< 1 Samuel 25 >

1 [Soon after that], Samuel died, and all the Israeli people gathered and mourned for him. They buried his body outside his home in Ramah. Then David and his men moved to the Maon Desert.
Basi Samweli akafa, nao Israeli wote wakakusanyika na kumwombolezea; wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akateremka kwenye Jangwa la Maoni.
2 In Maon [town] there was a man who owned land in Carmel, [a nearby village]. He was very rich; he owned 3,000 sheep and 1,000 goats.
Mtu mmoja huko Maoni, aliyekuwa na makao huko Karmeli, alikuwa tajiri sana. Alikuwa na mbuzi elfu moja na kondoo elfu tatu, aliokuwa akiwakata manyoya huko Karmeli.
3 His name was Nabal; he was a descendant of Caleb. His wife Abigail was a wise and beautiful woman, but Nabal was very cruel and treated people very unkindly [IDM].
Jina la mtu huyo lilikuwa Nabali, naye mkewe aliitwa Abigaili. Alikuwa mwanamke mwenye busara na mzuri wa sura, lakini mumewe, ambaye alikuwa wa ukoo wa Kalebu, alikuwa mwenye hasira na mchoyo katika utendaji wake.
4 One day while David [and his men] were in the desert, someone told him that Nabal was cutting the wool from his sheep.
Daudi alipokuwa huko jangwani, akasikia kuwa Nabali alikuwa anakata kondoo manyoya.
5 So David told ten of his men, “Go to Nabal at Carmel and greet him for me.
Basi akatuma vijana kumi na kuwaambia, “Pandeni kwa Nabali huko Karmeli, mkamsalimie kwa jina langu.
6 Then tell to him this message from me, ‘I wish/desire that things will go well for you and your family and for everything that you possess.
Mwambieni: ‘Amani iwe kwako! Amani iwe kwako pamoja na wa nyumbani mwako! Pia amani iwe pamoja na vyote ulivyo navyo!
7 ‘heard people say that you are cutting the wool from your sheep. Previously, when your shepherds were among us, we did not harm them. All the time that your shepherds were among us at Camel, we did not steal any sheep from them.
“‘Nasikia kuwa huu ni wakati wa kukata kondoo manyoya. Wachunga mifugo wako walipokuwa pamoja nasi, hatukuwatendea mabaya na wakati wote waliokuwa huko Karmeli hakuna chochote chao kilipotea.
8 You can ask your servants if this is true, and they will tell you [that it is true]. We have come here at a time when you are celebrating, so I ask you to please be kind to us and give these men whatever extra food you have, for me, David, and my men to eat.’”
Waulize watumishi wako nao watakuambia. Kwa hiyo uwatendee wema vijana wangu, kwani tumekuja wakati wa furaha. Tafadhali wape watumishi wako na mwanao Daudi chochote kitakachokuja mkononi mwako kwa ajili yao.’”
9 When David’s men arrived where Nabal was, they gave David’s message to him, and they waited [for him to reply]. But Nabal spoke harshly to them.
Watu wa Daudi walipofika wakampa Nabali ujumbe huu kwa jina la Daudi. Kisha wakangojea.
10 He said to them, “Who [does] this man, this son of Jesse, [think that he] is? [DOU, RHQ] There are many slaves who are running away from their masters at the present time, [and it seems to me that he is just one of them].
Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Huyu Daudi ni nani? Huyu mwana wa Yese ni nani? Watumishi wengi wanakimbia kutoka kwa bwana zao siku hizi.
11 I give bread and water to the men who are cutting the wool from my sheep, and I give them meat from animals that I have slaughtered. Why should I take some of those things and give them to a group of outlaws [RHQ]? (Who knows where they have come from?/I do not even know where they have come from.)” [RHQ]
Kwa nini nichukue mkate wangu, maji yangu na nyama niliyochinja kwa ajili ya wakata manyoya wangu, na kuwapa watu ambao hakuna anayejua wanakotoka?”
