< 2 Kings 9 >

1 Meanwhile, the prophet Elisha summoned one of the other prophets. He said to him, “Get ready [IDM] and go to Ramoth [city] in [the] Gilead [region]. Take this jar of [olive] oil with you.
Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
2 When you arrive there, search for a man named Jehu, the son of Jehoshaphat and grandson of Nimshi. Go with him into a room away from his companions,
Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
3 and pour [some of] this oil on his head. Then say to him, ‘Yahweh declares that he is appointing you to be the king of Israel.’ Then open the door and run away as quickly as you can.”
Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
4 So the young prophet went to Ramoth.
Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
5 When he arrived, he saw that the commanders of the army were having a conference. He [looked at Jehu and] said, “Sir, I have a message for [one of] you.” Jehu replied, “Which one of us is the message for?” The young prophet replied, “It is for you, commander/sir.”
Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
6 So Jehu got up and went with the young prophet into a house. There the young prophet poured some [olive] oil on Jehu’s head and said to him, “Yahweh, the God whom we Israelis [worship], declares this: ‘I am appointing you to be the king of my Israeli people.
Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
7 You must kill your master [King Joram], the son of Ahab, because I want to punish [Ahab’s wife] Jezebel for murdering [MTY] many of my prophets and other people who served me.
Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
8 You must kill [not only Joram but] all of Ahab’s family. I want to get rid of every male in the family, including young ones and old ones.
Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
9 I will get rid of Ahab’s family, like I got rid of the families of two other kings of Israel, Jeroboam and Baasha.
Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
10 And [when] Jezebel [dies], her corpse will not be buried. Dogs will eat her corpse there in Jezreel [city].’” After the young prophet said this, he left the room and ran.
Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
11 When Jehu came out of the room to where his other commanders were, they said to him, “Is everything all right? Why did that mad fellow come to you?” He replied, “You know what kinds of things young prophets like him say.”
Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
12 They said, “You are lying! Tell us what he said!” He replied, “He told me that Yahweh said, ‘I am appointing [MTY] you to be the king of Israel.’”
Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
13 Then they all spread their cloaks on the steps of the building [for Jehu to walk out on], and they blew trumpets and shouted, “Jehu is now the king!”
Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
14 King Joram and his army had been defending Ramoth against the attacks by the army of the king of Syria. King Joram had returned to Jezreel [city], to recover from being wounded in the battle against the army of Hazael, the king of Syria. And Jehu made plans to kill Joram. He said to his other commanders, “If helping me is truly what you want, make sure that no one leaves this city to go to warn the people of Jezreel [about what I am planning to do].”
Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
16 Then Jehu and his officers got into their chariots and rode to Jezreel, where Joram was still recovering. And King Ahaziah of Judah was there, visiting Joram.
Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
17 A guard was standing in the watchtower in Jezreel. He saw Jehu and his men approaching. He called out, “I see a lot of men [who are approaching]!” King Joram [heard what the watchman said, so he] said to his soldiers, “Send someone on a horse to go and find out if they are coming to be friendly to us or to attack us.”
Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
18 So a man rode out to meet Jehu and said to him, “The king wants to know [if you are coming to be] friendly to us.” Jehu replied, “This is not the time for you [RHQ] to be concerned about acting friendly! Turn around and come behind me!” So the guard in the watchtower reported that the messenger had reached the group [that was approaching], but that he was not returning [alone].
Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
19 So King Joram sent another messenger, who asked Jehu the same question. Again Jehu replied, “This is not the time [RHQ] for you to be concerned about acting friendly! Turn around and follow me!”
Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
20 Then the watchman reported again, “That messenger also reached them, but he is not coming back [alone]. And [the leader of the group must be] Jehu, the son of Nimshi, because he is driving [his chariot] furiously, [like Jehu does]!”
Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
21 Joram said [to his soldiers], “Get [my chariot] ready!” So they did that. Then King Joram and King Ahaziah both rode toward Jehu, each one in his own chariot. And [it happened that] they met Jehu at the field that had previously belonged to Naboth!
Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
22 When Joram met Jehu, he said to him, “Are you coming on a peaceful visit?” Jehu replied, “(How can there be peace while you and your people are prostrating themselves to worship idols and practicing very much (witchcraft/sorcery) like your mother Jezebel did?/There certainly cannot be peace while you and your people are prostrating themselves to worship idols and practicing (witchcraft/sorcery) like your mother Jezebel has been doing!)” [RHQ]
Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
23 Joram cried out, “Ahaziah, they have deceived us! [They want to kill us]!” So Joram turned his chariot around and tried to flee.
Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
24 But Jehu drew his bow mightily and shot [an arrow that pierced] Joram between his shoulder blades. The arrow [went through his body and] pierced his heart, and he slumped down dead in his chariot.
Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
25 Then Jehu said to his assistant Bidkar, “Take his corpse and throw it here into the field that belonged to Naboth. [I am sure that] you remember that when you and I were riding together [in chariots] behind King Joram’s father Ahab, that Yahweh said this about Ahab:
Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
26 ‘Yesterday I saw Ahab murder [MTY] Naboth and his sons here. And I solemnly promise that I will punish him right here in this same field!’ So take Joram’s corpse and throw it into that field! That will fulfill what Yahweh said would happen.”
Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
27 When King Ahaziah saw what happened, he fled [in his chariot] toward Beth-Haggan [town]. But Jehu pursued him and said [to his other commanders], “Shoot him, also!” So they shot him [with arrows] while he was riding in his chariot on the road up to Gur, near Ibleam [town]. He continued going in his chariot until he reached Megiddo [city], where he died.
Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
28 His officials took his corpse back to Jerusalem and buried it in the tombs in the [part of Jerusalem called] ‘The City of David’, where his ancestors had been buried.
Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
29 Ahaziah had become the king of Judah when Joram had been ruling Israel for almost eleven years.
Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
30 Then Jehu went to Jezreel. When [Ahab’s widow] Jezebel heard what had happened, she put paint/makeup on her eyelids, and combed her hair to make it beautiful, and looked out the window [of the palace toward the street below].
Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
31 While Jehu was entering the city gate, she called out to him, “You [are like] Zimri! You are a murderer! [I think] you are certainly not [RHQ] coming on a peaceful visit!”
Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
32 Jehu looked up toward the window, and then he said, “Who is (on my side/wants to help me)? Anyone?” Two or three palace officials looked down at him [from a window and pointed to themselves].
Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
33 Jehu said to them, “Throw her down here!” So they threw her down, and [when she hit the ground and died], some of her blood splattered on the city wall and on the horses [that were pulling the chariots].
Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
34 Then Jehu went into the palace and ate and drank. Then he said [to some of his men], “Take the corpse of that women whom Yahweh has cursed and bury it, because she is a king’s daughter [and therefore should be buried properly].”
Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
35 But when they went to get her corpse to bury it, all that was left was only her skull and [the bones of] her feet and her hands. Everything else was gone.
Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
36 When they reported this to Jehu, he said, “That is what Yahweh said would happen! He told his servant/prophet Elijah, ‘In [the city of] Jezreel, dogs will eat the flesh of Jezebel’s corpse.
Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
37 Her bones will be scattered there in Jezreel like dung, with the result that no one will be able to [recognize them and] say, “These are Jezebel’s bones.”’”
na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””

< 2 Kings 9 >