< 2 Kings 17 >

1 Elah’s son Hoshea began to rule Israel after King Ahaz had ruled Judah for twelve years. Hoshea ruled in Samaria for nine years.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
2 He did many things that Yahweh considered to be evil, but he did not do as many evil things as the previous kings of Israel had done.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
3 [The army of] King Shalmaneser of Assyria attacked and defeated [the army of] King Hoshea. As a result, the Israelis were forced to pay a lot of tribute/taxes to Assyria each year.
Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
4 But several years later, Hoshea secretly planned to rebel against the rulers of Assyria. He sent messengers to So/Osorkon, the king of Egypt, [asking if his army could help the Israelis fight against the army of Assyria]. Hoshea also stopped paying the tribute/taxes that he had been paying to Assyria every year. But the king of Assyria found out about those things, so he told his officers to put Hoshea in prison.
Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
5 Then he [brought the army of] Assyria to Israel, and they attacked everywhere in that land. His army surrounded Samaria [city] for three years.
Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
6 Finally, after King Hoshea had been ruling Israel for nine years, the army of Assyria [MTY] [forcefully entered] the city [and] captured [the people]. They took the Israeli people to Assyria and forced some of them to live in Halah [town]. They forced others to live near the Habor River in Gozan district. They forced others to live in the towns where the Mede people-group lived.
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
7 Those things happened because the Israeli people had sinned against Yahweh their God. He had rescued their [ancestors] from the power [MTY] of the king of Egypt and brought them [safely] out of Egypt, but later they began to worship other gods.
Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
8 They imitated the things that the heathen/pagan people-groups did. Those were the groups that Yahweh had expelled as the Israelis occupied their land. The Israeli people also did the evil things that the kings of Israel (introduced/showed to them).
na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
9 The Israeli people also secretly did many things that were not pleasing to Yahweh their God. They built shrines [to worship idols] in all their cities, including small towns and big cities with walls around them.
Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
10 They set up stone pillars [to honor gods], and poles [to worship the goddess] Asherah at the top of every high hill and under every [big] tree.
Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
11 The Israelis burned incense in every place where they worshiped those gods, just like the people-groups who lived there previously had done—the groups that Yahweh had expelled from the land. The Israelis did many wicked things that caused Yahweh to become angry.
Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
12 Yahweh warned them many times that they should not worship idols, but they did it anyway.
Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
13 Yahweh frequently sent his prophets and (seers/those who saw visions from Yahweh) to warn the people of Israel and the people of Judah. The message that Yahweh gave them was, “Turn away from all your evil behavior. Obey my commands and my laws, the laws that I told your ancestors [to obey] and which I told the prophets who served me to tell to you [again].”
Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
14 But the Israeli people would not pay attention. They were stubborn [IDM] just like their ancestors were. Just like their ancestors did, they refused to believe in Yahweh their God.
Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
15 They rejected Yahweh’s laws and the agreement that he had made with their ancestors. They ignored Yahweh’s warnings. They worshiped worthless idols and as a result they themselves became worthless. Although Yahweh had commanded them not to imitate the evil behavior of the people-groups that lived near them, they disobeyed that command.
Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
16 The Israeli people disobeyed all of Yahweh’s commands. They made two metal calves [to worship]. They set up two poles [to worship the goddess] Asherah, and they worshiped [the god] Baal, and the sun, the moon, and the stars.
Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
17 They also burned their own sons and daughters to be sacrifices [to those gods]. They went to fortune-tellers and they practiced sorcery. They continually chose [MET] to do [all kinds of] evil things that caused Yahweh to become angry.
Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
18 So, because Yahweh was very angry with the Israeli people, he allowed [their enemies] to take them away [from their country]. Only the people of the tribe of Judah were left [in the land].
Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
19 But even the people of Judah did not obey the commands of Yahweh their God. They imitated the evil customs that the Israelis had introduced.
na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
20 So Yahweh rejected all the people of Israel and of Judah. He punished them by allowing the armies of other nations to defeat them [and take them away]. He got rid of all of them.
Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
21 Earlier, when Yahweh allowed the people of Israel to separate/break away from the area [MTY] that King David [had estabished], they chose Jeroboam, the son of Nebat, to be their king. Then Jeroboam enticed the people of Israel to stop worshiping Yahweh [and to worship idols instead]. He led them to commit great sins.
Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
22 And the Israeli people continued to do the evil things that Jeroboam introduced. They did not turn away from those sins,
Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
23 until finally Yahweh got rid of them. That was just what his prophets had warned would happen. The Israeli people were taken away to the land of Assyria, and they still remain there.
hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
24 The king of Assyria [ordered his soldiers to] take [groups of] people from Babylon, Cuthah, Avva, Hamath, and Sepharvaim [cities] to [the] Samaria [region], and to resettle them in the towns there, to take the place of the Israelis [who lived there previously]. Those people took control over [the whole] Samaria [region] and lived in the towns there.
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
25 But those people [who came from other countries] did not worship Yahweh when they first arrived in Samaria. So Yahweh sent lions to kill some of them.
Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
26 Then those people sent a message to the king of Assyria. They wrote, “We people who have resettled in the towns in Samaria do not know how to worship the God [that the Israelis worshiped] in this land. So he has sent lions among us to kill us, because we have not worshiped him correctly.”
Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
27 [When] the king of Assyria [read this letter, he] commanded [his officers], “You brought many priests here from Samaria. Send one of them back there. Tell him to teach the people who are now living there how to worship correctly the God whom the Israelis worshiped in that land.”
Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
28 So [the officers did that]. They sent one of the Israeli priests back to Samaria. That priest went to live in Bethel [city], and he taught the people there how to worship Yahweh.
Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
29 But the people [who returned from Babylon and started to live in Samaria and] continued to make their own idols. They placed them in the shrines that the Israelis had built there. The people of each people-group made idols in the cities in which they were living.
Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
30 The people from Babylon made idols to represent their god Succoth-Benoth. The people from Cuthah made idols to represent their god Nergal. The people from Hamath made idols to represent their god Ashima.
Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
31 The people of Avva made idols to represent their gods Nibhaz and Tartak. The people from Sepharvaim sacrificed their own children. They completely burned them [in pits where hot fires were kept burning, ] as offerings to their gods Adrammelech and Anammelech.
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
32 But those people also worshiped Yahweh, and they appointed from among their own groups many people to be priests at the shrines on the tops of the hills, in order that those priests could offer sacrifices for them there.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
33 So they revered Yahweh, but they also worshiped their own gods, just as the people living in the countries from which they had been taken to Samaria did.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
34 They still keep their old customs. They really do not worship Yahweh, and they do not obey all the laws and commands that Yahweh gave to the descendants of Jacob, to whom he gave the new name Israel.
Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
35 Yahweh had previously made an agreement with their ancestors, commanding them not to worship other gods or bow down to honor them or do other things to please them or offer sacrifices to them.
Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
36 He had said to them, “You must have an awesome respect for me, Yahweh, the one who brought you out of Egypt with my very great power [DOU]. I am the one whom you must bow down to honor, and I am the one to whom you must offer sacrifices.
Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
37 You must always obey the laws and commands that I [told Moses to] write for you. You must not worship other gods.
Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
38 And you must not forget the agreement that I made with your ancestors. You must not revere other gods.
Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
39 Instead, you must revere me, Yahweh, your God. If you do that, I will rescue you from the power [MTY] of all your enemies.”
Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
40 But the people [from those foreign nations] would not heed what Yahweh said. Instead, they continued to adhere to their old customs.
Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
41 So, they worshiped Yahweh, but they also worshiped their idols. And their descendants still do the same thing.
Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.

< 2 Kings 17 >