< 2 Kings 10 >
1 There were seventy descendants of King Ahab who were living there in Samaria. Jehu wrote a letter [and made copies of it] and sent them to the rulers of the city, to the elders, and to those who raised and tutored Ahab’s children.
Basi Ahabu alikuwa na watoto sabini katika Samaria. Yehu akaandika barua na kuzituma kwenda Samaria, kwa watawala wa Yezreeli, pamoja na wazee na walinzi wa wana wa Ahabu akisema,
2 [This is what he wrote]: “You are the ones who are [taking care of] the king’s descendants. You have chariots and horses and weapons, and you live in cities that have walls around them. So as soon as you receive this letter,
“Wana wa bwana wako wako pamoja na wewe, na wewe pia una magari ya farasi na farasi na kuimarisha mji dhidi ya maadui na silaha. Hivyo basi, haraka iwezekanavyo barua hii ikufikiapo,
3 choose one of the king’s sons, the one who is the best qualified, and appoint him to be your king. Then [prepare to] fight to defend him.”
mchagueni aliye bora na anayestahili miongoni mwa mtoto wa bwana wenu na kumuweka kwenye kiti cha kifalme cha baba yake, na kupigania ufalme wa bwana wenu.”
4 But [when they got those letters from Jehu and read them], they became very afraid. They said, “King Joram and King Ahaziah could not resist him; (how can we resist him?/we cannot possibly resist him!)” [RHQ]
Lakini waliogopa na kusema miongoni mwao, “Tazama, wafalme wawili hawatasimama mbele ya Yehu. Hivyo tutasimamaje?”
5 So the officer who was in charge of the palace and the mayor of the city sent a message to Jehu saying, “We want to serve you, and we are ready to do whatever you tell us to do. We will not appoint anyone to become our king. You do whatever you think is best.”
Kisha yule mtu ambaye alikuwa kiongozi kwenye nyumba ya mfalme, na wale waliowalea watoto, wakatuma ujumbe kwa Yehu, kusema, “Sisi ni watumishi wako. Tutafanya chochote utakacho tuamuru. Hatutamfanya mtu yeyote kuwa mfalme. Fanya lile lililojema machoni pako.”
6 So Jehu sent a second letter to them, writing this: “If you (are on my side/want to help me), and if you are ready to obey me, [kill] King Ahab’s descendants [and cut off their heads and] bring their heads to me here in Jezreel at this time tomorrow.” The seventy descendants of King Ahab were being brought up and supervised by the leaders of [Samaria] city.
Kisha Yehu akaandika barua mara ya pili, akisema, “Kama mko upande wangu, na kama mtasikiliza sauti yangu, mtachukua vichwa vya watu wa wana wa mabwana wenu, na mje kwangu Yezreeli kesho mda kama huu.” Ndipo wana wa wafalme, sabini kwa hesabu, waliokuwa watu muhimu huko mjini, ambao walikuwa wakiwaleta.
7 When they received the letter from Jehu, they killed all seventy of Ahab’s descendants and [cut off their heads]. They put their heads in baskets and sent them to Jehu at Jezreel.
Hivyo barua ilipokuja kwao, waliwachukua wana wa wafalme na kisha kuwaua, watu sabini, wakaweka vichwa vyao kwenye vikapu, na kuivituma kwa Yehu katika Yezreeli.
8 A messenger came to Jehu and told him, “They have brought the heads of Ahab’s descendants.” So Jehu commanded that the heads should be put in two piles at the city gate and that the heads should stay there until the next morning.
Mjumbe mmoja akaja kwa Yehu, akisema, “Wamevileta vile vichwa vya watoto wa wafalme.” Hivyo akasema, viwekeni kwenye mafungu mawili kwenye lango hadi asubuhi.”
9 The next morning he went out [to the city gate] and said to all the people, “I am the one who plotted against King Joram and killed him. You are not guilty of doing that. But [it was Yahweh, not I] [RHQ] who [commanded that] all these [descendants of Ahab should be] killed.
Asubuhi Yehu akatoka nje na kusimama, na kusema kwa watu wote, “Ninyi hamna hatia. Tazameni, nimefanya fitina dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua hawa wote?
10 So you need to know that everything that Yahweh said would happen has happened. He has caused to happen what he told the prophet Elijah would happen.”
Sasa hakika tafakarini kwamba hakuna sehemu ya neno la Yahwe, lile alilonena Yahwe kuhusu familia ya Ahabu, itaanguka kwenye aridhini, kwa kuwa Yahwe amefanya kile alichokiongea kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 Then Jehu executed all the other relatives of Ahab in Jezreel, and all Ahab’s officers, and close friends, and his priests. He did not allow any of them to remain alive.
Basi Yehu akawaua wote waliokuwa wamebakia wa familia ya Ahabu katika Yezreeli, na watu wake muhimu wote, marafiki zake wa karibu, na makuhani wake, hakuna hata mmoja wao alisalia.