12 Then David’s men returned and told him what Nabal had said.
Watu wa Daudi wakageuka na kurudi. Walipofika, wakaarifu kila neno.
13 When David heard that, he told his men, “[We are going to kill Nabal; ] fasten your swords!” So he fastened on his sword and about 400 men fastened on their swords and went with David. There were 200 of his men who stayed with their supplies.
Daudi akawaambia watu wake, “Jifungeni panga zenu!” Basi wakajifunga panga zao, naye Daudi akajifunga upanga wake. Watu kama mia nne hivi wakapanda pamoja na Daudi, na watu mia mbili wakabaki na vifaa.
14 One of Nabal’s servants [found out what David and his men were planning to do, so he] went to Nabal’s wife Abigail and said to her, “David sent some messengers from the desert to greet our master Nabal, but Nabal only yelled at them.
Mmoja wa watumishi akamwambia Abigaili, mkewe Nabali: “Daudi alituma wajumbe kutoka jangwani kumpa bwana wetu salamu zake, lakini akawavurumishia matukano.
15 All the time that we were in the fields close to them, those men of David were very kind to us. They did not harm us. They did not steal anything from us.
Hata hivyo watu hawa walikuwa wema sana kwetu. Hawakututendea mabaya, na wakati wote tulipokuwa nje huko mashambani karibu nao, hatukupotewa na kitu chochote.
16 They protected us during the daytime and during the night. They were like a wall [MET] around us to protect us while we were taking care of our sheep.
Usiku na mchana walikuwa ukuta wakituzunguka wakati wote tulipokuwa tukichunga kondoo zetu karibu nao.
17 So now you should think about it and decide what you can do. [If you do not do something, ] terrible things will happen to our master and to all his family. Nabal is an extremely wicked man, with the result that [he will not heed anyone when] that person tries to tell him anything [that he should do].”
Sasa fikiri juu ya jambo hili na uone unaweza kufanya nini, kwa sababu maafa yanakaribia juu ya bwana wetu na nyumba yake yote. Yeye ni mtu mwovu kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kuzungumza naye.”
18 [When] Abigail [heard that, she] very quickly gathered 200 loaves [of bread], and also got two leather bags full of wine, the meat from five sheep, a bushel of roasted grain, 100 packs of raisins, and 200 packs of dried figs. She put all those things on donkeys.
Abigaili akafanya haraka, akachukua mikate mia mbili, viriba viwili vya divai, kondoo watano waliochinjwa vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu kavu, mikate mia mbili ya tini, akavipakia juu ya punda.
19 Then she told her servants, “Go ahead of me. I will follow you.” But she did not tell her husband [what she was going to do].
Kisha akawaambia watumishi wake, “Tangulieni; mimi nitakuja nyuma yenu.” Lakini hakumwambia Nabali mumewe.
20 David and his men [had left the place where they were staying and were on the road to Nabal’s property. They] were coming down a hill when they met Abigail.
Ikawa alipokuwa amepanda punda wake kwenye bonde la mlima, tazama, Daudi na watu wake wakawa wanateremka kumwelekea, naye akakutana nao.
21 David had been saying to his men, “It was useless for us to protect that man and all his possessions here in this desert. We did not steal anything that belonged to him, but he has done evil to me in return for our good [things we did for him].
Daudi alikuwa amesema, “Ilikuwa ni kazi bure kuchunga kwangu kote mali za huyu mtu huko jangwani hivi kwamba hakuna chochote chake kilichopotea. Yeye amenilipa baya kwa ajili ya wema.
22 I hope/desire that God will strike me and kill me [IDM] if he or even one of his men [IDM] is still alive tomorrow morning!”
Bwana na amshughulikie Daudi, tena kwa ukali, ikiwa kesho asubuhi nitambakizia mwanaume hata mmoja aliye hai miongoni mwa watu wake wote!”
23 When Abigail saw David, she quickly got down from her donkey and bowed before him, with her face touching the ground.
Abigaili alipomwona Daudi, akashuka haraka kwenye punda wake, akainama kifudifudi uso wake mpaka nchi mbele ya Daudi.
