< 1 Samuel 19 >
1 Then Saul urged all his servants and his son Jonathan to kill David. But Jonathan liked David very much.
Sauli akamwambia Yonathani mwanawe na watumishi wake wote kwamba wanapaswa kumuua Daudi. Lakini Yonathani, mwana wa Sauli, alitamani sana akae na Daudi.
2 So he warned David, “My father Saul is seeking for a way to kill you. So be careful. Tomorrow morning go and find a place to hide [in the field].
Hivyo Yonathani akamwambia Daudi, “Baba yangu Sauli anatafuta kukuua. Kwa hiyo uwe macho wakati wa asubuhi na jifiche mahali pa siri.
3 I will ask my father to go out there with me. [While we are out there], I will talk to him about you. Then I will tell you everything that he tells me.” [So David did what Jonathan told him to do].
Nami nitatoka nje na kusimama kando ya baba yangu huko shambani uliko wewe, na nitazungumza na baba yangu kuhusu wewe. Kama nikijua jambo lolote nitakuambia.”
4 [The next morning], Jonathan spoke with his father, saying many good things about David. He said, “You should never do anything to harm your servant David! He has never done anything to harm you! Everything that he has done has helped you very much.
Yonathani alimsifia Daudi mbele ya Sauli baba yake akisema, “Mfalme asije akafanya dhambi dhidi ya mtumishi wake Daudi. Maana yeye hajakutenda dhambi, mambo aliyofanya yamekusaidia sana.
5 He was in danger of being killed when he fought against [Goliath, the champion of] the Philistia [army. By enabling David to kill him], Yahweh won a great victory for all the people of Israel. You were very happy when you saw that. Why would you want to do anything now to harm David [RHQ]? There is no reason for you to kill him, because he has not done anything wrong!”
Maana alijitoa maisha yake na kumuua yule Mfilisti, naye BWANA akawaletea Waisraeli wote wokovu mkuu. Tena uliuona na kufurahi. Kwa nini utende dhambi juu damu isiyo na hatia kwa kumuua Daudi bila sababu?”
6 Saul listened to what Jonathan said. Then Saul said, “I solemnly promise that just as certain as Yahweh lives, I will not kill David.”
Sauli alimsikiliza Yonathani. Sauli akaapa, “Kama BWANA aishivyo, Yonathani hatauawa.”
7 Afterward, Jonathan summoned David and told him what he and Saul had said. Then Jonathan brought David to Saul, and David served Saul as he had done before.
Ndipo Yonathani akamwita Daudi na kumwambia mambo hayo yote. Na Yonathani akamleta Daudi kwa Sauli, naye Daudi akawa mbele zake kama zamani.
8 One day a war started again, and David [led his soldiers to] fight against the Philistia army. David’s [army] attacked them very furiously, with the result that the Philistia army ran away.
Baadaye kukawa na vita tena. Daudi akatoka na kupigana na Wafilisti na kuwashinda kwa mauaji makubwa mno. Nao wakakimbia mbele yake.
9 But one day when sitting in his house, an evil spirit [sent] from Yahweh [suddenly] came upon Saul. While David was playing his harp [for Saul],
Yule roho wa ubaya kutoka kwa BWANA ikamjia Sauli alipokuwa ameketi nyumbani mwake na mkuki mkononi mwake, na Daudi akiwa anapiga chombo chake.
10 Saul hurled his spear at David to try to fasten him to the wall. David (dodged/jumped to one side), and the spear did not hit him. The spear stuck in the wall, but that night David escaped.
Sauli alijaribu kumpigilia Daudi ukutani kwa mkuki wake, lakini akaponyoka kutoka machoni pake, na kwamba Sauli akashindilia mkuki ndani ya ukuta. Daudi alikimbia na kutoroka usiku huo.
11 Then Saul sent messengers to David’s house. He told them to watch the house and to kill David [while he was leaving the house] the following morning. But David’s wife Michal [saw them and] warned him, “To survive, you must run away tonight, because if you do not do that, you will be killed tomorrow!”
Bado Sauli aliwatuma wajumbe nyumbani kwa Daudi wamvizie kusudi aweze kumuua asubuhi. Mkewe Daudi, Mikali, akamwambia, “Usipoyaokoa maisha yako usiku huu, kesho utauwawa.”
12 So she enabled David to climb out through a window, and he ran away and escaped.
Hivyo Mikali akamteremsha Daudi kupita dirishani. Naye akaenda, akakimbia na kutoroka.
