< 2 Chronicles 31 >
1 After the festival ended, the Israelis who were there went to all the towns in Judah and smashed the stones/pillars [for worshiping idols], and cut down the poles [for worshiping the goddess] Asherah. They destroyed the shrines on the hilltops and the altars [of Baal] throughout the areas where the tribes of Judah and Benjamin lived, and also in the areas of the tribes of Ephraim and Manasseh. After destroying all of them, they returned to their own towns.
Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
2 Hezekiah divided the priests and [other] descendants of Levi into groups. He appointed some of the groups to offer sacrifices that would be completely burned [on the altar] and offerings to maintain fellowship [with Yahweh]. He appointed some groups to do other work at the temple: some to lead the people in their worship, some to thank Yahweh, and some to sing songs to praise to Yahweh at the gates of the temple.
Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
3 The king contributed some of his own funds to buy animals that would be sacrificed in the morning and in the evening of each day, and on the Sabbath days, to celebrate the new moons, and during the other feasts, according to what was written in the laws [that Yahweh gave to Moses].
Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
4 Hezekiah told the people living in Jerusalem to give to the priests and the other descendants of Levi the portions [of meat] that should be given to them, in order that they could devote all their time to obeying the laws of Yahweh.
Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
5 As soon as he told that to the people, they generously gave the first part of their harvest of grain, and the first part of the new wine [that they produced], and [olive] oil and honey, and of the crops that grew in their fields. They brought [to the temple] a tenth of all their crops.
Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
6 The men of Israel and Judah who were living in various towns in Judah also brought a tenth of their cattle and sheep and goats, and a tenth of other things that they had dedicated to Yahweh their God, and they piled all those things in heaps.
Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
7 They started to do that in May and finished doing it in September.
Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
8 When Hezekiah and his officials saw the heaps, they praised Yahweh and [requested God to] bless the people.
Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
9 But Hezekiah asked the priests and other descendants of Levi, “Why are these heaps of things here?”
Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
10 Then Azariah the [Supreme] Priest, a descendant of Zadok, replied, “Since the time that the people started to bring their offerings to the temple, we have had even more food than we need. This has happened because Yahweh has greatly blessed our fellow Israelis, with the result that all this is left over [after we priests and other descendants of Levi took all that we need]!”
naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
11 Then Hezekiah ordered that they should prepare storerooms in the temple. So they did that.
Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
12 Then they brought into the storerooms all the tithes and offerings and the things dedicated to Yahweh [which the people had brought]. One of the descendants of Levi whose name was Conaniah was in charge of those things, and his [younger] brother Shimei was his assistant.
Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
13 Those two men supervised Jehiel, Azaziah, Nahath, Asahel, Jerimoth, Jozabad, Eliel, Ismakiah, Mahath and Benaiah while they did the work. They were appointed by King Hezekiah; Azariah was in charge of [everything that was done in] the temple.
Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
14 Kore the son of Imnah, another descendant of Levi, who guarded the east gate of the temple, was in charge of the offerings to God that were made voluntarily. He distributed to the priests and [other] descendants of Levi the offerings and other things that were dedicated to Yahweh.
Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
15 Eden, Miniamin, Jeshua, Shemaiah, Amariah and Shecaniah faithfully assisted him in the towns where the priests lived. They distributed those things to the groups of their fellow priests; they distributed them to everyone, from the youngest to the oldest.
Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
16 They also distributed things to the males who were at least 30 years old, those whose names were written on the scrolls where lists of family names were written. They were males who [were allowed to] enter the temple to perform their tasks/work each day, the tasks that each group had been assigned to do.
Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
17 The names of the priests were on the scrolls where their clans’ names were written. They also distributed things to groups of [other] descendants of Levi, those who were at least 20 years old.
Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
18 They included all their little children and wives and other sons and daughters whose names were on the scrolls where their clans’ names were written, because they also faithfully had dedicated themselves to Yahweh.
Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
19 [Hezekiah] also appointed other men to distribute portions of those offerings to the priests and other descendants of Levi who were living in the pasturelands around the towns in Judah. But they gave things only to those who were descendants of Aaron [the first Supreme Priest], whose names were on the scrolls containing the names of their clans.
Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
20 That is what Hezekiah did throughout Judah. He always faithfully did things that Yahweh his God considered to be right and good.
Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
21 In everything that he did for the worship in the temple, and as he obeyed God’s laws and commands, he tried to find out what his God wanted, and he worked energetically. So he was successful.
Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.