24 Then she prostrated herself at David’s feet and said to him, “Sir, I deserve to be punished [for what my husband has done]. Please listen to what I say to you.
Akamwangukia miguuni pake na kusema: “Bwana wangu, kosa hili na liwe juu yangu mwenyewe. Tafadhali mruhusu mtumishi wako aseme nawe. Sikia kile mtumishi wako atakachosema.
25 Please do not pay attention to [IDM] what this worthless man Nabal has said. His name means ‘fool’, and he surely is a foolish man. But I, who am [willing to be] your servant, did not see the messengers whom you sent to him.
Bwana wangu na asimjali huyo mtu mwovu Nabali. Yeye anafanana na jina lake; jina lake ni Mpumbavu, nao upumbavu huenda pamoja naye. Lakini kwangu mimi, mtumishi wako, sikuwaona hao watu waliotumwa na bwana wangu.
26 Yahweh has prevented you from getting revenge on anyone and killing anyone. I hope/desire that as surely as Yahweh lives and as surely as you live, your enemies will be [cursed] like Nabal will be.
“Basi sasa, kwa kuwa Bwana amekuzuia, wewe bwana wangu, kutokumwaga damu na kutolipiza kisasi kwa mikono yako mwenyewe, hakika kama Bwana aishivyo na kama uishivyo, maadui zako na wote wanaokusudia kumdhuru bwana wangu wawe kama Nabali.
27 I have brought a gift for you and for the men who are with you.
Nayo zawadi hii ambayo mtumishi wako amemletea bwana wangu, wapewe watu wanaofuatana nawe.
28 Please forgive me if I have done anything wrong to you. Yahweh will surely [reward you by] allowing many of your descendants to become kings of Israel, because you are fighting the battles that Yahweh [wants you to fight]. And [I know that] throughout all your life you have not done anything wrong.
Tafadhali samehe kosa la mtumishi wako, kwa kuwa Bwana kwa hakika ataifanya imara nyumba ya ufalme kwa bwana wangu, kwa sababu anapigana vita vya Bwana.
29 Even when those who are trying to kill you pursue you, you are safe, because Yahweh your God takes care of you. You will be [protected as though you were] [MET] a bundle that he has safely tied up. But your enemies will [disappear as fast as stones] that are hurled from a sling.
Hata ingawa yuko mtu anayekufuatia kuuondoa uhai wako, usiruhusu baya lolote kuonekana kwako siku zote za maisha yako, uhai wa bwana wangu utafungwa salama kwenye furushi la walio hai na Bwana Mungu wako. Lakini uhai wa adui zako atavurumishwa kama vile jiwe kutoka kwenye kombeo.
30 Yahweh has promised to do good things for you, and he will do what he has promised. And he will cause you to become the ruler of the Israeli people.
Bwana atakapokuwa ameshamtendea bwana wangu kila kitu chema alichoahidi kumhusu yeye na kumweka kuwa kiongozi wa Israeli,
31 When that happens, [you will be glad that you did not kill any] people in Nabal’s household. You will not think that you deserve to be punished for having taken revenge yourself and killed innocent people. And when Yahweh enables you to successfully [become the king], please do not forget [to be kind to] me.”
bwana wangu hatakuwa na dhamiri inayolemewa na mzigo kwa kumwaga damu kusiko na sababu, au kujilipizia kisasi yeye mwenyewe. Bwana atakapomletea bwana wangu mafanikio, umkumbuke mtumishi wako.”
32 David replied to Abigail, “I praise Yahweh, the God whom we Israelis [worship], because he sent you to [talk with] me.
Daudi akamwambia Abigaili, “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli aliyekutuma kunilaki leo.
33 I hope/desire that Yahweh will bless you for being very wise. You have prevented me from taking revenge myself and killing many people [MTY] today.
Ubarikiwe kwa uamuzi wako mzuri na kwa kunizuia nisimwage damu leo na kulipiza kisasi kwa mikono yangu.