12 Then Jehu left [Jezreel] and went toward Samaria. While he was going there, at a place called ‘Shepherds’ Camp’,
Kisha Yehu akainuka na kuondoka; akaenda Samaria. Kadiri alivyokuwa akikaribia Bethi Ekedi ya wachungaji,
13 he met some relatives of King Ahaziah of Judah. He asked them, “Who are you?” They replied, “We are relatives of King Ahaziah. We are going to Jezreel to visit the children of Queen Jezebel and the other members of King [Joram’s] family.”
akamlaki na ndugu wa Ahazia mfalme wa Yuda. Yehu akawaambia, “Ninyi ni akina nani?” Wakajibu, “Sisi ni ndugu zake na Ahazia, na tunashuka chini kuwasalimia watoto wa mfalme na watoto wa Malkia Yezebeli.”
14 Jehu said to his men, “Seize them!” So they seized them and killed all of them at the pit named Beth-Eked. There were 42 people whom they killed; they did not allow any of them to remain alive.
Yehu akawaambia watu wake mwenyewe, “Wachukue wakiwa hai.” Hivyo wakawachukua wakiwa hai na kuwaua kwenye kisima cha Bethi Ekedi, watu wote arobaini na mbili. Hakumwacha hata mmoja wao akiwa hai.
15 Then Jehu [continued to travel toward Samaria]. Along the road, he was met by Jonadab, a leader of the Rechab clan. Jehu greeted him and said to him, “Are you as devoted to me [IDM] as I am devoted to you?” Jonadab replied, “Yes, I am.” Jehu said, “If you are, shake hands with me.” So Jonadab shook hands with him, and Jehu helped him to get into his chariot.
Baada ya Yehu kuondoka huko, akakutana na Yehonadabu mwana wa Rekabu anakuja kukutana naye. Yehu akamsalimia na kisha akamwambia, “Je moyo wako uko na mimi, kama moyo wangu ulivyo pamoja na wako?” Yehonadabu akajibu, Ndio.” Yehu akasema, “kama ni ndio, nipatie mkono wako.” Kisha Yehonadabu akampatia mkono wake, na Yehu akampandisha Yehonadabu juu kwenye magari ya farasi pamoja naye.
16 Jehu said to him, “Come with me, and you will see that I am very devoted to Yahweh.” So they rode together to Samaria.
Yehu akasema, “Fuatana pamoja nami na uone wivu wangu kwa Yahwe.” Hivyo alikuwa na Yehonadabu akiendesha gari la farasi.
17 When they arrived in Samaria, Jehu killed all of Ahab’s relatives who were still alive. He did not (spare any of them/allow any of them to remain alive). That was what Yahweh told Elijah would happen.
Wakati alipokuja Samaria, Yehu akawaua wote waliobakia kutoka uzao wa Ahabu katika Samaria, hata akawaangamiza ukoo wa kifalme wa Ahabu, kama walivyokuwa wameambiwa kabla ya neno la Yahwe, ambalo aliloambiwa Eliya.
18 Then Jehu summoned all the people [of Samaria], and said to them, “King Ahab was devoted to [your god] Baal a little bit, but I will serve him much more.
Kisha Yehu akawakusanya watu wote akwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo, lakini Yehu atamtumikia sana.
19 So now summon all the prophets of Baal, all of Baal’s priests, and all the others who worship Baal. I am going to make a great sacrifice to Baal. I want all of them to be there. Any of them who is not there will be executed.” But Jehu was planning to trick them; he was planning to kill all those who worshiped Baal.
Basi niitieni manabii wote wa Baali, wote wamwabuduo, na makuhani wake wote. Asikosekane mtu hata mmoja, kwa kuwa nina dhabihu kubwa nataka kutoa kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataishi.” Lakini Yehu alifanya haya kwa udanganyifu, kwa dhamira ya kuwaua wanaomwabudu Baali.
20 Then Jehu commanded, “Announce that we are going to set aside a day to honor Baal.” So they did that.
Yehu akasema, “Tengeni mda tuwe na mkutano kwa ajili ya Baali.” Hivyo wakalitangaza.
21 Jehu [decided what day they would gather and] sent messages throughout Israel [telling everyone what day to gather on], and on that day, everyone who worshiped Baal came. No one stayed at home. They all went into the huge temple of Baal and filled it from one end to the other.
Kisha Yehu akatuma Israeli yote na wamwabuduo Baali waje, hivyo basi hakuna mtu hata mmoja ambaye aliacha kuja. Walikuja kwenye hekalu la Baali, na ilijaa kutoka mwanzo hadi mwisho.
22 Jehu told the priest who took care of the sacred robes to bring them out and give them to the people who worshiped Baal. So the priest did that.
Yehu akamwambia yule mtu aliyekuwa anatunza kabati la nguo za makuhani, “Uwatolee mavazi wote wamwabuduo Baali.” Basi yule mtu akawatolea nguo.
23 Then Jehu went into the temple of Baal with Jonadab, and he said to the people who were there to worship Baal, “Be sure that only those who worship Baal are here. Be sure that no one who worships Yahweh has come in.”