13 Then Michal took an idol and put it in the bed. She covered it with some [of David’s] clothes, and put some goat’s hair on the head of the idol.
Mikali alichukua kinyago na kukilaza juu ya kitanda. Kisha akaweka mto wa singa za mbuzi kichwani pake, na akakifunika na nguo.
14 When the messengers came [to the house the next morning], she told them that David was sick [and could not get out of bed].
Sauli alipowatuma wajumbe kumchukua Daudi, mkewe akasema, “Daudi ni mgonjwa.”
15 [When they reported that to] Saul, he told them to go back to David’s house. He said to them, “Bring him to me lying on his bed, in order that I can kill him!”
Kisha Sauli akawatuma wajumbe kumtazama; akisema, “Mleteni kwangu akiwa kitandani, ili nimuue.”
16 But when those men entered David’s house, they saw that there was only an idol in the bed, with goat’s hair on its head.
Wale wajumbe walipoingia ndani, tazama, kile kinyago kilikuwa kitandani pamoja na mto wa singa za mbuzi kichwani.
17 [When they reported that to Saul, ] Saul [summoned] Michal [and] said to her, “Why did you trick me like that? You allowed my enemy to escape!” Michal replied to Saul, “David told me that if I did not help him escape, he would kill me!” [RHQ]
Sauli akamuuliza Mikali, “Kwa nini umenidanganya na kumwachilia adui yangu aende, na tena ametoroka?” Mikali akamjibu Sauli, “Aliniambia, 'Acha niende. Kwa nini nikuuwe?”'
18 After David had escaped from Saul, he went to Samuel, who was [at his home] at Ramah. He told Samuel everything that Saul had done to [try to kill] him. Then David and Samuel went to Naioth, [which was a section] of [Ramah city], and they stayed there.
Basi Daudi akakimbia na kutoroka, na akaenda kwa Samweli huko Rama na kumweleza yote ambayo Sauli amemtendea. Ndipo yeye na Samweli wakaenda na kukaa Nayothi.
19 Someone told Saul that David was in Naioth.
Naye Sauli akaambiwa kwamba, “Tazama, Daudi yuko huko Nayothi iliyoko Rama.”
20 So Saul sent some messengers to capture David. [When] those messengers [arrived in Ramah, they] met some men who were proclaiming ecstatic messages, and Samuel was there, as their leader. When Saul’s messengers met them, the Spirit of God took control of Saul’s men, and they also spoke ecstatically.
Kisha Sauli akawatuma wajumbe kumkamata Daudi. Nao walipowaona kundi la manabii wakitabiri, na Samweli akisimama kama kiongozi wao, Roho wa Mungu akawaingia wale wajumbe wa Sauli, nao pia wakatabiri.
21 When Saul heard about that, he sent messengers a third time, but they also started to speak ecstatically.
Sauli alipoambiwa hivyo, akawatuma wajumbe wengine, nao pia wakatabiri. Basi Sauli aliwatuma tena wajumbe kwa mara ya tatu, na hao pia wakatabiri.
22 Finally, Saul himself went to Ramah. When he arrived at the well at [a place named] Secu, he asked people there, “Where are Samuel and David?” The people replied, “They are at Naioth in Ramah [city].”
Kisha naye akaenda Rama na kufika katika kisima kirefu kilichoko huko Seku. Akauliza, “Samweli na Daudi wako wapi?” Mtu mmoja akasema, “Angalia, Wako Nayothi huko Rama.”
23 While Saul was walking toward Naioth, the Spirit of God also took control of him. [While he walked on], he continued speaking ecstatic messages until he came to Naioth.
Hivyo Sauli akaenda Nayothi huko Rama. Ndipo Roho wa Mungu pia akaja juu yake, naye alipokuwa akienda alitabiri, hadi alipofika Nayothi huko Rama.
24 There he took off his clothes, and he spoke messages from God in front of Samuel. He lay on the ground doing that all day and all night. That is the reason that [when people see someone doing something that is very unexpected, they think about what happened to Saul, and] they say, “We are surprised, like the people were surprised to see Saul [acting like] a prophet?” [RHQ]
Na yeye pia, alirarua mavazi yake, naye pia akatabiri mbele ya Samweli siku hiyo akilala uchi mchana kutwa na usiku kucha. Kwa sababu ya jambo hili, watu husema, “Je, Sauli pia ni miongoni mwa manabii?”