group lived,
Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kama vile baba yake alivyonitendea mimi wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kuonyesha wema wake kwa Hanuni kuhusu baba yake. Watu wa Daudi walipofika katika nchi ya Waamoni,
3 the leaders of the Ammon people-group said to Hanun, “Do you think that it is to honor your father that King David has sent these men to say that he is sorry that your father died [RHQ]? [We think that] he has sent them here to look around the city to determine how his [army] can conquer us!”
wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kukutumia watu ili kuonyesha masikitiko? Je, Daudi hakuwatuma watu hawa kuchunguza na kuupeleleza mji ili kuupindua?”
4 Hanun [believed what they said; so he commanded some soldiers to] seize David’s officials and [insult them by] shaving off one side of each man’s beard, and [by] cutting off the lower part of their robes, [with the result that their buttocks could be seen], and then they sent them away.
Basi Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa kila mmoja ndevu zake nusu, akakata mavazi yao nyuma katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
5 The men were very humiliated/ashamed, [so they did not want to return home]. When David found out about what had happened to his officials, he sent someone to tell them, “Stay at Jericho until your beards have grown again, and then return home.”
Daudi alipoambiwa jambo hili, akatuma wajumbe ili kwenda kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote ndipo mje.”
6 Then [the leaders of] the Ammon people-group realized that they had greatly insulted [IDM] David [IDM]. So they sent some men to hire/pay some soldiers [from other nearby areas to help defend them]. They hired 20,000 soldiers from [the] Beth-Rehob and Zobah [regions northeast of Israel], and 12,000 soldiers from [the] Tob [region], and 1,000 soldiers from [the army of] the king of Maacah [region].
Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, wakaajiri askari wa miguu 20,000 Waaramu kutoka Beth-Rehobu na Soba, pia mfalme wa Maaka pamoja na watu 1,000, na vilevile watu 12,000 kutoka Tobu.
7 When David heard about that, he sent Joab with all of the army [that Joab commanded], to fight against them.
Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
8 The soldiers of the Ammon people-group marched out and (stood in their positions/arranged themselves for battle) at the entrance [to their capital city, Rabbah]. The other soldiers from Syria and Tob and Maacah stood by themselves (in their positions/arranged themselves for battle) in the nearby fields.
Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati Waaramu wa Soba, wa Rehobu, watu wa Tobu na Maaka walikuwa peke yao kwenye eneo la wazi.
9 Joab saw that there were groups of enemy soldiers in front of his troops and behind his troops. So he chose some of the best Israeli soldiers, and put them in positions to fight against the soldiers of Syria.
Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
10 He appointed his [older] brother Abishai to be the commander of all the other soldiers, and he told them to (stand in their positions/arrange themselves) in front of [the army of] the Ammon people-group.
Akawaweka waliobaki chini ya uongozi wa Abishai nduguye na kuwapanga dhidi ya Waamoni.
11 Then Joab said, “If the soldiers from Syria are too strong for us to defeat them, your men must come and help us. But if the soldiers from the Ammon people-group are too strong for you to defeat, we will come and help your men.
Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itawabidi mje kunisaidia. Lakini kama Waamoni watawazidi nguvu, basi nitakuja kuwasaidia.
12 We must be strong, and fight hard [IDM] to [defend] our people and the cities [(that belong to/where we worship)] our God. I will pray/request that Yahweh do what he considers to be good.”
Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
13 So Joab and his army [advanced to] attack the army of Syria, and the soldiers from Syria ran away from them.
Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
14 And when [the soldiers of] the Ammon people-group saw that the soldiers from Syria were running away, they also started to run away from Abishai and his army, and they retreated back inside the city. So Joab’s [army] stopped fighting against [the army of] the Ammon people-group, and Joab [and his army] returned to Jerusalem.
Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao wakakimbia mbele ya Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi kutoka kupigana na Waamoni na kufika Yerusalemu.
15 After [the leaders of] the army of Syria saw that the Israeli army had defeated them, they gathered all their troops together.
Baada ya Waaramu kuona wameshindwa na Israeli, wakajikusanya tena.
16 [Their king, ] Hadadezer, summoned the soldiers of Syria who lived on the east side of the [Euphrates] River. They gathered at Helam [city]. Their commander was Shobach.
Hadadezeri akaagiza Waaramu walioletwa kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakaenda Helamu pamoja na Shobaki jemadari wa jeshi la Hadadezeri akiwaongoza.
17 When David heard about that, he gathered all the Israeli soldiers, and they crossed the Jordan [River] and marched to Helam. There, the army of Syria (took their positions/arranged themselves for battle), and the battle started.
Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote, wakavuka Mto Yordani, wakaenda Helamu. Waaramu wakapanga vikosi vyao vya askari kukabiliana na kupigana dhidi ya Daudi.
18 But the soldiers of Syria ran away from the Israeli soldiers. David [and his army] killed 700 of their chariot-drivers and 40,000 other soldiers. They also wounded Shobach, their commander, and he died there.
Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari mia saba na askari wao wa miguu 40,000. Vilevile alimpiga Shobaki jemadari wa jeshi lao, naye akafa huko.
19 When all the kings who had been ruled by Hadadezer realized that they had been defeated by the Israeli [army], they made peace with the Israelis and agreed to accept David as their king. So [the army of] Syria was afraid to help [the army of] the Ammon people-group any more.
Wafalme wote waliokuwa wanamtumikia Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya amani na Waisraeli na wakawa chini yao. Hivyo Waaramu wakaogopa kuwasaidia Waamoni tena.

< 2 Samuel 10 >