Basi Yehu akaingia pamoja na Yohonadabu mwana wa Rekabu kwenye nyumba ya Baali, na kisha akawaambia wanaomwabudu Baali, “Tafuteni na muhahakishe kwamba hakuna mtu hapa pamoja na ninyi kutoka watumishi wa Yahwe, lakini wamwabuduo Baali peke yao.”
24 Then he and Jonadab prepared to offer sacrifices and other offerings to Baal that would be completely burned [on the altar that was there in Samaria]. But Jehu had stationed eighty of his men outside the temple, and had said to them, “I want you to kill all the people [who are in the temple]. Anyone who allows one of them to escape will be executed!”
Kisha wakaenda kutoa dhabihu na sadaka ya kutekeza. Basi Yehu alichagua watu themanini ambao walikuwa wamesimama nje, na aliwaambia, Kama mtu yeyote miongoni mwa hawa watu ambao nimewaleta kwenye mikono yenu atoroke, yeyote atakayemwacha huyo mtu atoroke, maisha yake yatachukuliwa kwa ajili ya yule aliyeokoka.”
25 As soon as Jehu [and Jonadab] had finished killing the animals that would be completely burned to be an offering to Baal, they [went outside and] said to the guards and officers, “Go in and kill all of them! Do not allow any of them to escape!” So the guards and officers went in and killed them all with their swords. Then they dragged their corpses outside the temple. Then they went into the inner room of the temple,
Hivyo kisha baada ya mda mfupi Yehu alipomaliza kutoa sadaka ya kutekezwa, akamwambia mlinzi na manahodha, “Ingieni na muwaue. Msimwache mtu yeyote atoke.” Basi waliwaua kwa makali ya upanga, na mlinzi na manahodha wakawatupa nje na kwenda kwenye chumba cha ndani cha nyumba ya Baali.
26 and they carried out the sacred pillar of Baal that was there, and they burned it.
Wakazitoa nguzo za mawe ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Baali, na kisha kuzichoma.
27 So they destroyed that pillar that honored Baal, and then they burned down the temple, and made it a public toilet. And it is still a toilet!
Kisha wakazivunja zile nguzo za Baali, na kuiharibu nyumba ya Baali na kuifanya choo, ambacho kipo hadi leo.
28 That is how Jehu got rid of the worship of Baal in Israel.
Hivi ndivyo ambavyo Yehu alivyomharibu muabudu Baali kutoka Israeli.
29 But Jehu did not quit committing the kinds of sins that Jeroboam had committed, sins that led the people of Israel to sin by worshiping the gold [statues of] calves in Bethel and Dan [cities].
Lakini Yehu hakuacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo ilfanya Israeli kutenda dhambi-ambayo ni, kumwabudu ndama wa dhahabu katika Betheli na Dani.
30 Then Yahweh said to Jehu, “You have done what pleased me by getting rid of all of Ahab’s descendants. So I promise you that your son and grandson and great-grandson and great-great-grandson will all be kings of Israel.”
Hivyo Yahwe akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vema kwa kufanya yaliyo sahihi kwenye macho yangu, na kumailiza kwenye nyumba ya Ahabu kulingana na yote yaliyokuwa kwenye moyo wangu, uzao wako utakaa kwenye kiti cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 But Jehu did not obey all the laws of Yahweh, the God of the Israeli people. He did not stop committing the sins that Jeroboam had committed, sins that led the Israeli people to sin.
Lakini Yehu hakujali kutembea kwenye sheria ya Yahwe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakugeuka kutoka kwenye dhambi za Yeroboamu, ambayo iliwafanya Israeli kutende dhambi.
32 At that time, Yahweh began to cause the territory controlled by Israel to become smaller. [The army of] King Hazael [of Syria] conquered much of the Israeli territory.
Siku zile Yahwe akaanza kupunguza mikoa ya Israeli, na Hazaeli kuwashinda Waisraeli mipakani mwa Israeli,
33 He conquered the parts east of the Jordan [River], as far south as Aroer [town] on the Arnon [River]. That included [the] Gilead and Bashan [regions], where the tribes of Gad, Reuben, and half of the tribe of Manasseh lived.
kutoka Yordani upande wa mashariki, nchi yote ya Gileadi, Wagadi, na Wareubeni, na Wamanase, kutoka Aroeri, alipo karibu na bonde la Arnoni, kupita Geleadi hadi Bashani.
34 [If you want to read more] about all the other things that Jehu did [RHQ], they are written in the scroll called ‘The History of the Kings of Israel’.
Kama kwa mambo mengine yamhusuyo Yehu, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
35 Jehu died [EUP], and was buried in Samaria. His son Jehoahaz became the king in place of his father.
Yehu akalala na wazee wake, na walimzika katika Samaria. Kisha Yehoahazi mwanaye akawa mfalme katika sehemu yake.
36 Jehu had ruled in Samaria as the king of Israel for twenty-eight years.
Mda ambao Yehu alitawala juu ya Israeli katika Samaria ulikuwa miaka ishini na nane.