< 2 Chronicles 27 >
1 Jotham was 25 years old when he became the king of Judah. He ruled from Jerusalem for 16 years. His mother was Jerushah, the daughter of [the priest] Zadok.
Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
2 Jotham did many things that pleased Yahweh like his father Uzziah did. He obeyed Yahweh and did things that are right. He did many things that his father Uzziah had done, but he did not burn incense in the temple, like his father had done. However, the people of Judah continued to sin against Yahweh.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
3 Jotham’s [workers] rebuilt the Upper Gate of the temple, and they did a lot of work to repair the wall near Ophel [Hill].
Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
4 They built towns in the hills of Judah, and they built forts and defense towers in the forests.
Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
5 During the time that Jotham was the king of Judah, his army attacked and defeated the army of the Ammon people-group. Then, every year during the next three years, he required the Anmon people-group to pay to him four tons of silver, 60,000 bushels of wheat, and 60,000 bushels of barley.
Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
6 Jotham faithfully obeyed Yahweh his God, and as a result he became a very powerful king.
Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
7 A record of everything else that Jotham did during the time that he was the king, including the wars that his army fought, is written in the scroll called ‘[the History of] the Kings of Israel and Judah’.
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 After Jotham had ruled Judah for 16 years, he died when he was 41 years old.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
9 He was buried in Jerusalem, and his son Ahaz became the king [of Judah].
Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.