34 Just as surely as Yahweh the God whom we Israelis [worship] is alive, he has prevented me from harming you. If you had not come quickly to talk to me, neither Nabal nor even one of Nabal’s men [IDM] would be still alive tomorrow morning.”
La sivyo, hakika kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisiwadhuru, kama usingekuja haraka kunilaki, hakuna hata mwanaume mmoja wa Nabali angeachwa hai kufikia mapambazuko.”
35 Then David accepted the gifts that Abigail had brought to him. He said to her, “I hope/desire that things will go well for you. I have heard what you said, and I will do what you have requested.”
Ndipo Daudi akapokea kutoka mkononi mwake kile alichokuwa amemletea, naye akasema, “Nenda nyumbani kwako kwa amani; nimesikia maneno yako na kukujalia ombi lako.”
36 When Abigail returned to Nabal, he was in his house, having a big celebration like kings have. He was very drunk and feeling very happy. So Abigail did not say anything to him that night [about her meeting with David].
Abigaili alipokwenda kwa Nabali, alikuwa ndani ya nyumba yake akifanya karamu kama ile ya mfalme. Naye alikuwa ana furaha nyingi, akiwa amelewa sana. Kwa hiyo Abigaili hakumwambia mumewe kitu chochote mpaka asubuhi yake.
37 The next morning, when he was no longer drunk, she told him everything [that had happened when she talked with David]. [Immediately] (he had a stroke/a blood vessel burst in his brain) and he became paralyzed [MET].
Basi asubuhi, Nabali alipokuwa amelevuka, mkewe akamwambia mambo yote, nao moyo wake ukazimia, akawa kama jiwe.
38 About ten days later Yahweh struck him [again] and he died.
Baada ya siku kumi, Bwana akampiga Nabali, naye akafa.
39 After David heard that Nabal was dead, he said, “Praise Yahweh! Nabal insulted me, but Yahweh (vindicated me/got revenge for me). He has prevented me from [doing anything] wrong. And he has punished Nabal for the wrong that he did.” Then David sent [messengers] to Abigail, to ask her if she would become his wife.
Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “Ahimidiwe Bwana, ambaye amenitetea shauri langu dhidi ya Nabali kwa kuwa alinitendea kwa dharau. Amemzuia mtumishi wake asitende mabaya na Bwana ameuleta ubaya wa Nabali juu ya kichwa chake mwenyewe.” Kisha Daudi akatuma ujumbe kwa Abigaili kumwomba awe mke wake.
40 His servants went to Carmel and said to Abigail, “David sent us to take you to become his wife.”
Watumishi wa Daudi wakaenda mpaka Karmeli na kumwambia Abigaili, wakisema, “Daudi ametutuma kwako kukuchukua uwe mkewe.”
41 Abigail bowed down with her face touching the ground. Then she told [the messengers to tell David], “[I am happy to become your wife]. I will be your servant. And I am willing to wash the feet of your slaves.”
Akainama chini uso wake mpaka ardhini, akasema, “Mjakazi wako yuko hapa, tayari kuwatumikia na kuwanawisha miguu watumishi wa bwana wangu.”
42 Abigail quickly got on her donkey and went with David’s messengers. Five of her maids went with her. [When she arrived where David was, ] she became his wife.
Abigaili akainuka kwa haraka, akapanda punda wake, akihudumiwa na wajakazi wake watano, akaenda pamoja na wajumbe wa Daudi, naye akawa mkewe.
43 David had previously married Ahinoam, a woman from Jezreel [town near Carmel]. So both Abigail and Ahinoam were now David’s wives.
Pia Daudi alikuwa amemwoa Ahinoamu wa Yezreeli, wote wawili wakawa wake zake.
44 King Saul’s daughter Michal was also David’s wife, but Saul had given her to Laish’s son Paltiel, who was from Gallim [town].
Lakini Sauli alikuwa amemwoza Mikali binti yake, aliyekuwa mkewe Daudi, kwa Palti mwana wa Laishi, kutoka Galimu.

< 1 Samuel 25 >